Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAISHA YA MUKRISTO

Tutafanya Nini Kama Mutoto Ndiye Anatukaribisha?

Tutafanya Nini Kama Mutoto Ndiye Anatukaribisha?

Kama mutoto ndiye anatukaribisha, tunapaswa kuomba kuzungumuza na wazazi wake. Hilo linaonyesha kama tunaheshimia mamlaka yao. (Met 6:20) Kama mutoto anatukaribisha ndani ya nyumba, tunapaswa kukataa. Kama wazazi wake hawako, tunapaswa kurudia wakati mwingine.

Hata kama ni kijana, pengine mwenye miaka kati ya 15 na 19, ni lazima pia kuomba kuzungumuza na wazazi wake. Ikiwa hawako, tunaweza kumuuliza kama wanamuruhusu ajichagulie mambo ya kusoma. Kama wanafanya hivyo, tunaweza kumutolea kichapo fulani na kumuomba afungue jw.org.

Wakati tunarudilia kijana mwenye kupendezwa tunapaswa kuomba kuzungumuza na wazazi wake. Hilo litatupatia nafasi ya kuwaelezea sababu gani tunawatembelea na kuwaonyesha mashauri mazuri na yenye kutegemeka yenye Biblia inatoa juu ya familia. (Zab 119:86, 138) Kuonyesha kama tunahangaikia na kuheshimia wazazi kutatoa ushahidi muzuri na kunaweza kutupatia nafasi ya kutangazia familia yote habari njema.—1Pet 2:12.