Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mungu Alitumia Mageuzi Juu ya Kuumba Vitu Vyenye Uzima?

Mungu Alitumia Mageuzi Juu ya Kuumba Vitu Vyenye Uzima?

Mungu Alitumia Mageuzi Juu ya Kuumba Vitu Vyenye Uzima?

[Kisanduku]

MAGEUZI NI NINI?

Maana moja ya neno “mageuzi” ni: “mabadiliko ya hatua kwa hatua.” Lakini, ile neno inatumiwaka mu njia mbalimbali. Kwa mufano, inatumiwaka juu ya kuzungumuzia mabadiliko makubwa ya vitu vyenye havina uzima, kama vile mabadiliko ya ulimwengu. Ile neno inatumiwaka pia juu ya kuzungumuzia mabadiliko ya kidogo-kidogo ya vitu vyenye kuwa na uzima, kama vile namna mimea na wanyama inajipatanishaka na fasi kwenye inaishi. Lakini, mara mingi ile neno inatumiwaka juu ya kuzungumuzia fundisho yenye kusema kama uzima ulitokana na vitu vyenye havina uzima, vyenye vilifanyiza chembe zenye zinaweza kujigawanya na kutokeza chembe za mupya. Kisha hatua kwa hatua zile chembe zikafikia kuwa viumbe mbalimbali vya hali ya juu, na mwanadamu njo alikuwa kiumbe mwenye akili zaidi mwenye alitokana na ile mabadiliko. Mu hii gazeti, neno “mageuzi” inapatana na ile maana ya tatu, yenye tumezungumuzia.