Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tarehe 15-21/7

ZABURI 63-65

Tarehe 15-21/7

Wimbo 108 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. “Upendo Wako Mushikamanifu Ni Muzuri Kuliko Uzima”

(Dak. 10)

Kuwa rafiki ya Mungu njo jambo ya maana zaidi kuliko uzima (Zb 63:3; w01-SW 15/10 uku. 15-16 fu. 17-18)

Kutafakari juu ya namna Yehova iko natuonyesha upendo wake mushikamanifu kunafanya tumupende tena zaidi (Zb 63:6; w19.12 uku. 28 fu. 4; w15 15/10 uku. 22 fu. 7)

Kufurahia upendo mushikamanifu wa Mungu kutatuchochea kumusifu kwa furaha (Zb 63:4, 5; w09-SW 15/7 uku. 16 fu. 6)

KU IBADA YA FAMILIA: Muzungumuzie njia mbalimbali zenye Yehova amewaonyesha upendo mushikamanifu.

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 64:3—Namna gani hii andiko inatuchochea kuwa na maneno ya muzuri? (w07-SW 15/11 uku. 15 fu. 6)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 2) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye-nyumba hajue luga yako. (lmd somo ya 3 nukta ya 4)

5. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 2) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Mazungumuzo inaisha mbele utoe ushahidi. (lmd somo ya 2 nukta ya 4)

6. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YA MAHALI PA WATU WENGI. Tafuta habari yenye itafurahisha mutu mwenye uko naongea naye, na upange kuzungumuza naye siku ingine. (lmd somo ya 1 nukta ya 5)

7. Kufasiria Mambo Yenye Unaamini

(Dak. 4) Onyesho. ijwfq 51—Kichwa: Juu ya nini Mashahidi wa Yehova wanatembeleaka tena mutu mwenye alishakasema kama hapendake kuzungumuza nao? (lmd somo ya 4 nukta ya 3)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 154

8. Namna ya Kuonyesha Mungu Kama Tunamupenda

(Dak. 15) Mazungumuzo.

Yehova ni “mwenye upendo mwingi mushikamanifu.” (Zb 86:15) Maneno “upendo mushikamanifu” inamaanisha upendo wenye unachochewa na uaminifu-mushikamanifu, ushikamanifu, na kuambatana kabisa. Kwa ujumla Yehova anaonyeshaka wanadamu wote upendo. Lakini, “upendo mushikamanifu” ni upendo wenye Yehova anaonyeshaka watumishi wake, ni kusema wale wenye wako na urafiki wa nguvu sana pamoya naye. (Zb 33:18; 63:3; Yoh 3:16; Mdo 14:17) Tutaonyesha kama tunafurahia upendo mushikamanifu wa Yehova kwa kumupenda pia. Namna gani? Kwa kutii amri zake, kutia ndani amri ya ‘kufanya wanafunzi.’—Mt 28:19; 1Yo 5:3.

Muangalie VIDEO Onyesha Upendo wa Kweli Katika Mahubiri. Kisha uliza wasikilizaji:

Namna gani upendo utatuchochea kuhubiri wakati

  • tunachoka?

  • tunapata upinzani?

  • tuko mu kazi?

9. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 79 na Sala