Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kualika Watu Wenye Kupendezwa Kwenye Mikutano

Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kualika Watu Wenye Kupendezwa Kwenye Mikutano

SABABU GANI NI LAZIMA KUFANYA HIVYO: Kwenye mikutano yetu tunapata nafasi ya ‘kumuimbia Yehova’ na kumusifu mara kwa mara. (Zab 149:1) Kwenye mikutano tunafundishwa kufanya mapenzi ya Mungu. (Zab 143:10) Mara nyingi watu wenye kupendezwa na wenye kujifunza Biblia wanafanya maendeleo wakati wanaanza kufika kwenye mikutano.

NAMNA YA KUFANYA:

  • Ualike watu bila kukawia. Haiko lazima ungojee mupaka wakati mutaanza funzo la Biblia.—Ufu 22:17

  • Elezea mutu mwenye kupendezwa namna mikutano inapitika na habari yenye itazungumuziwa kwenye mikutano yenye kufuata. Mambo haya yanaweza kukusaidia kufanya hivyo: mualiko kwa ajili ya mikutano, video Kwa Kawaida, Ni Mambo Gani Inafanyika Kwenye Jumba la Ufalme?, na sura ya 5 na ya 7 ya broshua Mapenzi ya Yehova

  • Unaweza kusaidia mutu mwenye kupendezwa kufika kwenye mikutano ao kuchagua nguo yenye kufaa. Ukae pembeni yake kwenye mikutano, na mutumie pamoja vichapo vyako. Umutambulishe kwa wengine