Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tarehe 1-7/4

ZABURI 23-25

Tarehe 1-7/4

Wimbo 4 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. “Yehova ni Muchungaji Wangu”

(Dak. 10)

Yehova anatuongoza (Zb 23:1-3; w11-SW 1/5 uku. 31 fu. 3)

Yehova anatulinda (Zb 23:4; w11-SW 1/5 uku. 31 fu. 4)

Yehova anatulisha (Zb 23:5; w11-SW 1/5 uku. 31 fu. 5)

Yehova anahangaikiaka watumishi wake sawa vile muchungaji anahangaikiaka kondoo wake.

UJIULIZE, ‘Namna gani Yehova amenihangaikia kipekee?’

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 23:3—“Njia za haki” njo nini, na nini njo itatusaidia tusiziache? (w11-SW 15/2 uku. 24 fu. 1-3)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Zungumuzia kweli fulani ya Biblia na mutu mwenye anakuambia kama hali ya mazingira iko namuhangaisha. (lmd somo ya 2 nukta ya 5)

5. Kuendelesha Mazungumuzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YA NYUMBA KWA NYUMBA. Tembelea mutu mwenye aliitika broshua Furahia Maisha Milele! Na umuonyeshe namna tunajifunzaka Biblia na watu. (lmd somo ya 9 nukta ya 3)

6. Kufanya Wanafunzi

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 54

7. Tunakatala Kusikiliza Sauti ya Wageni

(Dak. 15) Mazungumuzo.

Kondoo wanasikiaka sauti ya muchungaji wao na kumufuata. Lakini wanakimbiaka wakati wanasikia mugeni mwenye hawajue sauti yake. (Yoh 10:5) Vilevile, tunasikilizaka wachungaji wetu wa kiroho wenye kutupenda na wenye kutumainika, Yehova na Yesu. (Zb 23:1; Yoh 10:11) Lakini tunakatala kusikiliza sauti ya wageni wenye wanapenda kufanya imani yetu ikuwe zaifu kupitia “maneno ya uongo.”—2Pe 2:1, 3.

Mwanzo sura ya tatu inatusaidia kujua mara ya kwanza yenye sauti ya mugeni ilisikilikaka ku dunia. Shetani alizungumuzaka na Eva kupitia nyoka juu Eva asimujue. Alijifanya kuwa sawa rafiki, akapotosha maneno yenye Yehova alisemaka na kufanya ionekane sawa vile Yehova alikuwa na nia ya mubaya juu ya wanadamu. Kwa kuhuzunisha, Eva alimusikiliza na ile ikamuletea yeye na familia yake mateso ya mingi sana.

Leo Shetani anajikaza kufanya watu wakuwe na mashaka juu ya Yehova na tengenezo yake kwa kueneza habari za mubaya, habari zenye haziko za kweli kabisa, na pia habari za uongo. Kama tunasikia sauti ya mugeni tunapaswa kukimbia! Kusikiliza, hata kwa wakati kidogo juu tu ya kupenda kujua mambo yenye wanasemaka, ni hatari. Usisahau kama Shetani alisemaka tu maneno kidogo wakati alimudanganyaka Eva. (Mwa 3:1, 4, 5) Lakini sasa, tutafanya nini kama mutu mwenye tunajua, mwenye anatupendaka na mwenye iko na nia ya muzuri—anapenda kutuambia habari fulani ya mubaya juu ya tengenezo ya Yehova?

Muangalie VIDEO Usisikilize Hata Kidogo “Sauti ya Wageni.” Kisha uulize wasikilizaji:

Umejifunza nini kupitia namna Rose alitenda wakati mama yake alipenda kumuambia habari fulani ya mubaya juu ya tengenezo ya Yehova?

8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 55 na Sala