Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tarehe 20-26/5

ZABURI 40-41

Tarehe 20-26/5

Wimbo 102 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. Juu ya Nini Tunapaswa Kusaidia Wengine?

(Dak. 10)

Kusaidia wengine kunatuleteaka furaha (Zb 41:1; w18.08 uku. 22 fu. 16-18)

Yehova anasaidiaka wale wenye kusaidia wengine (Zb 41:2-4; w15 15/12 uku. 24 fu. 7)

Wakati tunasaidia wengine, tunamuletea Yehova sifa (Zb 41:13; Mez 14:31; w17.09 uku. 12 fu. 17)

UJIULIZE, ‘Kuko mutu fulani mu kutaniko yangu mwenye naweza kusaidia ajue kutumikisha muzuri JW Library?’

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 40:5-10—Sala ya Daudi inatufundisha nini kuhusu kukubali kama Yehova ni Mwenye Mamlaka Makubwa zaidi? (it-1-F uku. 1260)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Anzisha mazungumuzo na mutu mwenye anaonekana kuwa na furaha. (lmd somo ya 2 nukta ya 3)

5. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Anzisha mazungumuzo na mutu mwenye anaonekana kuwa anajisikia mubaya. (lmd somo ya 3 nukta ya 5)

6. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) lff somo ya 14 nukta ya 6. Zungumuzia wazo fulani ya mu habari “Umusifu Yehova Katika Kutaniko” yenye kuwa mu sehemu “Habari Zingine” pamoya na mwanafunzi mwenye kusita kutoa maelezo ku mikutano. (th somo ya 19)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 138

7. Tutendee Wenye Kuzeeka Mambo ya Muzuri

(Dak. 15) Mazungumuzo.

Yehova anasamini kazi yenye ndugu na dada wenye kuzeeka wako nafanya mu kutaniko, na siye pia. (Ebr 6:10) Kwa miaka mingi, wamejitoa sana juu ya kufundisha, kuzoeza, na kutia moyo waamini wenzao. Inawezekana na weye unakumbuka namna walikusaidiaka. Namna gani unaweza kuonyesha kama unasamini yote yenye wamefanya na yenye wanaendelea kufanya mu kutaniko?

Muangalie VIDEO ‘Tutendee Ndugu Zetu Mambo ya Muzuri.’ Kisha uulize wasikilizaji:

  • Ndugu Ji-Hoon alijifunza nini kupitia Ndugu Ho-jin Kang?

  • Unafurahiaka mambo gani kuhusu ndugu na dada wenye kuzeeka wa mu kutaniko yako?

  • Mufano wa Musamaria mwema unatufundisha nini?

  • Ndugu Ji-Hoon aliita wengine juu waende kumusaidia Ndugu Ho-jin Kang pamoya. Juu ya nini ile ilikuwa jambo ya muzuri?

Kama tunafikiri sana kuhusu mahitaji yenye wenye kuzeeka wa mu kutaniko yetu wako nayo, tunaweza kupata nafasi mbalimbali za kuwasaidia. Kama unaona mwenye iko mu uhitaji, fikiria namna unaweza kumusaidia.—Yak 2:15, 16.

Soma Wagalatia 6:10. Kisha uliza wasikilizaji:

  • Ni mu njia gani unaweza “kutenda mambo ya muzuri kuhusu” wale wenye kuzeeka wa mu kutaniko yako?

8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 8 na Sala