Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Unaweza Kuchangia Furaha ya Familia Yenu

Unaweza Kuchangia Furaha ya Familia Yenu

Yehova anapenda familia zikuwe na furaha. (Zb 127:3-5; Muh 9:9; 11:9) Lakini tunaweza kupoteza furaha kwa sababu ya mahangaiko ya hii dunia na makosa ya watu wa familia yetu. Kila mutu mu familia anaweza kufanya nini juu ya kuchangia furaha ya familia?

Bwana apatie bibi yake heshima. (1Pe 3:7) Apitishe wakati pamoya naye. Hatamuomba kufanya mambo yenye kupita uwezo wake na atamuonyesha shukrani juu ya mambo yenye iko nafanya kwa ajili ya yake na kwa ajili ya familia. (Kol 3:15) Amuonyeshe upendo na kumusifu.​—Mez 31:28, 31.

Bibi atafute njia za kumutegemeza bwana yake. (Mez 31:12) Ajitiishe kwake na amuunge mukono. (Kol 3:18) Azungumuze naye kwa upendo na aseme mambo ya muzuri juu yake.​—Mez 31:26.

Wazazi wapitishe wakati pamoya na watoto wao. (Kut 6:6, 7) Waambie watoto wao kama wanawapenda. (Mt 3:17) Wanapaswa kuonyesha upendo na utambuzi wakati wanawapatia nizamu.​—Efe 6:4.

Watoto waheshimu na watii wazazi wao. (Mez 23:22) Waelezee wazazi wao mawazo yao na namna wanajisikia. Wakubali nizamu kutoka kwa wazazi wao.​—Mez 19:20.

MUANGALIE VIDEO FANYA FAMILIA YAKO IKUWE NA FURAHA, KISHA MUJIBIE HII ULIZO:

• Kila mumoja alifanya nini ili kuchangia furaha ya familia?