Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Namna ya Kuishi na Wengine kwa Amani

Namna ya Kuishi na Wengine kwa Amani

Muumbaji wetu anatuonyesha mambo yenye tunaweza kufanya juu tuishi na wengine kwa amani, ikuwe tuko ku nyumba, ku kazi, ao wakati tuko na marafiki. Kwa mufano, fikiria hii mashauri ya hekima yenye ilisaidia watu wengi wakati waliitumikisha.

Ukuwe Tayari Kusamehe

“Muendelee . . . kusameheana kwa kupenda hata kama mutu yeyote iko na sababu ya kulalamika juu ya mwingine.”​—WAKOLOSAI 3:13.

Siye wote tunafanyaka makosa. Tunaweza kukosea wengine ao wengine wanaweza kutukosea. Njo maana siye wote tuko na lazima ya kusamehe wengine na pia tuko na lazima wengine watusamehe. Wakati tunasamehe, tunaacha kuendelea kumukasirikia mutu mwenye alitukosea. ‘Hatumulipe uovu kwa uovu,’ na tunaepuka kuendelea kumukumbusha kila wakati makosa yenye alifanya ao uzaifu wenye iko nao. (Waroma 12:17) Halafu kama mutu alitukosea sana na tunashindwa kusahau mambo yenye alitufanyia? Ile wakati, ni muzuri kuenda kuongea naye. Tufanye vile kwa heshima na wakati tuko tu siye wawili. Na wakati tuko naongea, kusudi yetu inapaswa kuwa kufanya amani, hapana kutafuta kuonyesha mwenye iko na sheria na mwenye iko na kosa.​—Waroma 12:18.

Ukuwe Munyenyekevu na Mwenye Kuonyesha Heshima

“Kwa unyenyekevu muone wengine kuwa wazuri zaidi kuliko ninyi.”​—WAFILIPI 2:3.

Kama tuko wanyenyekevu na wenye kuonyesha heshima, wengine watapenda kuwa pamoja na siye, juu wanajua kama tutawatendea muzuri, tutawahangaikia, na hatutawakosea kimakusudi. Lakini kama tunajiona kuwa wa maana kuliko wengine, ao kama tunapenda kila wakati wakuwe wanafuata tu mambo yenye tunasema, tutakosa kuelewana na tutafikia hata kukasirikiana. Tena, watu watatuepuka, hatutakuwa na marafiki wengi, ao tutafikia kabisa kukosa marafiki.

Usikuwe na Ubaguzi

“Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.” ​—MATENDO 10:34, 35.

Muumbaji wetu haone watu fulani kuwa wa maana kuliko wengine juu ya inchi yao, luga yao, hali yao ya maisha ao rangi yao ya ngozi. “Kutoka kwa mutu mumoja, alifanya kila taifa la watu.” (Matendo 17:26) Ni kusema, watu wote ni ndugu na dada. Kwa hiyo wakati tunatendea watu muzuri na kwa heshima, watafurahi, na siye tutafurahi na Muumbaji wetu pia atafurahi.

Ukuwe Mupole

“Muvae . . . upole.”​—WAKOLOSAI 3:12.

Kama tuko wapole, tutafanya wengine wajisikie muzuri. Watajisikia huru kuongea na siye na hata kuturekebisha juu wanajua kama tutaendelea kuwa wenye kutulia. Na wakati mutu anatukasirikia, jibu yetu ya upole inaweza kumufanya atulie. Mezali 15:1 inasema hivi: “Jibu la upole linatuliza kasirani kali, Lakini neno la ukali linachochea hasira.”

Ukuwe na Roho ya Kutoa na Ukuwe Mwenye Shukrani

“Kuko furaha zaidi katika kutoa kuliko katika kupokea.”​—MATENDO 20:35.

Leo, watu wengi wako na pupa na wanapendaka wao tu njo wapewe. Lakini, tutakuwa na furaha ya kweli kama tuko na roho ya kutoa. (Luka 6:38) Watu wenye wako na roho ya kutoa wanakuwaka na furaha juu wanapendaka watu kuliko kupenda vitu. Ile upendo njo inawachocheaka waonyeshe shukrani wakati mutu anawapatia kitu fulani. (Wakolosai 3:15) Ujiulize hivi: ‘Napendaka kuwa pamoja na watu wenye hawapanake na wenye hawaonyeshake shukrani ao napendaka kuwa pamoja na watu wenye kuwa na roho ya kutoa na wenye wanaonyeshaka shukrani?’ Ile inatufundisha nini? Ukuwe vile unapenda wengine wakuwe.​—Matayo 7:12.