Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ujue Kama Utapata Magumu Wakati Utaacha Kuvuta Tumbako

Ujue Kama Utapata Magumu Wakati Utaacha Kuvuta Tumbako

Ujue Kama Utapata Magumu Wakati Utaacha Kuvuta Tumbako

“Niliamua kuacha kuvuta tumbako juu ya kulinda afya ya mutoto wetu mwenye alitoka tu kuzaliwa. Kwa hiyo, nilibandika mu nyumba yetu hii maandishi: ‘Hapana Kuvuta.’ Saa moya kisha kufanya vile, nilisikia hamu sana ya nicotine na nikawasha tumbako.”​—Yoshimitsu, Japan.

MAMBO yenye ilimufikia Yoshimitsu inaonyesha kama kuko magumu fulani yenye inaweza kufikia mutu wakati iko najaribu kuacha kuvuta tumbako. Zaidi ya ile, uchunguzi unaonyesha kama karibu 90% ya watu wenye wanajaribu kuacha kuvuta tumbako, wanarudiliaka ile tabia. Kwa hiyo, kama uko najikaza kuacha kuvuta tumbako, inawezekana uweze kufanya vile kama unajitayarisha kwa ajili ya magumu yenye inaweza kukufikia. Ni magumu gani njo inazoeaka kufikia mutu mwenye anajaribu kuacha kuvuta tumbako?

Hamu ya nicotine: Kwa kawaida, ile hamu inaongezekaka sana siku tatu kisha mutu kuacha kuvuta tumbako na inapungukaka kisha majuma mbili hivi. Mutu mumoja mwenye alikuwaka navuta zamani, anasema kama mu ile kipindi “hamu inakuyaka na inaenda; haikawiake.” Lakini hata kisha miaka mingi, kwa kushitukia unaweza kusikia hamu ya kuvuta. Kama unasikia tena ile hamu, usiwashe tumbako. Ngoya dakika tano hivi, na ile hamu itapita.

Magumu ingine: Ku mwanzo, mutu anaweza kuwa na magumu ya kubakia macho, kukaza akili juu ya jambo fulani, na anaweza kunenepa haraka. Anaweza pia kusikia maumivu fulani, mwili kuwasha, kutokwa jasho, kukohoa-kohoa, na pia anaweza kukosa uvumilivu, kukasirika haraka, ao hata kushuka moyo. Lakini, ile mambo yote inapungukaka kisha majuma ine ao sita hivi.

Kama uko mu ile hali, kuko mambo fulani yenye inaweza kukusaidia. Kwa mufano:

● Ulale sana.

● Ukunywe maji mingi ao vinywaji vyenye vilitengenezwa na matunda, na ukule chakula ya kujenga mwili.

● Ufanye mazoezi kwa kiasi.

● Vuta pumuzi, na uwazie vile hewa ya muzuri iko naingia mu mapafu yako.

Mambo yenye inaweza kukuletea hamu ya kuvuta: Kuko mambo fulani ao hisia fulani zenye zinaweza kukufanya ukuwe na hamu ya kuvuta. Kwa mufano, pengine ulikuwa unazoea kuvuta tumbako wakati ulikuwa nakunywa pombe. Kama ni vile, wakati uko unakunywa ile pombe, usikawie sana. Kisha wakati fulani, saa utakuwa ulishaacha kuvuta, unaweza kuanza kufurahia tena pombe yako polepole.

Hata kama mu mwili yako hamuna tena nicotine, unaweza kusikia hamu ya kuvuta wakati uko nafanya mambo fulani. Torben, mwenye tulishazungumuzia, alisema hivi: “Nimeacha kuvuta kumepita miaka kumi na kenda, lakini ningali nasikia hamu ya kuvuta wakati wa mapumuziko ku kazi.” Lakini kwa kawaida, kisha wakati fulani, ile hamu inapoteaka polepole na mutu hataisikia tena wakati iko nafanya mambo fulani.

Lakini ile hamu haipoteake wakati mutu iko nakunywa pombe. Njo maana, kama uko najikaza kuacha kuvuta tumbako, inaweza kuwa muzuri uache kunywa pombe na uepuke fasi za kukunywia pombe. Juu watu wengi wenye wanarudiliaka tabia ya kuvuta tumbako, wanafanyaka vile saa wako nakunywa pombe. Juu ya nini?

● Hata kiasi kidogo tu ya pombe inafanyaka mutu ajisikie muzuri, sawa vile mutu anajisikiaka kisha kutumia nicotine.

● Mara mingi watu wanavutaka wakati wako nakunywa na marafiki wao.

● Mara mingi mutu hakamatake maamuzi ya muzuri kama alishakunywa pombe na anafanyaka mambo yenye hangefanya. Njo maana Biblia inasema hivi: ‘Divai . . . inaondoa nia ya kufanya mambo yenye kuwa sawa.’​—Hosea 4:11.

Marafiki: Uchague muzuri marafiki wako. Kwa mufano, uepuke watu wenye wanavutaka, wenye wanaweza kukupatia tumbako juu na weye uvute. Tena, uepuke watu wenye wako nakuvunja moyo. Kwa mufano, kwa kukuchekelea juu uko najikaza kuacha kuvuta tumbako.

Hisia: Uchunguzi fulani unaonyesha kama 66% ya watu wenye walirudilia tabia ya kuvuta tumbako, walifanya vile wakati walikuwa na mahangaiko ao wakati walikasirika sana. Kama hisia fulani inafanya usikie hamu ya kuvuta, fanya jambo ingine. Kwa mufano, kunywa maji, tafuna bazoka, ao uende utembee kidogo. Ujikaze kufikiria mambo ya muzuri. Kwa mufano, unaweza kusali kwa Mungu ao kusoma maandiko fulani ya Biblia.​—Zaburi 19:14.

Visingizio vya Kuepuka

Nitakokota tu mara moya na basi.

Kweli njo hii: Kama unakokota tu mara moya, unaweza kupata nusu ya nicotine yenye ubongo wako uko nayo lazima kwa saa tatu. Mara mingi ile inafanyaka mutu aanze tena kuvuta tumbako.

Kuvuta tumbako kunanisaidiaka nitulie.

Kweli njo hii: Uchunguzi unaonyesha kama nicotine inafanyaka mutu akuwe na mahangaiko zaidi. Ile kusikia kama mutu anatulia kisha kuvuta tumbako, mara mingi inakuwaka juu mutu anapatia mwili wake nicotine yenye ulikuwa nayo lazima.

Miye tumbako ilishakaniingia mu damu, siwezi tena kuacha.

Kweli njo hii: Kuwaza kama hautaweza kuacha kunaweza kukuvunja moyo. Biblia inasema hivi: “Kama unavunjika moyo siku ya taabu, nguvu zako zitakuwa kidogo.” (Mezali 24:10) Njo maana, usiwaze kama hautawezaka kuacha kuvuta tumbako. Kila mutu mwenye anapenda kabisa kuacha kuvuta tumbako na mwenye anatumikisha mashauri ya muzuri sawa vile yenye iko mu hizi habari, anaweza kabisa kuacha.

Sitaweza kuvumilia magumu yenye nitapata wakati nitaacha tumbako.

Kweli njo hii: Ni kweli kama magumu yenye kuacha kuvuta tumbako inaletaka inaweza kuwa nguvu. Lakini, itapunguka kisha majuma fulani tu. Kama unasikia tena hamu ya kuvuta kisha miezi fulani ao miaka fulani, ile hamu nayo itapita. Pengine mu dakika fulani; kama tu hauwashe tumbako.

Niko na ugonjwa wa akili.

Kweli njo hii: Kama uko na ugonjwa fulani wa akili, ambia munganga wako akuambie mambo yenye unaweza kufanya juu uache kuvuta tumbako. Anaweza kuwa tayari kukusaidia, pengine kwa kukupatia dawa ingine.

Kama ninavuta tena, nitajiona wa bure.

Kweli njo hii: Kama unarudilia tena tabia ya kuvuta tumbako, ile haimaanishe kama umeshindwa kabisa. Ile inafikiaka watu wengi wenye wako najaribu kuacha kuvuta tumbako. Usivunjike moyo, endelea tu kujikaza. Kuanguka haiko kushindwa. Kubakia chini njo kushindwa. Kwa hiyo, usichoke. Ku mwisho utaweza tu!

Fikiria mufano wa Romualdo, mwenye alikuwa navuta kwa miaka 26, na kumepita sasa miaka 30 tangu aache kuvuta. Anaandika hivi: “Sikumbuke hata mara ngapi njo nilirudiliaka tena na tena kuvuta tumbako. Kila mara nilikuwa najisikia mubaya sana na kuwaza kama sitawezaka. Lakini wakati niliamua kabisa kuwa na urafiki na Yehova Mungu na kumuomba mara kwa mara anisaidie, nilifikia kuacha kuvuta tumbako.”

Mu habari yenye kufuata, tutaona mashauri ingine yenye itakusaidia ukuwe na furaha kisha kuacha kuvuta tumbako.

[Kisanduku/​Picha]

TUMBAKO NI HATARI HATA IKUWE YA AINA GANI

Tumbako inatumiwaka mu njia mbalimbali. Kuko hata tumbako yenye inauzishiwaka mu maduka ya kuuzishia chakula na mu maduka ya kuuzishia dawa. Lakini, sawa vile Shirika ya Afya Ulimwenguni inasema, aina zote za tumbako ni hatari. Magonjwa mingi yenye inatokanaka na tumbako, sawa vile kansere ao magonjwa ya moyo, inaweza kuua. Tena, kama mama mwenye iko na mimba anavuta, anaweza kutia afya ya mutoto wake mu hatari. Ni aina gani mbalimbali za tumbako zenye watu wanatumiaka?

Bidis: Ni tumbako za kidogo kidogo zenye zinatengenezwaka na mukono. Zinatumiwaka sana mu inchi za Asia. Wakati mutu anazivuta, mara mingi anapataka lami (ao goudron) ya mingi, nicotine ya mingi, na monokside ya karbone ya mingi, kupita hata tumbako za kawaida.

Diri ao Cigars: Ni tumbako yenye mutu yeye peke anajifungiaka kwa kutumia majani ya tumbako ao karatasi yenye kutengenezwa na tumbako. Namna diri imetengenezwa, inafanya ikuwe mwepesi nicotine kuingia mu mwili hata wakati diri haiyawashwa.

Kreteks, ao tumbako zenye kuongezwa clou de girofle: Kwa kawaida, zinakuwaka na 60% ya tumbako na 40% ya clou de girofle. Wakati mutu anazivuta anapata lami (ao goudron) ya mingi, nicotine ya mingi, na monokside ya karbone ya mingi kupita tumbako za kawaida.

Pipe: Kuvuta pipe ni hatari sawa tu vile kuvuta tumbako, juu yote mbili inaweza kuletea mutu kansere na magonjwa ingine.

Tumbako yenye haina moshi: Kuko tumbako ya kutafuna, ya kunusa, na gutkha, yenye inatumiwaka kusini-mashariki mwa Asia. Wakati mutu anaitumia, nicotine inaingia mu damu, kupitia kinywa. Tumbako yenye haina moshi, iko tu hatari sawa vile tumbako zingine.

Tumbako yenye inavutwa kupitia maji. (bongs, hookahs, narghiles, shishas): Moshi ya tumbako inapitaka mu maji mbele mutu aivute. Lakini ile haipunguzake sumu ya tumbako na haipunguzake vitu vyenye kuleta kansere vyenye vinaingiaka mu mapafu.

[Kisanduku/​Picha]

NAMNA YA KUSAIDIA MUTU AACHE KUVUTA TUMBAKO

Usimuchambue-chambue. Kumusifu na kumupongeza kunaweza kumusaidia sana kuliko kumuchambua-chambua. Ni muzuri zaidi kumuambia: “Nawaza utaweza kama unajaribu tena,” kuliko kumuambia: “Unashindwa tena!”

Ukuwe tayari kusamehe. Kama mutu mwenye iko najikaza kuacha kuvuta tumbako anakukasirisha usimuwekee kinyongo. Umuambie maneno ya upole sawa vile: “Najua haiko mwepesi, lakini nafurahi sana kuona vile uko najikaza.” Hata siku moya usimuambie: “Ulikuwaka mutu muzuri zaidi saa ulikuwaka navuta!”

Ukuwe rafiki wa kweli. Biblia inasema hivi: “Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.” (Mezali 17:17) “Nyakati zote,” ujikaze kuonyesha uvumilivu na upendo mutu mwenye iko najikaza kuacha kuvuta tumbako; hata ikuwe saa gani, ao akuwe mu hali gani.