Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Habari Fulani za Ulimwengu

Habari Fulani za Ulimwengu

Amerika

Uchunguzi wa Idara ya Ulimaji unaonyesha kwamba katika mwaka wa 2012, familia 14.5 juu ya 100 za Amerika, ni kusema, watu milioni 49, “hawakujua ikiwa wangepata chakula cha kutosha, wengine hata hawakuwa na uwezo wa kuuza chakula cha kutosha kwa ajili ya familia zao” kwa muda wa kipindi fulani katika mwaka huo.

Hispania

Uchunguzi uliofanywa kati ya wanafunzi wa masomo ya juu ya Hispania ulionyesha kwamba wanawake 56 juu ya 100 na wanaume 41 juu ya 100 walikubali kwamba wanakunywa pombe sana, uchunguzi huo ulionyesha kwamba wanakunywa vipimo karibu munane vinavyokubaliwa (kwa wanaume) ao vipimo sita vinavyokubaliwa (kwa wanawake) kwa wakati mumoja.

Bahari ya Pasifiki

Wanasayansi wanaotosha vitu katika sehemu za chini zaidi kufikia meta 11000 hivi katika Bonde la Mariana walivumbua kwamba bakteria na mikrobe ingine inajaa huko—hata ikiwa kuna giza nyingi sana, shinikizo kali, na baridi kali. Hapo mbele, watu walifikiri kama haingewezekana viumbe viishi katika sehemu za chini zaidi kama hizo.

Muungano Wa Falme Za Kiarabu

Katika bidii yao ili kupunguza hesabu ya watu wenye kunenepa sana, hivi karibuni, wakubwa wa serikali ya muji wa Dubai, waliahidi kutolea kila mukaaji anayepunguza kilo moja gramu moja ya zahabu, ambayo wakati huo ilikuwa na bei ya karibu dola 45. Ili kupata zahabu hiyo, iliomba mutu ajiandikishe na kisha apunguze kilo 2 ao zaidi katika mwezi wa Ramazani.