Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Uko Tayari Kupambana na Muvurugo Wenye Unaweza Kutokea mu Eneo Yenu?

Uko Tayari Kupambana na Muvurugo Wenye Unaweza Kutokea mu Eneo Yenu?

Kadiri mwisho ya hii ulimwengu inakaribia, tunatazamia kama muvurugo, ugaidi na vita vitaongezeka. (Ufu 6:4) Namna gani tunaweza kujitayarisha kuhusu magumu ya wakati wenye kuya?

  • Kujitayarisha kiroho: Tafuta kanuni na habari zenye kuwa mu Biblia zenye zinaweza kukusaidia umutegemee kabisa Yehova na tengenezo yake, na zenye zinaweza kukusaidia usiunge mukono upande wowote. (Mez 12:5; jr-SW uku. 125-126 fu. 23-24) Hii njo wakati ya kufanya urafiki wa nguvu pamoya na ndugu na dada mu kutaniko.​—1Pe 4:7, 8

  • Kujitayarisha kimwili: Kama hauwezi kutoka ku nyumba, ujitayarishe juu ya kuwa salama na utayarishe vitu vya kutosha vyenye unaweza kuwa navyo lazima. Tena, ufikirie mambo yenye unaweza kufanya kama ni lazima kutoka ku nyumba. Angalia vitu vyenye viko mu sakoshe yako ya kukimbia nayo, na usisahau makuta na vitu vyenye unaweza kutumia ili kujilinda. Upatie wazee namba yako ya telefone na weye ukuwe na namba zao.​—Isa 32:2; g17.5 uku. 3-7

Wakati muvurugo unatokea, uendelea kufanya mambo ya kiroho. (Flp 1:10) Epuka kutoka-toka kama haiko lazima. (Mt 10:16) Utumie pamoya na wengine chakula na vitu vingine vyenye uko navyo.​—Ro 12:13.

MUANGALIE VIDEO UKO TAYARI KWA AJILI YA MUSIBA? NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Yehova anaweza kutusaidia namna gani wakati musiba inatokea?

  • Ni mambo gani yenye tunaweza kufanya ili kujitayarisha?

  • Tunaweza kufanya nini ili kusaidia wenye wanafikiwa na musiba?