BUKU YA MUKUTANO UTUMISHI NA MAISHA YA MUKRISTO Mwezi wa 4, 2017

Namna ya Kuanzisha Mazungumuzo

Namna ya kutoa gazeti Amuka! na fundisho la kweli la Biblia juu ya Ufalme wa Mungu. Fuata mifano hiyo ili kuandika namna yako ya kuanzisha mazungumuzo.

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU

Kubali Yehova Afinyange Mawazo na Mwenendo Wako

Mufinyanzi Mukubwa anatufinyanga ili sifa zetu za kiroho zikuwe muzuri zaidi, lakini sisi pia tunapaswa kukubali atufinyange.

MAISHA YA MUKRISTO

Tuwakaribishe kwa Furaha

Kila mutu mwenye anahuzuria mikutano yetu anapaswa kujionea upendo wetu wa Kikristo. Unaweza kufanya nini ili wajionee upendo huo?

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU

Je, Una ‘Moyo wa Kumujua’ Yehova?

Katika Yeremia sura ya 24, Yehova Mungu alilinganisha watu na tini. Ni nani walilinganishwa na tini za muzuri, na namna gani tunaweza kuwaiga leo?

MAISHA YA MUKRISTO

Unaweza Kutia Moyo Wahubiri Wenye Hawatende Tena

Wahubiri wenye hawatende tena wangali wa lazima sana kwa Yehova Mungu. Namna gani tunaweza kuwasaidia wamurudilie Yehova?

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU

Ukuwe na Ujasiri Kama Yeremia

Yeremia alitabiri kwamba muji wa Yerusalemu utaharibiwa. Ni nini ilimusaidia aendelee kuwa na ujasiri?

MAISHA YA MUKRISTO

Nyimbo za Ufalme Zinaleta Nguvu

Kuimba nyimbo za Ufalme kulitia nguvu ndugu na dada katika kambi ya mateso ya Sachsenhausen. Nyimbo hizo zinaweza kututia pia nguvu wakati tunapambana na majaribu.

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU

Yehova Alitabiri Agano Jipya

Agano jipya linatofautiana namna gani na agano la Sheria, na ni katika njia gani baraka zenye agano jipya linaleta ni za milele?