Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Juu ya Nini Ni Jambo ya Maana Kuamini Kama Kuko Muumbaji?

Juu ya Nini Ni Jambo ya Maana Kuamini Kama Kuko Muumbaji?

Juu ya nini ni jambo ya maana kujua jibu ya ile ulizo? Kama ushuhuda mbalimbali unakusaidia uamini kama kuko Mungu, unaweza pia kupenda kuchunguza mambo yenye kuhakikisha kama yeye njo aliandikishaka Biblia. Na kama unaamini mambo yenye Biblia inasema, unaweza kufikia kupata faida mbalimbali zenye kuwa hapa chini.

Utafurahia maisha zaidi

BIBLIA INASEMA: ‘[Mungu] alitenda mema, aliwapatia ninyi mvua kutoka mbinguni na vipindi vya kuzaa matunda, na kuwapatia chakula kwa wingi na kujaza mioyo yenu furaha.’​—Matendo 14:17.

ILE IKO NA MAANA GANI?: Kila kitu yenye unafurahia mu vitu vyenye viliumbwa vyenye viko mu dunia, ni zawadi yenye Muumbaji ametupatia. Utafurahia zile zawadi hata zaidi, kama unafikia kuelewa namna mwenye alitupatia zile zawadi anakuhangaikia kabisa.

Utapata mashauri ya muzuri, yenye inaweza kukusaidia mu maisha

BIBLIA INASEMA: “Utaelewa mambo ya uadilifu na ya haki na yenye kunyooka; njia yote ya mambo ya muzuri.”​—Mezali 2:9.

ILE IKO NA MAANA GANI?: Juu Mungu njo alituumba, yeye njo anajua mambo yenye tuko nayo lazima juu tukuwe na furaha. Kama unachunguza mambo yenye Biblia inafundisha, unaweza kujifunza mambo mingi yenye itakusaidia mu maisha.

Utapata majibu ya maulizo yako

BIBLIA INASEMA: “Utapata ujuzi juu ya Mungu.”​—Mezali 2:5.

ILE IKO NA MAANA GANI?: Kujua kama kuko Muumbaji, kunaweza kukusaidia upate majibu ya maulizo ya maana, yenye watu wanajiulizaka. Kwa mufano: Juu ya nini tunaishi? Juu ya nini kuko mateso ya mingi? Mutu mwenye anakufa iko mu hali gani? Unaweza kupata majibu ya kweli mu Biblia.

Utakuwa na tumaini

BIBLIA INASEMA: “‘Ninajua muzuri mawazo yenye ninafikiria kuwaelekea ninyi,’ ni vile Yehova anasema, ‘mawazo ya amani, na hapana ya musiba, ili kuwapatia ninyi wakati wenye kuja wa muzuri na tumaini.’”​—Yeremia 29:11.

ILE IKO NA MAANA GANI?: Mungu anatuambia kama mu siku zenye ziko nakuya atamaliza mambo ya mubaya, mateso, na hata kifo. Wakati unaamini ahadi ya Mungu, utatumaini kama maisha itakuwa muzuri mu siku zenye ziko nakuya. Na ile itakusaidia ukuwe na nguvu ya kupiganisha magumu yenye uko napata.