Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Ujione Vile Yehova Anakuona

Ujione Vile Yehova Anakuona

“Yehova anafurahia watu wake.” (Zb 149:4) Hata kama hatukamilike, Yehova anaonaka sifa zetu za muzuri na mambo ya muzuri yenye tunaweza kufikia kufanya. Lakini, wakati fulani inaweza kuwa nguvu kwetu kuona sifa za muzuri zenye tuko nazo. Wakati fulani, tunaweza kujiona kuwa hatuko wa maana kwa sababu ya namna watu wanatutendea. Ao kama tunakazia akili makosa yetu ya zamani, tunaweza kushakia kama Yehova anatupenda. Nini inaweza kutusaidia ikiwa tuko na mawazo ya vile?

Kumbuka kama Yehova anaonaka mambo yenye wanadamu hawawezi kuona. (1Sa 16:7) Ile inamaanisha kama Yehova anaonaka mambo yenye hata siye wenyewe hatuonake ndani yetu. Tuko wenye shukrani kwa sababu Biblia inatusaidia kuelewa namna Yehova anatuonaka. Tunaelewa ile wakati tunasoma maandiko na habari za Biblia zenye kuonyesha namna Yehova anapenda watu wake.

MUANGALIE VIDEO HAKIKISHIA MOYO WAKO MBELE YA YEHOVA, NA KISHA MUJIBIE MAULIZO YENYE KUFUATA:

  • Mufano wa ule kijana mwenye kukimbia na baba yake unatufundisha nini juu ya namna Yehova anatuona?

  • Kama mutu mwenye amefanya zambi nzito amekamata hatua zote zenye zinaombwa juu ya kurudisha urafiki wake na Yehova, namna gani anaweza kuhakikishia moyo wake mbele ya Yehova?​—1Yo 3:19, 20

  • Namna gani kusoma na kufikiri sana juu ya habari ya Daudi na ya Yehoshafati kulimusaidia ule ndugu?