Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

NAMNA MAGUMU ITAMALIZWA KABISA

Chini ya Ufalme wa Mungu “Amani Itakuwa Nyingi”

Chini ya Ufalme wa Mungu “Amani Itakuwa Nyingi”

Hivi karibuni, Ufalme wa Mungu wenye tumengojea kwa muda murefu​—serikali ya ulimwengu wote yenye Mungu ameanzisha​—itafanya wanadamu wote ku dunia waishi kwa umoja na amani. Kama vile andiko la Zaburi 72:7 limeahidi, “amani itakuwa nyingi.” Lakini ni wakati gani Ufalme huo utaanza kutawala dunia yote? Utafanya vile namna gani? Na unaweza kufanya nini ili kufaidika na utawala wa Ufalme huo?

UFALME WA MUNGU UTAKUJA WAKATI GANI?

Biblia ilitabiri matukio fulani makubwa yenye ingeonyesha kama Ufalme wa Mungu uko unakuja hivi karibuni. Ile matukio yote inafanyiza “alama” zenye kutia ndani vita kati ya mataifa, njaa, magonjwa, matetemeko mingi ya dunia, na kuongezeka kwa uvunjaji wa sheria.​—Matayo 24:3, 7, 12; Luka 21:11; Ufunuo 6:2-8.

Unabii mwingine unasema hivi: “Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari zenye kuwa ngumu kuvumilia. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda feza, . . . wenye hawatii wazazi, wenye hawana shukrani, wenye hawana ushikamanifu, wenye hawana upendo wa asili, wenye hawataki makubaliano yoyote, wachongezi, wenye hawajizuie, wakali, wenye hawapendi wema, . . . wenye kujivuna kwa kiburi, wenye kupenda raha kuliko kumupenda Mungu.” (2 Timoteo 3:1-4) Tangu zamani, watu fulani wamekuwa wakionyesha zile tabia. Lakini leo, watu wengi sana wanaonyesha zile tabia.

Unabii mbalimbali wenye tumezungumuzia ulianza kutimia mwaka wa 1914. Kwa kweli, wanahistoria, wakubwa wenye kuheshimiwa katika mambo ya politike, na waandikaji walizungumuzia namna ulimwengu ulibadilika kisha ule mwaka. Kwa mufano, mwanahistoria wa Danemark Peter Munch aliandika hivi: “Vita yenye ilitokea mwaka wa 1914 ilileta mabadiliko makubwa katika historia ya wanadamu. Mbele ya ule mwaka, watu waliwaza kama hali ya ulimwengu itakuwa muzuri zaidi, . . . lakini ule mwaka ulituingiza mu kipindi cha misiba, woga, chuki na cha kukosa amani kila fasi.”

Lakini jambo la kufurahisha ni kwamba, kisha ile mambo yote, kutakuwa hali za amani. Ile inaonyesha kama hivi karibuni Ufalme utaanza kutawala dunia. Yesu alizungumuzia jambo hili la muzuri wakati alitaja alama za siku za mwisho: “Hii habari njema ya Ufalme itahubiriwa katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote, na kisha ule mwisho utakuja.”​—Matayo 24:14.

Ile habari njema njo kichwa cha musingi cha ujumbe wenye Mashahidi wa Yehova wanatangaza. Kwa kweli, kichapo chenye wanachapisha sana kinaitwa Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova. Unazungumuzia kwa ukawaida mambo ya muzuri yenye Ufalme wa Mungu utafanyia wanadamu ku dunia.

NAMNA GANI UFALME WA MUNGU UTAANZA KUTAWALA?

Jibu linatia ndani mambo ine ya maana yenye kufuata:

  1. Ufalme hautatumia kiongozi yeyote wa politike wa hii dunia.

  2. Viongozi wa politike wa hii dunia hawatapenda kuacha mamlaka yao na kwa upumbavu watapigana na Ufalme wa Mungu.​—Zaburi 2:2-9.

  3. Ufalme wa Mungu utaharibu serikali za kipolitike zenye zinapenda kuendelea kutawala wanadamu. (Danieli 2:44; Ufunuo 19:17-21) Ile vita ya mwisho yenye itapiganwa mu dunia yote inaitwa Armagedoni.​—Ufunuo 16:14, 16.

  4. Wale wenye wanapenda kujitiisha ku Ufalme wa Mungu wataokoka vita ya Armagedoni na kuingia mu dunia mupya yenye amani. Watafanyiza ile yenye Biblia inaita “kundi kubwa la watu,” wenye pengine hesabu yao itakuwa mamilioni.​—Ufunuo 7:9, 10, 13, 14.

UNAWEZA KUFANYA NINI ILI KUFAIDIKA NA UTAWALA WA UFALME?

Hatua ya kwanza yenye unaweza kukamata ili kuwa raia wa Ufalme wa Mungu ni kupata elimu. Kwa kweli, wakati alisali kwa Mungu, Yesu alisema hivi: “Uzima wa milele ndio huu, wafikie kukujua wewe Mungu wa pekee wa kweli, na ule mwenye ulituma, Yesu Kristo.”​—Yohana 17:3.

Wakati watu wanamujua Yehova Mungu kuwa Mutu wa kweli, wanapata faida mu njia mingi. Tufikirie faida mbili kati ya zile faida: Kwanza, wanakuwa na imani yenye nguvu katika Yehova. Ile imani yenye kutegemea mambo yenye kuwa hakika, inawafanya wakuwe hakika kama Ufalme wa Mungu ni kitu cha kweli kabisa na kuwa utawala wake uko karibu. (Waebrania 11:1) Pili, upendo wao kwa Mungu na jirani unakuwa wenye nguvu zaidi. Upendo wao kwa Mungu unawachochea wamutii yeye kwa kupenda. Upendo wao kwa jirani unawachochea kutumikisha maneno ya Yesu yenye kusema hivi: “Kama vile munataka watu wawatendee ninyi, muwatendee kwa njia ileile.”​—Luka 6:31.

Kama Baba mwenye upendo, Muumbaji wetu anatutakia mambo ya muzuri sana. Anapenda tukuwe na ile yenye Biblia inaita “uzima wa kwelikweli.” (1 Timoteo 6:19) Leo uzima hauko “wa kwelikweli.” Kwa mamilioni ya watu, maisha iko nguvu sana, na wanapaswa kujikaza sana ili waendelee kuishi. Ili ujue namna ule “uzima wa kwelikweli” utakuwa, fikiria mambo fulani ya muzuri yenye Ufalme wa Mungu utafanyia raia wake.

Wakati wa utawala wa Ufalme, watu wataishi kwa amani na usalama na watakuwa na chakula mingi