Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kwenye picha zilitoka: Ukurasa wa 3: Kokkinakis na Ugiriki: Haki zimehifaziwa

Kwa kufuata mukuki wa saa kutoka juu kushoto: Kesi kati ya Baraza ya Elimu ya Virginia na Barnette; Kokkinakis na Ugiriki; Taganrog LRO Pamoya na Wengine na Urusi; Cha Pamoya na Wengine na Korea ya Kusini

MAISHA YA MUKRISTO

“Kutetea Habari Njema na Kuifanya Ikubaliwe Kisheria”

“Kutetea Habari Njema na Kuifanya Ikubaliwe Kisheria”

Wakati wapinzani walijaribu kuzuia Waisraeli kujenga tena hekalu, wajenzi walifanya yao yote ili kutetea kisheria haki yao ya kujenga. (Ezr 5:11-16) Vilevile, Wakristo leo wamefanya yao yote ili kutetea habari njema kisheria. (Flp 1:7) Njo maana Idara ya Mambo ya Kisheria ilianzishwa ku makao makubwa mu mwaka wa 1936. Leo Idara ya Mambo ya Kisheria inasimamia kazi ya kutetea faida za Ufalme mu dunia yote. Namna gani ile idara imesaidia kuendeleza kazi ya Ufalme na namna gani imesaidia watu wa Mungu?

MUANGALIE VIDEO KUTEMBELEA IDARA YA MAMBO YA KISHERIA KU MAKAO MAKUBWA, KISHA MUJIBIE MAULIZO YENYE KUFUATA:

  • Mashahidi wa Yehova wamepambana na matatizo gani ya Kisheria?

  • Tumepata ushindi gani mbalimbali? Toa mufano

  • Kila mumoja wetu anaweza kufanya nini ili kusaidia “kutetea habari njema na kuifanya ikubaliwe kisheria?”

  • Ku site yetu ni wapi tunaweza kupata habari za kisheria kuhusu watu wa Mungu na liste ya Mashahidi wenye wamefungwa mu gereza kwa sababu ya imani yao?