Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tarehe 26/8–1/9

ZABURI 78

Tarehe 26/8–1/9

Wimbo 97 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. Ukosefu wa Uaminifu wa Waisraeli—Mufano Wenye Unatupatia Onyo

(Dak. 10)

Waisraeli walisahau mambo ya muzuri yenye Yehova aliwafanyia (Zb 78:11, 42; w96-SW 1/12 uku. 29-30)

Waisraeli hawakuonyesha shukrani juu ya mambo yote ya muzuri yenye Yehova aliwafanyia (Zb 78:19; w06-SW 15/7 uku. 17 fu. 16)

Kuliko kujifunza kupitia makosa yao, Waisraeli waliendelea kukosa uaminifu (Zb 78:40, 41, 56, 57; w11 1/7 uku. 10 fu. 3-4)


ULIZO YA KUTAFAKARI: Nini njo itatusaidia tuendelee kuwa waaminifu kwa Yehova?

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 78:24, 25—Juu ya nini mana inaitwa “nafaka ya mbinguni” na “mukate wa wenye nguvu”? (w06-SW 15/7 uku. 11 fu. 4)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Ambia mwenye-nyumba kuhusu mupango wetu wa kujifunza Biblia na watu. (lmd somo ya 5 nukta ya 5)

5. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 3) NYUMBA KWA NYUMBA. Tumia trakte juu ya kuanzisha mazungumuzo; na ambia mwenye-nyumba kuhusu mupango wetu wa kujifunza Biblia na watu. (lmd somo ya 5 nukta ya 4)

6. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 1) NYUMBA KWA NYUMBA. Mwenye-nyumba anakuambia usikawie. Umuambie kuhusu mupango wetu wa kujifunza Biblia na watu. (lmd somo ya 2 nukta ya 5)

7. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Bila kuzungumuzia kweli fulani ya Biblia, ongea mu njia yenye itasaidia musikilizaji aelewe kama uko Shahidi wa Yehova, na umuambie kuhusu mupango wetu wa kujifunza Biblia na watu. (lmd somo ya 2 nukta ya 4)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 96

8. Mujifunze Kupitia Mufano wa Filipo Mweneza-Injili

(Dak. 15) Mazungumuzo.

Mu Biblia muko mifano ya watu wengi, ya muzuri na ya mubaya. Tunapaswa kupanga wakati na kujikaza kujifunza mambo fulani kutokana na ile mifano. Zaidi ya kusoma habari za Biblia, tunapaswa kutafakari juu ya mambo yenye zile habari zinatufundisha, na kupatanisha mwenendo wetu na ile mambo yenye tumejifunza.

Filipo mweneza-injili alikuwa Mukristo mwenye alijulikana kuwa ‘mwenye kujaa roho na hekima.’ (Mdo 6:3, 5) Mufano wake unatufundisha nini?

Muangalie VIDEO Mambo Yenye Mufano Wao Unatufundisha— Filipo Mweneza-Injili. Kisha uliza wasikilizaji waeleze mambo yenye wamejifunza kuhusu:

  • Namna Filipo alitenda wakati hali ilibadilika haraka.—Mdo 8:1, 4, 5

  • Baraka zenye Filipo alipata kwa kuwa tayari kuenda fasi kwenye kulikuwa uhitaji kubwa.—Mdo 8:6-8, 26-31, 34-40

  • Faida zenye Filipo na familia yake walipata juu walionyesha ukarimu.—Mdo 21:8-10

  • Furaha yenye ile familia ya mu video ilipata juu walifuata mufano wa Filipo

9. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 101 na Sala