Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Tafuta Musaada

Tafuta Musaada

Tafuta Musaada

“Mutu anaweza kumushinda nguvu mwenye kuwa peke yake, lakini wawili wenye kuwa pamoja wanaweza kushindana naye.”​Muhubiri 4:12.

KAMA wengine wanatusaidia, tunaweza kupiganisha tatizo yoyote, hata ikuwe ya nguvu namna gani. Kwa hiyo, kama unapenda kuacha kuvuta, ni muzuri uombe watu wa familia yako na marafiki wako wakusaidie. Ao unaweza kuomba musaada mutu mwingine mwenye iko na nia kabisa ya kukusaidia na mwenye atakuvumilia.

Tafuta musaada wa watu wenye waliwezaka kuacha kuvuta tumbako, juu wanaweza kukuelewa na kukusaidia. Torben, Mukristo wa inchi ya Danemark, anasema hivi: “Musaada wa wengine ulikuwa wa maana sana.” Abraham, mwenye anaishi India, anaandika hivi: “Upendo wa kweli wenye watu wa familia yangu na Wakristo wenzangu walinionyesha ulinisaidia kuacha kuvuta tumbako.” Lakini wakati fulani, zaidi tu ya musaada wa watu wa familia na marafiki, unaweza kuwa na lazima ya kitu ingine.

Mwanaume mwenye kuitwa Bhagwandas anasema hivi: “Nilikuwa navuta kwa miaka 27, lakini juu nilijifunza mambo yenye Biblia inasema juu ya tabia chafu, niliamua kuacha. Nilijaribu kupunguza kiasi ya tumbako yenye nilikuwa navuta, nikaachana na marafiki fulani, na nikaenda kuonana na wanganga. Lakini ile mambo yote haikunisaidia. Ku mwisho, usiku moya nilisali kwa Yehova na kumuambia mambo yote yenye ilikuwa mu moyo wangu. Nilimulilia anisaidie niache kuvuta tumbako. Ni kisha kufanya tu vile, njo niliweza kuacha kuvuta tumbako!”

Jambo ingine ya maana, ni kujitayarisha kwa ajili ya magumu yenye kuacha kuvuta tumbako kunaweza kuleta. Magumu gani? Tutaizungumuzia mu habari yenye kufuata.

[Kisanduku]

NI MUZURI UTUMIE DAWA?

Dawa za kusaidia watu kuacha kuvuta tumbako zimefanya wenye kuzitengeneza wakuwe matajiri sana. Lakini mbele ya kuamua kama utatumia zile dawa, fikiria hii maulizo:

Ziko na faida gani? Wale wenye kutetea zile dawa, wanasema kama zinasaidiaka mutu asijisikie mubaya sana wakati iko najaribu kuacha kuvuta tumbako. Lakini, watu wengi hawakubali kama zile dawa zinasaidiaka kabisa.

Ziko na hatari gani? Dawa fulani, zinafanyaka watu wasikie hamu ya kutapika, washuke moyo, na wakuwe na mawazo ya kujiua. Ujue kama zile dawa ni njia ingine tu ya kukupatia nicotine, bila kusahau kama zinatia afya yako mu hatari. Kwa hiyo, mutu mwenye kutumia zile dawa anabakiaka tu mutumwa wa nicotine.

Kuko mambo ingine yenye inaweza kusaidia? Mu uchunguzi fulani wenye ulifanywa, 88% ya watu wenye waliwezaka kuacha kuvuta tumbako, walisema kama waliachaka mara moya kuvuta tumbako bila kutumia dawa yoyote.