UTAJIRI WA NENO LA MUNGU
Ayubu Alipinga Mawazo Mabaya
Leo,Shetani anatumia uwongo ili kuwavunja moyo watumishi wa Yehova. Tuone tofauti kati ya uwongo wa Shetani na namna Yehova anajisikia kabisa kama vile inaonyeshwa katika kitabu cha Ayubu. Utafute maandiko mengine katika Biblia yenye kuonyesha kwamba Yehova anakuhangaikia kabisa.
UWONGO WA SHETANI |
NAMNA YEHOVA ANAJISIKIA KABISA |
---|---|
Mungu anawaomba watumishi wake mambo mengi sana hivi kwamba hatosheke na yenye wanafanya. Hakuna mutu mwenye anaweza kumupendeza (Ayu 4:18; 25:5) |
Yehova anapendezwa sana wakati tunajikaza kuwa waaminifu (Ayu 36:5) |
Mwanadamu hana faida yoyote kwa Mungu (Ayu 22:2) |
• Yehova anakubali na anabariki utumishi wenye tunamutolea kwa uaminifu (Ayu 33:26; 36:11)) |
Mungu haangaikie uaminifu wa watu (Ayu 22:3) |
Yehova anapendezwa na watu waaminifu (Ayu 36:7) |