Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KUULIZWA MAULIZO | RACQUEL HALL

Mwanamuke Muyahudi Anaeleza Sababu Yenye Ilifanya Achunguze Tena Imani Yake

Mwanamuke Muyahudi Anaeleza Sababu Yenye Ilifanya Achunguze Tena Imani Yake

Racquele alizaliwa na mama Muyahudi wa Israeli na baba wa Austria mwenye alikuwa ameingia mu dini ya Wayahudi. Wazazi wa mama yake walikuwa mu kikundi ya kutetea haki za Wayahudi, na walihamia Israeli mu mwaka wa 1948, wakati inchi ya Israeli ilifikia kupata uhuru. Amuka! ilimuuliza Racquele nini njo ilifanya achunguze tena mambo yenye alikuwa naamini mu dini ya Kiyahudi.

Tuelezee namna ulikomala.

Nilizaliwa mwaka wa 1979 katika Amerika. Wakati nilikuwa na miaka tatu, wazazi wangu walivunja ndoa. Mama yangu alinifundisha desturi za kiyahudi na alinituma ku yeshivas, ao masomo za Kiyahudi. Wakati nilikuwa na miaka saba, tulihamia Israeli kwa mwaka moya, na kule nilikuwa naenda ku masomo yenye ilipatikana katika kibbutz, ni kusema eneo kwenye watu walikuwa nafanya kazi ya kulima. Kisha miye na mama yangu tulihamia Meksiko.

Hata kama kwenye tulikuwa naishi hakukukuwa sinagogi, niliendelea kufuata desturi za Kiyahudi. Nilikuwa nawasha mishumaa ao bougies kila siku ya sabato, nilikuwa nasoma Tora, na nilikuwa nasali kwa kutumia siddur, ao kitabu ya sala. Wakati nilikuwa ku masomo, mara mingi nilikuwa naambia wanafunzi wenzangu kama dini yangu njo ilianzaka. Nilikuwa siyasomaka ile yenye wanaitaka Agano Jipya, yenye inazungumuzia utumishi wa Yesu na mafundisho yake. Mama yangu alikuwa amenikataza kuisoma juu isiharibishe imani yangu.

Nini njo ilifanya uamue kusoma Agano Jipya?

Wakati nilieneza miaka 17, nilirudia Amerika juu nimalize masomo. Kule, mutu fulani mwenye nilikuwa najua, mwenye alikuwa Mukristo aliniambia kama kuko kitu yenye ninakosa mu maisha kama simujue Yesu.

Nilimujibia hivi: “Watu wenye wanamuamini Yesu wamepotea.”

Kisha akaniuliza: “Ulishakasoma Agano Jipya?”

Nikajibia: “Hapana.”

Kisha akasema: “Kama ni vile, hauone kama ni kosa kusema mawazo yako juu ya jambo yenye haujue muzuri?”

Maneno yake ilinigusa sana, juu nilikuwaka naona kama ni kukosa akili kutoa mawazo juu ya jambo yenye sijue muzuri. Nilijifunza somo ya maana ile siku, nikaenda na Biblia yake ku nyumba, na nikaanza kusoma Agano Jipya.

Mambo yenye ulisoma ilikusaidia namna gani?

Nilishangala kujua kama wenye waliandika Agano Jipya walikuwa Wayahudi. Pia, wakati niliendelea kusoma, nilitambua kama Yesu alikuwa Muyahudi muzuri, munyenyekevu, na mwenye alipenda kusaidia watu, hapana kuwatesa. Na hata nilienda ku nyumba ya kuuzishia vitabu na nikaomba vitabu vyenye vilizungumuzia Yesu. Lakini, hakuna kitabu yenye ilinihakikishia kama Yesu alikuwa Masiya. Na hata vitabu fulani vilisema kama alikuwa Mungu. Niliona kama ile haiwezekane kabisa juu kama Yesu alikuwa Mungu, alikuwa nasali kwa nani? Alikuwa nasali kwake yeye peke? Na zaidi ya ile, Yesu alikufaka. Lakini Biblia inasema hivi juu ya Mungu: “Wewe hauwezi kufa.” *

Namna gani ulipata majibu juu ya ile maulizo?

Kweli haiwezi kujipinga, njo maana niliamua kabisa kutafuta majibu ya kweli. Kwa hiyo, kwa mara ya kwanza nilisali kwa Mungu bila kutumia siddur, nilimulilia anisaidie. Wakati tu nilimaliza kusali, watu fulani waligonga ku mulango. Walikuwa Mashahidi wawili ku mulango. Walinipatia kichapo ya kusaidia kujifunza Biblia. Ile kichapo na mambo yenye nilizungumuza nao, ilinihakikishia kama mambo yenye wanaamini inatoka mu Biblia. Kwa mufano, hawaamini kama Yesu iko sehemu ya utatu, lakini wanaamini kama Yesu ni “Mwana wa Mungu” * na “mwanzo wa uumbaji wa Mungu.” *

Wakati fulani kisha pale, nilirudia Meksiko, na kule niliendelea kujifunza na Mashahidi wa Yehova kuhusu maunabii yenye kuzungumuzia Masiya. Nilishangala kuona kama kuko maunabii mingi sana yenye kuzungumuzia Masiya! Lakini, niliendelea kuwa na mashaka kidogo. Nilijiuliza hivi: ‘Yesu tu njo alitimiza ile maunabii yote? Ao alikuwa tu nacheza filme ya mambo yenye Biblia ilisemaka kuwa Masiya atafanya?’

Nini njo ilifikia kukuhakikishia kama Yesu alikuwa Masiya?

Mashahidi wa Yehova walinionyesha ma unabii yenye hakuna mutu anaweza kupanga itimie mu maisha yake. Kwa mufano, zaidi ya miaka 700 mbele Masiya azaliwe, nabii Mika alitabiri kama atazaliwa Betlehemu, katika Yudea. * Nani njo anapangaka fasi kwenye atazaliwa? Hakuna. Tena Isaya alitabiri kama watu wangemuua Masiya sawa mutu mwenye kosa, na kama angezikwa pamoya na matajiri. * Na ile mambo yote ilitimia mu maisha ya Yesu.

Jambo ingine yenye ilinihakikishia kama Yesu ni Masiya ni kizazi yenye alizaliwa ndani. Biblia ilikuwa ilishasema kama Masiya angetoka mu kizazi ya Mufalme Daudi. * Zamani, Wayahudi walikuwa naweka maandishi yenye ilionyesha vizazi. Kwa hiyo kama Yesu hangetoka mu kizazi ya Daudi, maadui wake hawangenyamanzia ile jambo! Lakini hawakusema kitu juu ilikuwa wazi kama Yesu alitoka mu kizazi ya Daudi. Na hata watu walikuwa namuita “mwana wa Daudi.” *

Mu mwaka wa 70, ni kusema miaka 37 kisha Yesu kufa, Waroma waliharibu Yerusalemu, na maandishi yote ya vizazi ikapotea ao ikaharibiwa. Kwa hiyo, Masiya alipaswa kutokea mbele ya mwaka ya 70 juu watu waweze kupata maandishi yenye ingehakikisha kama ni wa mu kizazi ya Daudi

Kujua ile mambo kulikusaidia namna gani?

Mu Kumbukumbu la Torati 18:18, 19, Mungu alisema kama atainua katika Israeli nabii mwenye kuwa kama Musa. Mungu alisema hivi: “Nitamuomba hesabu kila mutu mwenye hatasikiliza maneno yangu yenye nabii huyo atasema katika jina langu.” Kujifunza sana Biblia yote kulinisaidia nikuwe hakika kama ule nabii ni Yesu wa Nazareti.

^ Isaya 9:6, 7; Luka 1:30-32. Matayo sura ya 1 inaonyesha kizazi ya Yesu upande wa baba yake, na Luka sura ya 3, inaonyesha kizazi ya Yesu upande wa mama yake.