MAISHA YA MUKRISTO
Yehova Atawaza Nini?
Mbele ya kukamata maamuzi fulani, ikuwe ya mukubwa ao ya kidogo, je, tunajiulizaka: ‘Yehova atawaza nini?’ Kusema kweli, hakuna siku tutajuaka mawazo yote ya Yehova. Lakini, anatuonyesha mu Biblia mambo yenye tuko nayo lazima juu tuweze kufanya “kila kazi njema.” (2Ti 3:16, 17; Ro 11:33, 34) Yesu alijua muzuri mapenzi ya Yehova ni nini na aliitia pa nafasi ya kwanza mu maisha yake. (Yoh 4:34) Juu tumuige Yesu, tunapaswa kufanya yetu yote ili kukamata maamuzi yenye itamufurahisha Yehova.—Yoh 8:28, 29; Efe 5:15-17.
MUANGALIE VIDEO MUENDELEE KUJUA MAPENZI YA YEHOVA (LAW 19:18), NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
-
Juu ya nini tunapaswa kutumikisha kanuni za Biblia mu maisha yetu?
-
Ni kanuni gani za Biblia zinapaswa kutusaidia kuchagua muziki?
-
Ni kanuni gani za Biblia zinapaswa kutusaidia kuchagua nguo zenye tutavaa na namna tutajipamba?
-
Tunapaswa kutumikisha kanuni za Biblia mu mambo gani ingine?
-
Tunaweza kufanya nini juu tukuwe tunatambua haraka mapenzi ya Yehova ni nini?