Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Epuka Mitego Hii Wakati Unaongoza Funzo la Biblia

Epuka Mitego Hii Wakati Unaongoza Funzo la Biblia

Kusema Mingi: Haiko lazima ufasirie kila jambo. Yesu alitumia maulizo ili kusaidia watu wafikiri na wafikie kupata jibu. (Mt 17:24-27) Maulizo yanafanya funzo lichangamuke na yanakusaidia kujua mambo yenye mwanafunzi anaelewa na kuamini. (be uku. 253 fu. 3-4) Wakati unauliza ulizo, ngojea jibu. Kama mwanafunzi hajibie muzuri, kuliko kumuambia jibu, tumia maulizo yenye yatamusaidia afikie kupata jibu. (be uku. 238 fu. 1-2) Zungumuza kwa mwendo wenye utasaidia mwanafunzi aelewe mambo mapya.—be uku. 230 fu. 4.

Kuchanga-changa mambo: Epuka kueleza mambo yote yenye unajua juu ya habari yenye munajifunza. (Yoh 16:12) Kazia wazo kubwa lenye kuwa katika fungo. (be uku. 226 fu. 4-5) Maelezo mengi, hata kama ni yenye kufurahisha, yanaweza kufanya wazo kubwa lisionekane wazi. (be uku. 235 fu. 3) Kama mwanafunzi anaelewa wazo kubwa, muende kwenye fungo lenye kufuata.

Kujifunza Mambo Mengi: Kusudi letu ni kugusa moyo wa mwanafunzi, haiko kutafuta kumaliza kitabu. (Lu 24:32) Tumia nguvu ya Neno la Mungu kwa kukazia maandiko ya maana ya habari yenye munajifunza. (2Kor 10:4; Ebr 4:12; be uku. 144 fu. 1-3) Tumia mifano yenye kueleweka. (be uku. 245 fu. 2-4) Tambua magumu ya mwanafunzi wako na mambo yenye anaamini, na upatanishe funzo kulingana na hali yake. Umuulize maulizo kama haya: “Unawaza nini juu ya mambo yenye unajifunza hapa?” “Mambo haya yanatufundisha nini juu ya Yehova?” “Unawaza utapata faida gani kama unatumikisha mashauri haya?”—be uku. 238 fu. 3-5; uku. 259 fu. 1.