Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Tuwakaribishe kwa Furaha

Tuwakaribishe kwa Furaha

Watu gani? Watu wote wenye wanahuzuria mikutano yetu ya Kikristo, iwe ni wapya ao wenye tunajua tangu zamani. (Rom 15:7; Ebr 13:2) Inaweza kuwa ndugu ao dada mwenye anatutembelea kutoka inchi ingine ao Mukristo mwenye anafika kwenye mikutano kisha kukosekana miaka mingi. Wazia namna unaweza kujisikia kama wewe ndiye Mukristo huyo. Ni wazi kwamba utapenda wakupokee kwa furaha. (Mt 7:12) Kwa hiyo, tunapaswa kujikaza kuzunguka katika Jumba la Ufalme mbele na kisha mikutano ili kusalimia watu. Hilo linafanya watu wachangamukiane na kuonyeshana upendo, na linamuletea Yehova utukufu. (Mt 5:16) Kusema kweli, pengine haitawezekana kuzungumuza na kila mutu. Hata hivyo, watu watafurahi ikiwa tunajikaza kuwakaribia. *

Tunapaswa kukaribisha watu kwa furaha kila wakati, haiko tu nyakati za pekee, kama vile wakati wa Ukumbusho. Wakati wapya wanajionea upendo wa Kikristo, wanaweza kuchochewa kumusifu Mungu na kujiunga na sisi ili kumuabudu pamoja.—Yoh 13:35.

^ fu. 3 Kanuni za Biblia zinaonyesha waziwazi kama hatupaswe kusalimia watengwa hata wakati wanafika kwenye mikutano.—1Kor 5:11; 2Yoh 10.