Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Juu ya Nini Batu Habaheshimie Tena Uzima?

Juu ya Nini Batu Habaheshimie Tena Uzima?

JUU YA NINI NI JAMBO MAANA KUHESHIMIA UZIMA?

Wakati unafanya mambo yenye kuharibisha afya yako ao yenye kutia mu hatari afya ya bengine, ile inaonyesha kama hauone uzima wako na wa bengine kuwa wa maana.

  • Tumbako hailetake tu kansere, lakini inaharibishaka pia uwezo wa mwili wa kupiganisha ule ugonjwa. Karibu asilimia 90 (90%) ya batu benye banakufaka na kansere ya mapafu, banaipataka juu ya kuvuta ao juu ya kuishi fasi kwenye batu banavutaka.

  • Mauaji yenye kufanyiwa fasi ya batu mingi, kila mwaka inafanyaka batu mingi bashuke moyo sana. Ripoti moya ya Stanford University inasema hivi: “Uchunguzi moya ulionyesha kama hata bale benye habalumie mu mauaji fulani yenye kufanyika ku masomo, banaendeleaka tu kukumbuka bya mubaya byenye bilifanyika, na ile inaweza kubahangaisha sana hata kisha miaka mingi.”

  • Batu benye banatembezaka na balishakunywa ao balishatumia dawa za kulewesha banafanyaka ikuwe hatari kwa bengine benye kutembeza ao hatari kwa benye kutembea na mugulu. Wakati batu habaheshimie uzima, ile inaweza kufanya batu benye habakufanya kitu bapate matokeo ya mubaya.

MAMBO YENYE UNAWEZA KUFANYA

Ulinde afya yako. Haiyakuwaka kuchelewa kuacha kufanya mambo ya mubaya, sawa vile kuvuta tumbako ao tumbako ya kielektroniki, kukunywa pombe kupita kiasi, ao kutumia dawa za kulewesha juu tu ya kujifurahisha. Kufanya ile mambo, inaweza tu kuharibisha maisha yako na inaonyesha kama hauheshimie uzima wa batu benye banaishi pembeni yako, kutia ndani batu ya familia yako.

“Tujisafishe kila uchafu wa mwili.”—2 Wakorinto 7:1.

Ufikirie usalama wako na wa bengine. Juu ya kuepuka hatari, ulinde nyumba yako mu hali ya muzuri. Ufikirie usalama wakati uko natembeza na ulinde gari ao moto yako mu hali ya muzuri. Usiache bengine bakusukume ufanye mambo yenye inaweza kukuletea hatari ya nguvu sana ao kifo.

“Kama unajenga nyumba mupya, unapaswa pia kujenga ukuta mufupi kwa ajili ya sehemu ya juu ya nyumba yako, ili usilete hatia ya damu juu ya nyumba yako kwa sababu ya mutu kuanguka kutoka kwenye nyumba yako.”—Kumbukumbuku la Torati 22:8. a

Utendee bengine muzuri. Kuheshimia uzima inamaanisha pia kutendea muzuri batu ya rangi ya ngozi mbalimbali, batu ya inchi mbalimbali, ikuwe biko batajiri ao bamaskini, benye kusoma sana ao hapana. Juu ya nini ni jambo ya maana kufanya vile? Juu mara mingi, ubaguzi na chuki njo inaanzishaka matendo ya jeuri na vita mu dunia.

“Muondoe kutoka kwenu kila namna ya uchungu wenye uovu, hasira, kasirani kali, kufoka, matukano, na kila jambo lenye kuumiza. Lakini mukuwe wenye fazili ninyi kwa ninyi.”—Waefeso 4:​31, 32.

MAMBO YENYE TUKO NAFANYA

Mashahidi wa Yehova wanasaidiaka wengine kuwa na afya ya muzuri. Programu yetu ya kufundisha batu Biblia imebasaidia kupiganisha utumwa wa tabia za mubaya.

Tunafuataka kanuni za usalama mu kazi yetu ya ujenzi. Bajitoleaji benye banasaidiaka kujenga fasi zetu za mikusanyiko na majengo ingine yenye inatumiwa juu ya kuendelesha kazi ya kufundisha batu Biblia, banapataka mazoezi juu ya kuepuka aksida. Majengo yetu inachunguziwaka kwa ukawaida juu ya kuona kama inafuata kanuni za usalama za mu inchi.

Tunasaidiaka batu benye banapatwa na misiba. Mu 2022, tulitumia dolare milioni 12 hivi ya michango ya kujipendea juu ya kusaidia bale benye balipatwa na misiba ya asili mu maeneo 200 hivi mu dunia yote.

Wakati ugonjwa wa Ebola ulianza kuenea ku batu ya Mashariki ya Afrika mu 2014 na mu Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo mu 2018, tulifasiria batu bya kufanya juu ule ugonjwa wenye kuleta kifo usienee. Tulituma waakilishi juu ya kuongea na batu kuhusu habari “Utii Unaokoa Uzima.” Tulitia ku maingilio ya fasi yetu ya ibada maji ya kunawa mikono na tulifasiria batu ulazima wa kunawa mikono na mambo ingine yenye banaweza kufanya juu ya kuzuia ule ugonjwa usienee.

Mu Sierra Leone, chaîne moya ya radio ilipongeza Mashahidi wa Yehova juu walisaidia Mashahidi na wenye hawako Mashahidi wajue namna ya kuepuka virusi ya Ebola.

Fasi ya kunawia mikono ku Jumba ya Ufalme ya mu Liberia mu kipindi ya Ebola mu 2014

a Mu eneo ya Mashariki ya Kati ya zamani, ile sheria yenye kuwa na hekima ilionyesha namna Yehova anahangaikia usalama wa batu ya familia na wa bengine.