Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Kampanye ya Pekee ya Kutangazia Watu Ufalme mu Mwezi wa 9!

Kampanye ya Pekee ya Kutangazia Watu Ufalme mu Mwezi wa 9!

Mu Mwezi wa 9 tutajikaza kutangazia watu kama Ufalme wa Mungu njo tu utamaliza magumu ya wanadamu. (Mt 24:14) Unaweza kushiriki namna gani mu ile kampanye? Mu Mwezi wa 9 somea watu wengi kadiri inawezekana andiko fulani kuhusu Ufalme wa Mungu. Kama mutu anapendezwa umupatie Munara wa Mulinzi Na. 2 2020. Kisha umurudilie bila kukawia na ujikaze kuanzisha funzo ya Biblia mu broshua Furahia Maisha Milele! Wote wenye watakuwa mapainia wasaidizi mu Mwezi wa 9 wanaweza kutumikia saa 15- ao 30.

Hivi karibuni Ufalme wa Mungu utaharibu serikali zote zenye kuipinga. (Da 2:44; 1Ko 15:24, 25) Tutumie kabisa hii nafasi ya pekee yenye tuko nayo ili kuonyesha kabisa kama tunaunga mukono Yehova na Ufalme wake!