Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | DUNIA HII ITAOKOKA AO HAPANA?

Dunia hii Itaokoka ao Hapana?

Dunia hii Itaokoka ao Hapana?

MWAKA wa 2017 ulianza na tangazo la mubaya la wanasayansi. Katika Mwezi wa 1, kikundi kimoja cha wanasayansi kilitangaza kwamba dunia inakaribia sana musiba mubaya zaidi wenye haujatokeaka. Kwa kutumia Saa ya Mwisho wa Dunia ili kuonyesha namna dunia inakaribia mwisho, wanasayansi walipeleka mbele, kwa segonde 30, mukuki wa kuonyesha dakika. Kwa sasa, Saa ya Mwisho wa Dunia iko kwenye saa 6 ya usiku kosa dakika mbili na nusu (23:57:30), ni kusema, karibu zaidi na musiba wa ulimwengu muzima kuliko wakati wowote katika kipindi cha miaka 60!

Katika mwaka wa 2018, wanasayansi wanapanga kupima tena kadiri gani tuko karibu na mwisho wa dunia. Saa ya Mwisho wa Dunia itaendelea kuonyesha kwamba musiba mukubwa kuliko yote unakaribia sana? Unawaza namna gani? Dunia hii itaokoka? Pengine unaona kwamba iko nguvu kupata majibu ya maulizo haya. Hata wanasayansi wako na mawazo tofauti kuhusu jambo hilo. Haiko kila mutu ndiye anaamini hatari hiyo yenye haiwezi kuepukwa.

Kwa kweli, mamilioni ya watu wanatumainia wakati muzuri wenye kuja. Wanaamini kwamba wako na mambo yenye kuhakikisha kwamba wanadamu na dunia wataokoka milele na maisha yetu yatakuwa muzuri. Unaweza kuamini mambo hayo? Dunia hii itaokoka ao hapana?