Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Unaweza Kutia Moyo Wahubiri Wenye Hawatende Tena

Unaweza Kutia Moyo Wahubiri Wenye Hawatende Tena

Kila mwaka, wahubiri wengi wenye hawatende tena wanahuzuria Ukumbusho. Walianza kukimbia shindano la mbio la uzima lakini wameregeza mwendo kwa sababu mbalimbali; sababu fulani zinapatikana katika broshua Umurudilie Yehova. (Ebr 12:1) Lakini, kwa sababu Yehova aliwanunua kwa damu ya Mutoto yake, wangali wa lazima sana kwake. (Mdo 20:28; 1Pet 1:18, 19) Namna gani tunaweza kuwasaidia wamurudilie Yehova?

Muchungaji anatafuta kwa uangalifu kondoo mwenye amepotea; vilevile wazee wanajikaza sana kutafuta na kusaidia wahubiri wenye hawatende tena. (Lu 15:4-7) Hilo linaonyesha kama Yehova anawahangaikia sana. (Yer 23:3, 4) Sisi wote tunaweza kutia moyo Wahubiri hao, haiko wazee tu. Yehova anafurahi wakati anaona tunajikaza sana ili kuwaonyesha wema na kujitia pa nafasi yao; na hilo linaweza kutuletea baraka nyingi sana. (Met 19:17; Mdo 20:35) Kwa hiyo, fikiria Wahubiri wenye unaweza kutia moyo, na usikawie kuwasaidia!

MUANGALIE VIDEO TUTIE MOYO WAHUBIRI WENYE HAWATENDE TENA, KISHA MUJIBIE MAULIZO HAYA:

  • Dada Abbey alifanya nini wakati alikutana na Shahidi mwenye hajue?

  • Kama tunapenda kusaidia muhubiri fulani mwenye hatende tena, sababu gani tunapaswa kwanza kuona wazee?

  • Namna gani dada Abbey alijitayarisha ili kumutembelea tena Laura?

  • Namna gani dada Abbey aliendelea kuonyesha uvumilivu na upendo wakati alikuwa anajaribu kumusaidia Laura?

  • Mufano wa Yesu katika Luka 15:8-10 unaweza kutufundisha nini?

  • Dada Abbey alipata Baraka gani kwa kujikaza kumusaidia Laura?