MAISHA YA MUKRISTO
“Upendo . . . Haufurahie Ukosefu wa Haki”
Mu mambo yote yenye Wakristo wanafanyaka, wanajikazaka kuacha upendo uwaongoze. Upendo “haufurahie ukosefu wa haki.” (1Ko 13:4, 6) Kwa hiyo, tunaepuka mambo ya kujifurahisha yenye inasifu uasherati na jeuri. Pia, hatufurahi wakati wengine wanapatwa na mambo ya mubaya, hata kama ni wale wenye walituumiza.—Mez 17:5.
MUANGALIE VIDEO KUMBUKA NAMNA UPENDO UNAJIENDESHA—HAUFURAHIE UKOSEFU WA HAKI, KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
-
Daudi alitenda namna gani wakati alipata habari kama Sauli na Yonatani wamekufa?
-
Ni wimbo gani wa huzuni wenye Daudi alitunga kwa ajili ya Sauli na Yonatani?
-
Juu ya nini Daudi hakufurahi wakati Sauli alikufa?