Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

WALIPAMBANA NA MAGUMU

Ricardo na Andres Wanaeleza Maisha Yao

Ricardo na Andres Wanaeleza Maisha Yao

Elimu yenye kutegemea Biblia iko na nguvu ya ajabu ya kubadilisha maisha ya watu. Fikiria mifano mbili kuhusu jambo hilo: Mufano wa Ricardo na Andres.

RICARDO: Wakati nilikuwa na miaka 15, nilijiunga na kikundi cha vijana wenye kutendea wengine mubaya. Nilichochewa sana kufanya mambo yenye marafiki wangu wa mupya walikuwa wanafanya. Kwa kweli, tamaa yangu ilikuwa kufanya miaka 10 mu gereza! Ile inaweza kuonwa kuwa upumbavu. Lakini fasi kwenye niliishi, watu wenye walikuwa wamefanya siku mingi mu gereza walisifiwa na kuheshimiwa. Na nilipenda kuwa kama wao.

Nilifanya mambo yote yenye kufanywa na kikundi hicho, kutia ndani kutumia dawa za kulewesha, uasherati, na jeuri (ao, violence). Usiku moja nilikuwa mu ugomvi wa kupigana masasi. Niliwaza kama wataniua, lakini nilikimbia bila kuumizwa. Kisha ile tukio, nilianza kuwaza sana juu ya maisha yangu na mambo ya kufanya mu maisha, na niliamua kama nilipaswa kufanya mabadiliko. Lakini ningefanya vile namna gani? Ningepata wapi musaada?

Watu wengi wa jamaa yangu walikosa furaha. Maisha yao ilikuwa na matatizo mingi. Lakini familia ya mujomba wangu mumoja haikuwa mu ile hali. Nilijua kama walikuwa watu wazuri, na kama waliishi kulingana na mambo yenye kuwa mu Biblia. Kwa kweli, wakati moja walikuwa wamenifundisha kuwa jina la Mungu ni Yehova. Kwa hiyo, muda mufupi kisha ile tukio lenye nilitaja, nilisali kwa Yehova, kwa kutaja jina lake na kumuomba anisaidie. Kwa kushangaza, siku yenye ilifuata, Shahidi mumoja wa Yehova aligonga ku mulango wangu! Alifikia kuwa mwalimu wangu wa Biblia.

Bila kukawia nilipambana na tatizo kubwa. Marafiki wangu wa zamani waliniita mara mingi kupitia telefone, wakiniomba nipitishe wakati nao. Hata kama haikukuwa mwepesi, nilikataa. Niliazimia kuendelea kujifunza Biblia, na ninafurahi kuwa nilifanya vile! Maisha yangu ilibadilika kwa njia ya ajabu, na nilipata furaha ya kweli.

Nakumbuka siku nilimuambia Mungu katika sala kama, zamani nilitamani kupitisha miaka 10 mu gereza ili kupata heshima nikiwa mumoja wa vijana wa kikundi cha kutendea watu mubaya. Kwa hiyo, nilimuomba aniruhusu nimutumikie hata miaka 10 nikiwa muhubiri wa wakati wote ili nisaidie wengine kama tu vile nilisaidiwa. Mungu alijibia sala yangu, juu nimepitisha miaka 17 nikiwa muhubiri wa wakati wote! Na ninaweza pia kusema, sijafungwaka mu gereza.

Lakini, wengi kati ya marafiki wangu wa zamani wamefanya miaka mingi mu gereza. Wengine wamekwisha kufa. Wakati ninakumbuka maisha yangu ya zamani, ninashukuru sana watu wa jamaa yangu wenye kuwa Mashahidi. Walikuwa tayari kuwa tofauti kwa kuishi kulingana na kanuni za Biblia. Niliendelea kuwaheshimia zaidi kuliko vile niliheshimia mutu yeyote mu kikundi cha wale vijana. Zaidi ya yote, niko mwenye shukrani kwa Mungu kwa kunifundisha njia ya muzuri zaidi ya maisha.

ANDRES: Nilizaliwa na kukomalia mu eneo moja maskini mwenye dawa za kulewesha, unyanganyi, kuua, na kufanya uasherati vilikuwa mambo ya kawaida. Baba yangu alikuwa mutumwa wa pombe na kokeini. Yeye na mama yangu walikuwa wanagombana kila mara, kwa maneno na walipigana.

Nilianza kunywa pombe na kutumia dawa za kulewesha wakati nilikuwa ningali mudogo. Wakati wangu wa mingi zaidi niliupitisha mu barabara, nikiiba na kuuzisha vitu vyenye nilikuwa ninaiba. Kadiri niliendelea kukomaa, baba yangu, alijaribu kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na mimi, lakini alifanya vile mu njia yenye haifae. Alinifundisha namna ya kuingiza kwa siri katika inchi dawa za kulewesha na vitu vingine vyenye kukatazwa na serikali ili kuviuzisha. Nilipata feza mingi haraka. Kisha, siku moja polisi walikuja ku nyumba yangu. Walinikamata na nilihukumiwa kufungwa miaka 5 mu gereza.

Asubui moja, tangazo fulani kupitia chombo cha kuongeza sauti ilialika wafungwa wenzangu ku mazungumuzo ya Biblia yenye ilifanywa na Mashahidi wa Yehova. Mimi pia niliamua kuifuata. Mambo yenye nilisikia ilipatana na akili, kwa hiyo nilianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Hawakufundisha maandiko kijuujuu tu, lakini walinionyesha waziwazi kanuni za Mungu za juu kuhusu mwenendo.

Bila kukawia, nilitambua kama singeweza kufanya mabadiliko yenye kuombwa bila kusaidiwa, zaidi sana wakati niliogopeshwa na wafungwa wenzangu wenye hawakupenda mambo yenye nilikuwa ninafanya. Kwa hiyo, nilisali ili kupata nguvu na hekima, na Yehova alinisaidia. Kwa kweli, kuliko kuogopa, nilifikia hata kupata uhodari wa kuzungumuza na wafungwa wengine kuhusu Biblia.

Wakati muda wa kufunguliwa ulifika, nilikuwa na wasiwasi wa kutoka inje hivi kwamba nilipenda kubakia mu gereza wakati murefu zaidi! Wakati nilikuwa ninatoka, wafungwa fulani waliniaga. Wengine hata waliniambia hivi kwa furaha, “Uende muzuri ku nyumba, mutumishi.”

Ninaogopa wakati ninafikiria namna maisha yangu ingekuwa kama singemupatia Mungu nafasi ya kunifundisha. Niko mwenye shukrani sana, tena sana kuwa Mungu ananipenda na kuwa hakuniona kama mutu mwenye hawezi kubadilika. a

a Mifano mingi yenye kuonyesha uwezo wa Biblia wa kubadilisha maisha ya watu iko ku jw.org. Uende ku MAKTABA mu Habari Mbalimbali, kisha ufungule sehemu “Biblia Inabadilisha Maisha ya Watu.”.