Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tarehe 6-12/5

ZABURI 36-37

Tarehe 6-12/5

Wimbo 87 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. “Usikasirike kwa Sababu ya Waovu”

(Dak. 10)

Waovu wanatutafutiaka magumu na kututesa (Zb 36:1-4; w17.04 uku. 10 fu. 4)

Kukuwa na kasirani kali juu ya “waovu” kunaweza pia kutuletea magumu (Zb 37:1, 7, 8; w22.06 uku. 10 fu. 10)

Kutumainia ahadi za Yehova kutatupatia amani (Zb 37: 10, 11; w03-SW 1/12 uku. 13 fu. 20)

UJIULIZE, ‘Nakaziaka uangalifu habari zenye zinazungumuzia matendo ya jeuri?’

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 36:6—Mwandikaji wa zaburi alimaanisha nini wakati alisema kama haki ya Yehova iko sawa vile “milima mikubwa [ao, “kama milima ya Mungu,” maelezo ya chini.]”? (it-2-F uku. 340)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. (lmd somo ya 1 nukta ya 5)

5. Kuendelesha Mazungumuzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Anzisha funzo ya Biblia na mutu mwenye alikatalaka kujifunza zamani. (lmd somo ya 9 nukta ya 4)

6. Hotuba

(Dak. 5) ijwbv-SW habari ya 45—Kichwa: Zaburi 37:4 inamaanisha nini? (th somo ya 13)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 33

7. Uko Tayari kwa Ajili ya “Nyakati za Taabu”?

(Dak. 15) Mazungumuzo.

Juu ya misiba mingi ya asili na yenye kutokezwa na wanadamu, ndugu na dada zetu mu dunia yote wamepoteza vitu vya kimwili na wapendwa wao. (Zb 9:9, 10) Jambo ya kuhuzunisha ni kama “nyakati za taabu” zinaweza kutokea wakati wowote. Njo maana tunapaswa kujitayarisha juu ya kupambana na ile magumu.

Zaidi ya kutayarisha vitu vyenye vinaweza kutusaidia kama musiba unatokea, a ni mambo gani ingine yenye tunaweza kufanya ili kupambana na musiba?

  • Kujitayarisha kiakili: Ujue kama magumu inatokeaka, na ufikirie mambo yenye unaweza kufanya kama musiba unatokea. Uepuke kupenda sana vitu vya kimwili. Ile itakusaidia kutenda kwa hekima na kukamata maamuzi bila kusita. Kama unafanya vile utaonyesha kama usalama na uzima wako njo mambo ya maana kuliko vitu vyenye uko navyo. (Mwa 19:16; Zb 36:9) Itakusaidia pia ukuwe na mutazamo wenye kufaa kisha musiba, na inaweza kukusaidia usihuzunike sana kama unapoteza vitu vya kimwili.—Zb 37:19

  • Kujitayarisha kiroho: Ujikaze kukuwa hakika zaidi kama Yehova iko na uwezo wa kukutegemeza na anapenda kukuhangaikia. (Zb 37:18) Mbele musiba utokee, kila mara ukumbuke kama Yehova ataongoza na kutegemeza watumishi wake hata kama tutaokoa tu ‘uzima wetu kama kitu chenye kilichukuliwa katika vita.’—Yer 45:5; Zb 37:23, 24

Kama tunachunga mu akili ahadi za Yehova, tutamufanya kuwa ‘ngome yetu wakati wa taabu.’—Zb 37:39.

Muangalie VIDEO Uko Tayari kwa Ajili ya Musiba? Kisha uulize wasikilizaji:

  • Namna gani Yehova anaweza kutusaidia wakati wa taabu?

  • Tunaweza kufanya mambo gani ili kujitayarisha?

  • Namna gani tunaweza kusaidia wale wenye walipatwa na misiba?

8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 57 na Sala