Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

DUNIA ITAOKOKA KABISA?

Hewa

Hewa

TUKO na lazima ya hewa, lakini haiko tu juu ya kupumua. Hewa inalindaka dunia yetu na miale (rayons) za jua zenye kuwa hatari. Bila hewa, hapa ku dunia kungekuwa baridi sana.

Mambo Yenye Kuharibisha Hewa

Hapa ku dunia, kuharibika kwa hewa kunaweza kutia uzima mu hatari. Shirika ya Afya ya Ulimwengu inaonyesha kama ni watu kidogo tu ku dunia njo wanapumuaka hewa yenye kuwa safi.

Kuharibika kwa hewa kunaweza kuleta magonjwa ya kupumua, kansere ya mapafu (cancer du poumon), na magonjwa ya moyo. Kila mwaka, kuharibika kwa hewa kunafanyaka watu 7 000 000 hivi wakufe mbele ya wakati.

Dunia Iliumbwa Juu Iendelee Kuwa

Dunia iliumbwa juu itolee kila kiumbe yenye kuwa hapa ku dunia hewa mingi yenye kuwa safi. Lakini inaweza kufanya vile tu kama wanadamu hawaharibishe hali ya hewa. Fikiria mifano fulani.

  • Watu wengi wanajua muzuri kama mapori inakuwaka na uwezo wa kukokota diokside ya karbone mu hewa. Lakini ni watu kidogo tu njo wanajua kama mu maeneo yenye kuwa karibu na bahari kunakuwaka miti yenye kuitwa mangrove yenye inaweza kukokota muzuri zaidi diokside ya karbone kupita hata misitu ya mvua (forêt tropicale). Miti ya mangrove inaweza kukokota diokside ya karbone mu hewa mara tano kushindia hata vile misitu ya mvua inaweza kufanya.

  • Uchunguzi fulani wenye ulifanywa hivi karibuni unaonyesha kama mimea fulani mikubwa yenye kuitwa varech inakokotaka diokside ya karbone mu angahewa lakini pia inaizikaka. Sehemu ya varech yenye kufanana majani inakuwaka na mifuko kidogo-kidogo mwenye munakuwaka hewa yenye inaisaidia itambale na iende mbali sana. Wakati ile mifuko inapasuka ikiwa mbali na plage, varech inayala diokside ya karbone na inazama chini ya bahari. Bila shaka mule inabakiaka yenye kuzikwa kwa miaka mingi.

  • Uwezo wa angahewa wa kutosha vitu mbalimbali vyenye kuichafua ulionekana wazi mu kipindi ya korona wakati hatukukuwa natoka inje. Mu 2020, wakati izine za mu dunia na magari mingi iliacha kabisa kutumika, bila kukawia, hewa ikakuwa muzuri zaidi. Kulingana na ripoti ya mu 2020 yenye inahusu hali ya hewa ya mu dunia, zaidi ya asilimia 80 (80%) ya mainchi kwenye uchunguzi ulifanyiwa, ilionekana kama mu ile mainchi, hali ya hewa ilikuwa muzuri wakati kidogo tu kisha watu kuanza kubakia ku nyumba juu ya ugonjwa wa korona.

Mambo Yenye Iko Nafanyika

Kutumia kinga kunasaidia kupunguza kuharibika kwa hewa

Guvernema zinaendelea kuambia izine zenye kuharibisha hali ya hewa zipunguze kufanya vile. Tena, wanasayansi wanaendelea kuvumbula njia mbalimbali juu ya kufanya uharibifu wa hali ya hewa usikuwe na matokeo ya mubaya. Kwa mufano, njia moya yenye wanatumia ni kufanya mikrobe igeuze vitu vyenye kuharibisha hali ya hewa visikuwe hatari. Tena, wenye kuwa na elimu wanashauria watu watembee na mugulu ao kutembea na kinga kuliko kutembea na gari. Na pia, wanashauria watu wasitumie courant mingi ku nyumba.

Guvernema fulani ziko napatia watu jiko ya kupikia ya sasa juu ya kupunguza kuharibika kwa hali ya hewa. Hata vile watu wengi hawayaipata

Lakini kuko mambo ingine mingi yenye inaomba kufanya. Vile njo ripoti ya 2022 za shirika mbalimbali za mu dunia ilionyesha, kutia ndani Shirika ya Afya ya mu Dunia (Organisation Mondiale de la Sante) na Banke ya mu Dunia. (Banque Mondiale)

Ile ripoti inaonyesha kama mu 2020, karibu asilimia 33 (33%) ya watu mu dunia wako natumikisha vitu vyenye viko naharibisha hewa wakati wanapiga. Mu maeneo mingi, ni watu kidogo tu njo wanaweza kuuza jiko (réchaud) za mupya na kutumikisha vitu vingine vyenye vinaweza kuwakisha moto (combustible).

Sababu Zenye Kutupatia Tumaini—Mambo Yenye Biblia Inasema

“Mungu wa kweli, Yehova, Muumbaji wa mbingu na . . . Yeye mwenye kutandika dunia na mazao yake, Yeye mwenye kupatia pumuzi watu wenye kuwa juu yake.”—Isaya 42:5.

Mungu aliumba hewa yenye tunapumua na mizunguko mbalimbali ya kuisafisha. Tena, iko na nguvu yenye haina mwisho na anapenda sana wanadamu. Sasa, unawaza kama ataacha tu hewa iendelee kuharibika bila kufanya kitu? Ona habari “Mungu Anaahidi Kama Dunia Itaokoka Kabisa.”