Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tarehe 7-13/10

ZABURI 92-95

Tarehe 7-13/10

Wimbo 84 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU

1. Kumutumikia Yehova Njo Namna ya Muzuri Zaidi ya Kuishi!

(Dak. 10)

Yehova anastahili kupokea ibada yetu (Zb 92:1, 4; w18.04 uku. 26 fu. 5)

Anasaidiaka watu wake kukamata maamuzi yenye inawaleteaka furaha (Zb 92:5; w18.11 uku. 20 fu. 8)

Anaonaka wale wenye kumutumikia kuwa wa maana hata kama walishazeeka (Zb 92:12-15; w20.01 uku. 19 fu. 18)

UJIULIZE, ‘Nini njo iko nanizuia kujitoa kwa Yehova na kubatizwa?’

2. Mali ya Kiroho

(Dak. 10)

  • Zb 92:5—Namna gani hii maneno inaonyesha wazi hekima ya Yehova? (cl-SW uku. 176 fu. 18)

  • Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?

3. Usomaji wa Biblia

TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI

4. Kuanzisha Mazungumuzo

(Dak. 4) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Tafuta nafasi ya kumuambia mutu mwenye uko naongea naye kuhusu kazi yenye uko nafanya ya kufundisha Biblia. (lmd somo ya 5 nukta ya 3)

5. Kuendelesha Mazungumuzo

(Dak. 3) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Anzisha funzo ya Biblia na mutu mwenye kupendezwa mwenye alikatalaka kujifunza zamani. (lmd somo ya 8 nukta ya 4)

6. Kufanya Wanafunzi

(Dak. 5) Uzungumuze na mwanafunzi mwenye hafanye maendeleo. (lmd somo ya 12 nukta ya 5)

MAISHA YA MUKRISTO

Wimbo 5

7. Wakati Vijana Wako na Mahangaiko

(Dak. 15) Mazungumuzo.

Hata watumishi wa Yehova wanakuwaka pia na mahangaiko. Kwa mufano, Daudi alikuwaka na mahangaiko wakati fulani mu maisha yake, sawa vile tu ndugu zetu wengi leo. (Zb 13:2; 139:23) Jambo ya kuhuzunisha ni kama, hata vijana wanakuwaka na mahangaiko. Wakati fulani, mahangaiko inaweza kufanya mambo ya kawaida itulemee; mambo sawa vile kuenda ku masomo ao kuhuzuria mikutano. Ile inaweza kufanya tuogope na tukuwe hata na mawazo ya kujiua.

Vijana, kama munalemewa na mahangaiko, muambie wazazi wenu ao mutu mwenye kukomala kiroho. Na musisahau pia kumuomba Yehova musaada katika sala. (Flp 4:6) Atawasaidia. (Zb 94:17-19; Isa 41:10) Tuone mufano wa Steing.

Muangalie VIDEO Yehova Alinihangaikia. Kisha uliza wasikilizaji:

• Ni andiko gani ya Biblia ilimusaidia Steing, na juu ya nini?

• Namna gani Yehova alimuhangaikia?

Wazazi, munaweza kusaidia watoto wenu wapambane na mahangaiko kwa kuwasikiliza kwa uvumilivu, kwa kuwaonyesha kama munawapenda, na kwa kuwasaidia wakuwe hakika kama Yehova pia anawapenda. (Tit 2:4; Yak 1:19) Mumutegemee Yehova juu ya kupata vitia moyo na nguvu yenye muko nayo lazima ili kusaidia watoto wenu.

Pengine hatujue kama mutu fulani iko napambana na mahangaiko mu kutaniko ao hatuelewe namna iko najisikia kabisa. Lakini, tunaweza kusaidia kila mutu mu kutaniko ajisikie kuwa anapendwa na kama iko wa maana.—Mez 12:25; Ebr 10:24.

8. Funzo ya Biblia ya Kutaniko

Maneno ya Kumalizia (Dak. 3) | Wimbo 81 na Sala