Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAGALATIA 4-6

Maana ya “Tukio la Mufano”

Maana ya “Tukio la Mufano”

4:24-31

Mutume Paulo alitumia “tukio la mufano” juu ya kuonyesha kama agano jipya lilikuwa muzuri zaidi kuliko agano la Sheria. Wakati Kristo na wariti wenzake watatawala wanadamu kwa upendo, watu wote watakuwa na tumaini la kukombolewa katika zambi, kutokamilika, mateso, na kifo.​—Isa 25:8, 9.

 

HAGARI​—MUTUMWA MWANAMUKE

Waisraeli wa kimwili wenye walikuwa chini ya agano la Sheria. Yerusalemu njo ilikuwa muji wao mukubwa

SARA​—MWANAMUKE MWENYE ALIKUWA HURU

Yerusalemu la juu, ni kusema sehemu ya mbinguni ya tengenezo la Mungu

“WATOTO” WA HAGARI

Wayahudi (wenye walifanya agano la Sheria na Yehova) walitesa Yesu na kumukataa

“WATOTO” WA SARA

Kristo na Wakristo watiwa-mafuta 144 000

UTUMWA WA AGANO LA SHERIA

Sheria ilikumbusha Waisraeli wa kimwili kama walikuwa watumwa wa zambi

AGANO JIPYA LINAKOMBOA

Kuonyesha imani mu bei ya ukombozi ya Yesu kunakomboa mutu mu laana ya Sheria