Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Habari Mupya ili Kuanzisha Mazungumuzo

Habari Mupya ili Kuanzisha Mazungumuzo

Tangu Mwezi wa 1, 2016, ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi umekuwa na habari yenye kichwa “Biblia Inasema Nini?” Kusudi la habari hii ni kutusaidia kuanzisha mazungumuzo juu ya habari zenye kutegemea Biblia. Habari hiyo inaandikwa kwa namna moja na trakte zetu. Kuna ulizo lenye kumuchochea mutu atoe mawazo yake, kisha kunakuwa andiko lenye kutoa jibu, na mambo mengine kwa ajili ya mazungumuzo.

Mara nyingi, mazungumuzo mazuri kuhusu habari zenye kutegemea Biblia yanaongoza kwenye funzo la Biblia. Tumia habari hiyo mupya ili kusaidia watu wengi zaidi watosheleze njaa yao ya kiroho.—Mt 5:6.

NAMNA YA KUTUMIA HABARI HIYO:

  1. Uliza mawazo ya musikilizaji kuhusu ulizo moja kati ya maulizo hayo

  2. Usikilize na ushukuru musikilizaji kwa jibu lake Soma andiko yenye kuwa chini ya kichwa kidogo “Mambo Biblia Inasema,” na umuulize mawazo yake juu ya andiko hiyo. Kama iko na wakati, uendelee na mazungumuzo kwa kutumia nukta moja chini ya kichwa kidogo “Biblia Inatufundisha Tena Nini?”

  3. Umutolee gazeti

  4. Upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo la pili