Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kupitia mufano wao, wazazi wanafundisha watoto wao namna ya kuonyesha upendo

HATUA YA KUFUATA ILI KUMALIZA MAGUMU

Watu Wanapaswa Kujua Tofauti Kati ya Tabia ya Muzuri na Tabia ya Mubaya

Watu Wanapaswa Kujua Tofauti Kati ya Tabia ya Muzuri na Tabia ya Mubaya

Wakati walikuwa mu matembezi yenye ilipangwa na masomo, vijana fulani wanaume walishitakiwa kuwa walimutendea mubaya kingono mwanafunzi mwingine mwanaume. Wote walisomea ku masomo fulani ya kipekee yenye kuheshimiwa mu inchi ya Kanada. Kisha tukio hilo la mubaya, Leonard Stern aliandika hivi mu gazeti la Ottawa Citizen: “Kuwa mwenye akili, kuwa na elimu ya muzuri, na kuwa tajiri hakuzuie vijana kufanya mambo ya mubaya.”

Stern alisema pia hivi: “Kwa kawaida, jambo la maana sana lenye wazazi wanaweza kufanya ni kufundisha watoto wao wajue tofauti kati ya tabia ya muzuri na tabia ya mubaya. Lakini tofauti na ile, inaonekana kama wazazi wengi wanawaza kuwa jambo la maana zaidi ni kusaidia watoto wao waweze masomo na wapate kazi za muzuri ili wafikie kupata feza mingi.”

Ni kweli kwamba, masomo ni ya lazima. Lakini, hata elimu ya ulimwengu ya muzuri zaidi haiwezi kusaidia mutu aachane na tamaa za mubaya ao mawazo ya mubaya. Sasa, ni wapi kwenye tunaweza kupata elimu yenye inaweza kutusaidia kupiganisha ile mambo​—elimu yenye inaweza kutoa muongozo kuhusu mwenendo?

ELIMU YA MUZURI ZAIDI KULIKO ELIMU YA ULIMWENGU

Biblia iko kama kioo. Wakati tunajiangalia ndani, tunaona waziwazi zaidi mipaka yetu na uzaifu wetu. (Yakobo 1:23-25) Lakini, Biblia inafanya zaidi ya ile. Inatusaidia kufanya mabadiliko yenye kuombwa, kukomalisha sifa zenye kuchochea amani ya kweli na umoja. Zile sifa zinatia ndani wema, fazili, uvumilivu, kujizuia, na upendo. Upendo unaitwa hata “kifungo kikamilifu cha umoja.” (Wakolosai 3:14) Juu ya nini upendo ni sifa ya pekee sana? Ona mambo yenye Biblia inasema juu ya ile sifa.

  • “Upendo ni wenye uvumilivu na wenye fazili. Upendo hauna wivu. Haujisifu, haujivune [kwa kiburi], haujiendeshe bila adabu, hautafute faida zake wenyewe, haukasirike haraka. Hauweke hesabu ya ubaya. Haufurahie ukosefu wa haki [mambo ya mubaya], lakini unafurahi pamoja na kweli. Unafunika mambo yote, . . . unavumilia mambo yote. Upendo haushindwe hata kidogo.”​—1 Wakorinto 13:4-8.

  • “Upendo haumufanyie jirani mambo ya mubaya.”​—Waroma 13:10.

  • “Zaidi ya mambo yote, mukuwe na upendo mwingi ninyi kwa ninyi, kwa sababu upendo unafunika zambi nyingi.”​—1 Petro 4:8.

Unajisikia namna gani wakati uko pamoja na watu wenye wanakupenda? Unajisikia salama? Mwenye amani? Mwenye kutulia? Ndiyo, unajua kama wanakutakia mambo ya muzuri, na kama hawawezi hata kidogo kukuumiza kimakusudi.

Upendo unaweza pia kuchochea watu waache mambo yenye wanapenda, hata kubadilisha namna yao ya kuishi, kwa faida ya watu wengine. Kwa mufano, wakati mwanaume fulani mwenye tutaita George alifikia kuwa tate (ao, nkambo), alipenda sana kupitisha wakati pamoja na mutoto wa mutoto wake mwanamuke. Lakini kulikuwa tatizo. George alikuwa anavuta sana tumbako, na mukwe wake hakupenda avutie pembeni ya mutoto wake. George alifanya nini? Hata kama alikuwa amevuta kwa miaka 50, aliachana na ile tabia kwa faida ya mujukuu wake. Ndiyo, upendo ni wenye nguvu sana!

Biblia inatusaidia kukomalisha sifa mingi za muzuri, kama vile wema, fazili, na zaidi sana upendo

Upendo ni sifa yenye tunajifunza kuonyesha. Wazazi wanatimiza daraka kubwa katika kufundisha watoto wao namna ya kuonyesha upendo. Wanawapatia watoto wao chakula na kuwalinda na wanawasaidia wakati wanaumia ao wanagonjwa. Wazazi wazuri wanazungumuza na watoto wao na kuwafundisha. Wanawatia pia nizamu, jambo lenye linatia ndani kuwafundisha kanuni za muzuri kuhusu mema na mabaya. Zaidi ya ile, wazazi wazuri wanajikaza kuwa mifano ya muzuri yenye watoto wao wanaweza kufuata.

Lakini, jambo la kuhuzunisha ni kwamba, wazazi fulani wanashindwa kutimiza madaraka yao. Je, ile inamaanisha kama watoto wao hawatakuwaka watu wazuri? Hapana kabisa! Hata watu wengi wakubwa, kutia ndani watu fulani wenye walikomalia mu familia zenye kuwa na matatizo, wamefanya mabadiliko yenye kushangaza mu maisha yao, na wamefikia kuwa watu wenye kuhangaikia wengine na wenye kutumainika. Kama vile tutaona mu habari yenye kufuata, ile inatia ndani watu fulani wenye walionwa kuwa hawawezi kubadilika hata kidogo!