Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA

Adresi ya Internete Yenye Habari Nzuri Sana

Adresi ya Internete Yenye Habari Nzuri Sana
  • SOMA Biblia katika luga karibu 50 na habari zinazotegemea Biblia katika luga zaidi ya 500.

  • CHUNGUZA habari fulani katika luga za ishara karibu 70.

  • FUNGUA​-FUNGUA habari katika mamia ya luga.

  • SIKILIZA michezo inayotegemea Biblia inayoeleza matukio yenye kuchangamusha ya Biblia.

  • ONA masimulizi ya Biblia kuwa halisi kupitia hadisi zilizochorwa.

  • TAZAMA michezo inayotegemea Biblia na video ambazo zitakusaidia kupambana na matatizo ya maisha.

  • CHUKUA bila kulipa vitabu, habari za magazeti, na habari za kusikiliza.

  • TAFUTA habari mbalimbali kwa kutumia maktaba kwenye Internete (Watchtower ONLINE LIBRARY)​—njia ya kukusaidia kupata habari nyingi. Maktaba hiyo inapatikana katika luga zaidi ya 100.

KWA AJILI YA BIBI NA BWANA

“Ninapenda familia yangu iwe yenye furaha. Mimi na bibi yangu tumepata matatizo fulani katika ndoa yetu, na matatizo hayo yalikuwa magumu zaidi wakati tulizaa watoto. Tuna lazima ya musaada”

BIBLIA INASEMA HIVI:

‘Nyumba inajengwa kwa hekima, na kwa utambuzi itasimamishwa imara.’​—Methali 24:3.

SEHEMU FULANI ZENYE MAFAA ZA ADRESI YETU YA INTERNETE

Sehemu yenye kichwa “Bibi na Bwana & Wazazi” inaweza kukusaidia ushinde matatizo kama vile:

  • Jinsi ya kufaulu katika mwaka wa kwanza wa ndoa

  • Kushugulika na wakwe

  • Kuwatia watoto nizamu

  • Jinsi ya kuacha kugombana

  • Kushugulikia matatizo ya feza

(Fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > BIBI NA BWANA & WAZAZI)

Kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia kina habari nyingi zinazohusu familia, kuanzia kujitayarisha kwa ajili ya ndoa wakati mutu hajaoa ao kuolewa mupaka kufikia kuwatunza wazazi waliozeeka.

(Unaweza pia kupata kitabu hicho kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com. Fungua kichwa VICHAPO > VITABU & BROSHUA)

KWA AJILI YA WAZAZI

“Hakuna kitu cha maana kwangu kuliko watoto wangu. Ninapenda wakomae na kuwa watu wazima ambao ninaweza kujivunia”

BIBLIA INASEMA HIVI:

‘Umulee muvulana [ao kijana mwanaume] kulingana na njia inayomufaa; hata atakapozeeka hatageuka kando na kuiacha.’​—Methali 22:6.

SEHEMU FULANI ZENYE MAFAA ZA ADRESI YETU YA INTERNETE

Sehemu yenye kichwa “Watoto” ina sehemu kama vile hadisi za Biblia zilizochorwa, mazoezi ya picha, video, na ninajifunza Biblia; sehemu hizo zinaweza kukusaidia uwafundishe watoto wako . . .

  • kutii

  • kuonyesha fazili

  • kusikilizana na wengine

  • kusema “aksanti”

(Fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > WATOTO))

Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia na Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu ni vitabu vilivyo na picha nzuri vilivyochapishwa ili uvisome na watoto wako.

(Unaweza pia kupata vitabu hivyo kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com. Fungua kichwa VICHAPO > VITABU & BROSHUA)

KWA AJILI YA VIJANA

“Ningehitaji mashauri fulani ya kunisaidia kushugulikia mambo kama vile masomo, wazazi wangu, marafiki wangu, na vijana wanawake. Mimi si mutoto tena, kwa hiyo sihitaji kuambiwa kila mara jambo la kufanya”

BIBLIA INASEMA HIVI:

“Moyo wako ukufanyie mema siku za ujana wako.”​—Mhubiri 11:9.

SEHEMU FULANI ZENYE MAFAA ZA ADRESI YETU YA INTERNETE

Sehemu yenye kichwa “Vijana” ina habari na video zinazoweza kukusaidia . . .

  • ikiwa unajihisi mpweke

  • ikiwa una matatizo kwenye shule

  • ikiwa umevunja sheria za wazazi wako

  • ikiwa unaonewa ao unasumbuliwa kingono

(Fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > VIJANA))

Vitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza​—Majibu Yafanyayo Kazi (buku la 1 na la 2) vinazungumuzia maulizo 77 ya maana ambayo yanaulizwa sana.

(Unaweza pia kupata vitabu hivyo kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com. Fungua kichwa VICHAPO > VITABU & BROSHUA)

KWA AJILI YA WATU WANAOPENDA KUJIFUNZA BIBLIA

“Ningependa kuelewa Biblia. Nifanye nini?”

BIBLIA INASEMA HIVI:

“Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu nalo ni lenye faida kwa kufundisha.”​—2 Timotheo 3:16.

SEHEMU FULANI ZENYE MAFAA ZA ADRESI YETU YA INTERNETE

Biblia Takatifu​—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ni tafsiri isiyo na makosa na iliyo rahisi kusoma.

(Fungua kichwa VICHAPO > BIBLIA))

Sehemu yenye kichwa “Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa” inajibu waziwazi maulizo kuanzia “Sababu gani Mungu aliruhusu maangamizi ya Wayahudi?” mupaka “Yesu alizaliwa wakati gani?”

(Fungua kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA))

Ukurasa wenye kichwa “Omba Funzo la Biblia Bila Kulipa” unakusaidia kufaidika na funzo la Biblia bila kulipa.

(Ufinyange kiunganisho “Omba Funzo la Biblia Bila Kulipa” kwenye ukurasa wa mwanzo)

“Niliacha kusoma Biblia kwa sababu sikuwa ninaielewa. Lakini nilipoanza kujifunza Biblia nikitumia kitabu ‘Biblia Inafundisha Kabisa Nini?’ nilishangaa kuona kwamba Biblia iko wazi na haiko ngumu kuelewa.”​—Christina.

Kila siku, watu karibu 700 000 wanafungua adresi yetu jw.org. Sababu gani wewe pia usiifungue?