Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tarehe 27/5–2/6

ZABURI 42-44

Tarehe 27/5–2/6

Wimbo 86 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. Utumikishe Muzuri Mafundisho Yenye Yehova Anakupatia

(Dak. 10)

Umuabudu Yehova pamoya na wengine, na ufanye vile zaidi sana kwa kukuwa pamoya nao fasi ya ibada, kama inawezekana (Zb 42:4, 5; w06-SW 1/6 uku. 9 fu. 4)

Usali mbele ya kujifunza Neno ya Mungu (Zb 42:8; w12 15/1 uku. 15 fu. 2)

Uache kweli ya Biblia ikuongoze mu maisha yako yote (Zb 43:3)

Mafundisho ya Mungu inatupatia nguvu ya kuvumilia magumu na kuendelea kutimiza ahadi yenye tulimutoleaka Yehova ya kumutumikia milele.—1Pe 5:10; w16.09 uku. 6 fu. 11-12.

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 44:19—Maneno “mahali mbweha wanakaa” inazungumuzia nini? (it-1-F uku. 417)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 4) NYUMBA KWA NYUMBA. Anzisha funzo ya Biblia. (lmd somo ya 5 nukta ya 5)

5. Kuendelesha Mazungumuzo

(Dak. 5) NYUMBA KWA NYUMBA. Alika musikilizaji ku hotuba ya watu wote. Tumia video Kwa Kawaida Tunafanya Nini Kwenye Jumba la Ufalme? (lmd somo ya 7 nukta ya 5)

6. Hotuba

(Dak. 3) lmd nyongeza ya A nukta ya 4—Kichwa: Kila Mutu Atakuwaka na Afya ya Muzuri. (th somo ya 2)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 21

7. Kamata Maamuzi ya Hekima Kuhusu Kazi na Masomo

(Dak. 15) Mazungumuzo.

Vijana, muko napanga mambo yenye mutafanya kisha tu kumaliza masomo ya segondere? Pengine uko nafikiria kufanya kazi yenye itakusaidia ukuwe painia. Ao pengine uko nafikiria kuendelea na masomo yenye itafanya upate ufundi fulani, brevet, ao diplome yenye itakusaidia upate ile kazi. Hii ni wakati ya maana sana mu maisha yako! Lakini, inaweza kuwa nguvu kuamua, juu uko nafikiria bya mingi byenye unaweza kufanya ao juu watu wako nakuchochea ukamate maamuzi yenye itawafurahisha. Sasa nini njo itakusaidia ukamate maamuzi ya hekima?

Soma Matayo 6:32, 33. Kisha uulize wasikilizaji:

  • Juu ya nini ni muzuri kujiwekea miradi ya kiroho yenye kuwa wazi mu akili mbele ya kukamata maamuzi ya maana kuhusu kazi na masomo?

  • Namna gani wazazi wanaweza kusaidia watoto wao watumikishe Matayo 6:32, 33?—Zb 78:4-7

Ukuwe muangalifu, usiache tamaa ya kukuwa tajiri na kukuwa na maisha ya raha ichochee maamuzi yako. (1Yo 2:15, 17) Ukumbuke kama kukuwa tu na vitu mingi vya kimwili inaweza kufanya ikuwe nguvu kwa mutu kukubali ujumbe wa Ufalme. (Lu 18:24-27) Kufuatilia utajiri na kufanya maendeleo ya kiroho habiendake pamoya.—Mt 6:24; Mk 8:36.

Muangalie VIDEO Epuka Kutumainia Mambo Yenye Itaisha!—Mali. Kisha uliza wasikilizaji:

  •   Namna gani Mezali 23:4, 5 inaweza kukusaidia ukamate maamuzi ya hekima?

8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 47 na Sala