Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mambo Yenye Wanasayansi Hawawezi Kutuambia

Mambo Yenye Wanasayansi Hawawezi Kutuambia

Inaonekanaka sawa vile wanasayansi walishakajifunza kila kitu juu ya ulimwengu. Lakini, kusema kweli, kuko maulizo mingi yenye hawawezi kujibia.

Wanasayansi walishakaonyesha namna ulimwengu na vitu vyenye uzima vilianzaka? Kwa kifupi jibu ni hapana. Watu fulani wanasema kama elimu fulani yenye kuitwa kosmolojia inaweza kutufasiria namna ulimwengu ulianzaka. Lakini, ona mambo yenye Marcelo Gleiser alisema. Yeye ni profesa wa mambo ya anga ku masomo ya Dartmouth, na anaamini kama haiwezekane kujua ikiwa Mungu anakuwaka ao hapana. Alisema hivi: “Hatuyawezaka hata kidogo kufasiria namna ulimwengu ulianzaka.”

Vilevile, habari moja mu gazeti Science News inasema hivi kuhusu namna vitu vyenye uzima vilianzaka: “Inaweza kuwa nguvu kujua namna vitu vyenye uzima vilianzaka ku Dunia, juu majiwe na vitu vingine vyenye tungeweza kuchunguza juu ya kutusaidia kujua namna mambo ilikuwaka wakati Dunia ilianza, vilishakapotea.” Ile maneno inaonyesha kama sayansi haiyawezaka kuonyesha namna ulimwengu na vitu vyenye uzima vilianzaka.

Lakini unaweza kujiuliza, ‘Kama vitu vyenye uzima vyenye kuwa mu dunia vilifanywa, nani njo alivifanya?’ Pengine pia ulishakajiuliza hii maulizo: ‘Kama kuko Muumbaji mwenye hekima na mwenye upendo, juu ya nini anaacha watu wenye aliumba wateseke? Juu ya nini anaacha watu wamuabudu mu njia mbalimbali zenye kutofautiana? Juu ya nini anaacha watu wenye kumuabudu wafanye mambo mingi ya mubaya?’

Sayansi peke yake haiwezi kujibia ile maulizo. Lakini ile haimaanishe kama hauwezi kupata majibu yenye kufaa. Kusema kweli, watu wengi walishakapata majibu yenye kufaa mu Biblia.

Ukipenda kujua juu ya nini wanasayansi fulani wenye walishakajifunza Biblia wanasema kuwa wanaamini kama kuko Muumbaji, fungua jw.org. Kwenye sehemu ya kutafutia, andika maneno: “Maoni Mbalimbali Kuhusu Mwanzo wa Uzima.