Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

DUNIA ITAOKOKA KABISA?

Mapori

Mapori

WANASAYANSI fulani wanalinganisha mapori na mapafu (poumons) yenye inafanyaka mutu aendelee kuishi. Juu ya nini? Sawa vile mapafu, miti inachuyaka hewa. Miti inakokotaka diokside ya karbone yenye inaweza kutufanya mubaya. Kisha, inatokezaka oksijeni yenye ni sehemu ya maana sana ya hewa yenye tunapumua. Karibu asilimia 80 (80%) ya mimea na wanyama wanakuwaka mu mapori. Bila mapori hatuwezi kuishi.

Mambo Yenye Kuharibisha Mapori

Kila mwaka, mamiliare ya miti inakatwa, zaidi sana juu ya kulima ili kupata chakula. Tangu mwisho wa miaka ya 1940, nusu ya mapori ya mu dunia imepotea.

Wakati mapori inaharibiwa, mimea na wanyama wote wenye kuishi ndani, wanaharibiwa pia.

Dunia Iliumbwa juu Iendelee Kuwa

Mu maeneo ya mapori kwenye karibu miti yote ilikatwa, miti iko na uwezo wa ajabu sana wa kuota tena. Hivi karibuni wanasayansi walishangaa kuona namna mapori kwenye miti mingi ilikatwa, ilianza tena kujiotea mbiombio na mapori ikarudia tena mu hali ya muzuri. Fikiria mifano yenye kufuata:

  • Wanasayansi walifanya uchunguzi ili kuona mambo yenye inatokea mu maeneo ya mapori kwenye miti ilikatwa ili kupanda chakula, kisha wakati fulani watu wakaacha kupanda chakula mule. Uchunguzi wa maeneo 2 200 yenye kuwa mu Amerika na mu Afrika ya Mangaribi umeonyesha kama miti ya ile mapori inaweza kuota tena mu miaka kumi hivi.

  • Kulingana na utafiti wenye ulitolewa na gazeti Science, wachunguzi wanawaza kama mu miaka 100 hivi, ile mapori inaweza kurudia tena mu namna yenye ilikuwa mbele miti yenye kuwa ndani ikatwe.

  • Hivi karibuni, wanasayansi wa mu Brazili walijifunza ili kujua ikiwa mapori inaweza kuota tena mbio kama watu wanapanda miti ndani.

  • Kupatana na ile uchunguzi, National Geographic inatoa hii ripoti: “Wale wachunguzi walishangaa kuona kama haikukuwa lazima kupanda miti juu mapori irudie mbiombio mu hali yenye ilikuwa zamani.” Mu miaka tano tu, mu maeneo kwenye walifanyia uchunguzi, walijionea kama miti ilijiotea ayo peke bila mwanadamu kuipanda.

Mambo Yenye Iko Nafanyika

Mu dunia yote, watu wamejikaza kulinda mapori yenye iko na wamejikaza kutengeneza ile yenye ilikuwa ilishaharibika. Kulingana na habari moya ya Umoja wa Mataifa, matokeo ni kama mu miaka 25 yenye imepita, mu dunia yote, zaidi ya asilimia 50 (50%) ya mapori mingi haikukatwa kwa kulinganisha na vile mapori mingi ilikuwa nakatwa zamani.

Lakini ile mambo yote haitoshe ili kulinda mapori. Ripoti moya yenye ilitolewa na tengenezo Global Forest Watch inasema hivi: “Mu miaka kidogo yenye imepita, hesabu ya misitu ya mvua (forêt tropicale) yenye iko naharibiwa haibadilike sana.”

Kompanyi zenye zinakata miti bila ruhusa ya guvernema zinapataka mamiliare ya dolare. Na ile njo inafanya misitu ya mvua ya mingi iendelee kuharibiwa.

Kikundi fulani ya watu inatumika pamoya juu ya kulinda mapori kwa kukata miti kidogo yenye kukomala na kupanda ya mupya

Sababu Zenye Kutupatia Tumaini —Mambo Yenye Biblia Inasema

“Yehova a Mungu akaotesha juu ya udongo kila muti wenye kupendeza macho na wenye kufaa kwa chakula.”—Mwanzo 2:9.

Muumbaji aliumba mapori na uwezo wa kujifanya uendelee kuwa mu hali ya muzuri juu tuendelee kufaidika nayo. Anapenda kuilinda na kuifanya iendelee kuwa mu hali ya muzuri pamoya na mimea na wanyama wenye kuwa ndani.

Biblia inaonyesha kama Mungu hataruhusu wanadamu waharibishe kabisa dunia na viumbe vyenye uzima vyenye kuwa ndani. Ona habari “Mungu Anaahidi Kama Dunia Itaokoka Kabisa,” ku ukurasa wa 15.

a Yehova njo jina ya pekee ya Mungu.—Zaburi 83:18.