Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Matunzo ya muzuri haimalize tu alama za ugonjwa; inapaswa kushambulia ugonjwa wenyewe

MAGUMU

Sababu Zenye Kufanya Kukuwe Matatizo

Sababu Zenye Kufanya Kukuwe Matatizo

Je, unaamini kama wanadamu wanaweza kumaliza matatizo mingi yenye kufanya tukose amani na usalama na yenye kufanya tukuwe na woga kuhusu wakati wetu wenye kuja? Ili munganga aweze kututunza muzuri, anapaswa kwanza kujua ugonjwa wenye kufanya tuteseke, hapana tu alama za inje.

Kwa mufano, mwanaume mumoja mwenye kuitwa Tom aligonjwa na kisha akakufa. Juu ya nini alikufa? Munganga mwenye alimupokea muda kidogo mbele akufe, aliandika hivi: “Wakati alama za kwanza za magonjwa yake zilionekana, hakuna mutu mwenye alifikiria kutafuta kujua zilitokana na nini.” Inaonekana kama wanganga wenye walimutunza ku mwanzo walimupatia tu dawa za kumufanya ajisikie muzuri.

Je, wanadamu pia wanajaribu kumaliza matatizo ya ulimwengu kwa kutumia njia ya namna hiyo? Kwa mufano, ili kupiganisha uvunjaji wa sheria, serikali zinaweka sheria, zinatia kamera za kuchunguza watu, na zinaongeza hesabu ya polisi. Lakini, hata kama kufanya vile kunasaidia kwa njia fulani, hakumalize sababu zenye kuchochea watu watende kwa njia fulani. Kwa kweli, mara mingi namna watu wanatenda inaonyesha ni mawazo gani yenye wako nayo, namna wanajisikia, na mambo yenye wanapenda kabisa.

Daniel mwenye kuishi mu inchi moja ya Amerika ya Kusini yenye inaendelea kuwa maskini, anasema hivi: “Zamani tulikuwa na maisha ya kawaida. Hakukuwa wezi wenye kutumia bunduki. Lakini leo, hakuna tena muji ao kijiji chenye kuwa na amani. Kwa sababu maisha inakuwa nguvu, tunaweza sasa kuona waziwazi kuwa watu wengi ni wenye pupa na hawaheshimie uzima wa watu ao mali yao.”

Mwanaume mumoja mwenye tutaita Elias alikimbia vita mu inchi moja ya Mashariki ya Kati, na kisha akajifunza Biblia. Anasema hivi: “Vijana wengi wanaume wa muji wangu, walitiwa moyo na familia zao na watu wa dini yao ya kipolitike kujiingiza mu vita ili wafikie kuonwa kuwa washujaa (ao, héros). Wale wenye walipaswa kupigana nao walitiwa moyo pia wafanye vile! Ile mambo yote ilinifanya nione kuwa ni mubaya sana kutumainia watawala wanadamu.”

Kitabu kimoja cha zamani chenye hekima kiko na haki kwa kusema hivi:

  • “Muelekeo wa moyo wa mwanadamu ni mubaya kuanzia ujana wake.”​—Mwanzo 8:21.

  • “Moyo ni mudanganyifu kuliko kitu kingine chochote na uko hatari. Ni nani anaweza kuujua?”​—Yeremia 17:9.

  • “Mawazo mabaya, mauaji, . . . uasherati, wizi, ushahidi wa uongo, . . . yanatoka katika moyo.”​—Matayo 15:19.

Wanadamu wameshindwa kumaliza tabia za mubaya zenye kuwa ndani yetu zenye kuumiza wengine. Kwa kweli, kama vile tumetoka kuona mu habari yenye ilizungumuzia matatizo, tabia hizo zinaendelea kuwa za mubaya zaidi. (2 Timoteo 3:1-5) Na hali hiyo inaendelea hata kama leo watu wanajua mambo mingi sana, na hata kama kuko njia mingi sana za kupashana habari kuliko zamani! Sasa, juu ya nini hatuwezi kufanya ulimwengu ukuwe wenye amani na usalama? Je, tunapenda tu kufanya mambo yenye hatuna uwezo wa kufanya? Tunajaribu kufanya jambo lenye haliwezekane?

TUNAJARIBU KUFANYA JAMBO LENYE HALIWEZEKANE?

Hata kama kunaweza kuwa njia fulani ili kumaliza tabia za wanadamu zenye kuumiza, hatuna uwezo wa kufanya ulimwengu ukuwe wenye amani na usalama kwa ajili ya watu wote. Juu ya nini? Ni juu sisi wanadamu tuko na mipaka.

Ukweli ni huu: “Mwanadamu . . . hana hata uwezo wa kuongoza hatua yake.” (Yeremia 10:23) Hatukuumbwa ili tujiongoze sisi wenyewe. Kwa kweli, hatukuumbwa ili tutawale wanadamu wenzetu kama vile tu hatukuumbwa ili tuishi ndani ya maji ao nafasi kwenye hakuna hewa!

Hatukuumbwa ili tutawale wanadamu wenzetu kama vile tu hatukuumbwa ili tuishi ndani ya maji

Waza juu ya jambo hili: Je, wanadamu wengi wanapendaka wenzao wawaambie namna ya kuishi ao wawaambie kanuni zenye wanapaswa kufuata kuhusu mwenendo? Je, watu wanapendaka kuambiwa namna wanapaswa kuona mambo kama vile kutosha mimba, hukumu ya kifo ao namna wanapaswa kutia nizamu watoto wao? Ile ni mambo kidogo tu kati ya mambo yenye kugawanya watu. Hata kama inaweza kuwa nguvu kukubali, mambo yenye Biblia inasema ni ya kweli. Hatuna tu uwezo ao haki ya kutawala wanadamu wenzetu. Tunaweza kupata wapi musaada?

Jambo lenye tunapaswa tu kufanya ni kutafuta musaada wa Muumbaji wetu. Kwa kweli, yeye njo alituumba! Watu fulani wanaweza kuwaza kama Mungu amekwisha kutusahau, lakini haiko vile. Kwa kweli, hekima yenye kuwa mu Biblia inaonyesha kuwa anatuhangaikia. Wakati tunaelewa kitabu hicho cha pekee, tunajielewa pia muzuri zaidi. Na tunaweza kuelewa sababu yenye inafanya historia ya wanadamu ikuwe yenye kuhuzunisha sana. Sababu ni kuwa, kama vile mwanafilozofia Mujerumani aliandika, “watu na serikali hawajajifunza jambo lolote kupitia historia, na ile imefanya washindwe kubadilisha tabia zao.”

HEKIMA YA BIBLIA INATULINDA!

Siku moja, mutu mumoja mwenye hekima alisema kama “hekima inaonekana kuwa yenye haki kupitia watoto wake wote,” ao matokeo. (Luka 7:35) Mufano mumoja kuhusu ile hekima unapatikana mu andiko la Isaya 2:22, lenye kusema: “Kwa ajili yenu wenyewe, muache kutumainia mwanadamu bure.” Shauri hilo lenye hekima linaweza kutulinda ili tusikuwe na matumaini ao matazamio ya uongo. Kenneth, mwenye kuishi katika muji mumoja wenye jeuri wa Amerika ya Kaskazini, anasema hivi: “Watu wote wenye kufanya politike wanaahidi kuwa watafanya mambo ikuwe muzuri zaidi, lakini hawawezi hata kidogo. Wanashindwa kila mara kutimiza ahadi zao, na ile inaonyesha kama mambo yenye Biblia inasema ni ya kweli na ni yenye hekima.”

Daniel, mwenye tulizungumuzia ku mwanzo wa habari hii, anasema hivi: “Kila siku yenye kupita inanisadikisha zaidi kama wanadamu hawawezi kutawala muzuri. . . . Kuwa tu na feza mu benki ao kuwa na njia fulani ya kupata feza hakumaanishe kila mara kama mutu atakuwa na wakati wenye kuja wa muzuri. Nimeona watu wanavunjika moyo sana juu ya ile mambo.”

Biblia haitulinde tu ili tusikuwe na matumaini ya uongo, lakini pia inafanya zaidi ya ile. Kama vile tutaona, inatupatia pia tumaini.