MAISHA YA MUKRISTO
Nini Njo Ninaona Kuwa ya Maana Zaidi?
Yakobo alipigana na malaika ili apate jambo fulani la maana sana, ni kusema, baraka ya Yehova. (Mwa 32:24-31; Ho 12:3, 4) Je, sisi pia tuko tayari kujikaza sana ili kumutii Yehova na kupata baraka yake? Kwa mufano, tutachagua nini kati ya kuhuzuria mukutano wa kutaniko na kutumika saa fulani za zaidi kisha kazi yetu ya kimwili? Kama tunamutolea Yehova wakati wetu, nguvu yetu, na mali yetu, atatumuangia “baraka mupaka kusikuwe kitu chenye kitakosa.” (Mal 3:10) Atatuongoza, atatulinda, na kutusaidia kupata mambo yenye tuko nayo lazima.—Mt 6:33; Ebr 13:5.
-
Namna gani dada alijaribiwa na jambo lenye alikuwa anapenda?
-
Namna gani kazi yetu ya kimwili inaweza kuwa jaribu kwetu?
-
Juu ya nini Timoteo alipaswa kuendelea kujiwekea miradi hata kama tayari alikuwa Mukristo mwenye kukomaa Kiroho?—1Ti 4:16
-
Namna gani tunaweza kuonyesha ni kazi gani tunaona kuwa ya maana zaidi?