Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA WAKATI MUSIBA UNATOKEA—UNAWEZA KUFANYA NINI?

Ugonjwa wa Hatari

Ugonjwa wa Hatari

Mabel, huko Argentina, aliishi maisha yenye shuguli nyingi na alikuwa muganga wa kunyorosha viungo vya mwili. Katika mwaka wa 2007, alianza kujisikia mwenye kuchoka sana na kila siku alikuwa na maumivu makali ya kichwa. Anasema hivi: “Nilionana na madaktari wengi na nilijaribu kutumia namna zote za dawa, lakini hazikunisaidia.” Mwishowe, waganga walifanya uchunguzi wa mwili wa Mabel kupitia mashine inayochunguza sehemu za ndani za mwili; mashine hiyo ilionyesha kwamba alikuwa na kivimba kwenye ubongo. “Nilishituka sana! Sikuamini kwamba nilikuwa na adui kama huyo katika mwili wangu.”

“Hata hivyo, nilielewa kwamba huo ulikuwa ugonjwa mukali sana kisha kupata upasuaji. Wakati niliamuka katika chumba cha kutunzia watu wenye kugonjwa sana, sikuweza tena kutembea. Jambo nililoweza kufanya lilikuwa tu kutazama juu. Mbele ya kupata upasuaji, nilikuwa nikitumika sana na nilijitegemea. Kisha tu upasuaji, sikuwa na uwezo wa kufanya jambo lolote. Nilipokuwa katika chumba cha kutunzia watu wenye kugonjwa sana nilisumbuliwa na makelele ya vifaa vya kiganga, kengele za kuonyesha kwamba kuna jambo la kutenda kwa haraka, na sauti za kulia za wengine wagonjwa. Nilijisikia mwenye kuzungukwa na maumivu na mateso.

“Leo, ninajisikia muzuri kidogo. Ninaweza kutembea bila kutegemezwa na mutu mwengine, na ninaweza hata kujipeleka inje. Macho yangu yanaona kitu kimoja kuwa vitu viwili na nina matatizo ya mishipa.”

NAMNA YA KUPAMBANA NA MUSIBA

Endelea kutazamia mema. Kwenye Methali 17:22, Biblia inasema: ‘Moyo wenye shangwe ni dawa nzuri, lakini roho iliyopondeka inakausha mifupa.’ Mabel anakumbuka: “Kisha upasuaji, nilipambana na matatizo kama yale ambayo watu ambao nilikuwa nikitunza walipambana nayo. Kufanya mazoezi ya mwili kuliniletea maumivu makali, na wakati fulani nilifikiria kuacha. Nilijikaza kuondoa mawazo hayo kwa sababu nilijua kwamba mwishowe kufanya mazoezi kungenisaidia sana.”

Ili uvumilie, kaza akili juu ya tumaini ulilo nalo. Mabel anasema hivi: “Kupitia Biblia, nilijua sababu gani misiba inatokea, lakini nilijua pia kwamba siku inapopita, tunakaribia zaidi wakati ambao maumivu yatakwisha milele.” *

Kumbuka kwamba Mungu anakuhangaikia. (1 Petro 5:7) Mabel anakumbuka namna kujua kwamba Mungu anamuhangaikia kulimusaidia: “Wakati waliniingiza katika chumba cha upasuaji, nilitambua ukweli wa maneno ambayo Mungu anasema katika andiko la Isaya 41:10: ‘Usiogope, kwa maana mimi nipo pamoja nawe.’ Nilijisikia mwenye kutulia kwa sababu nilijua kama Yehova Mungu alikuwa anaona kile kinachonipata.”

Je, ulijua? Biblia inasema kwamba kutakuwa wakati ambapo watu hawatakuna tena na matatizo ya afya.—Isaya 33:24; 35:5, 6.

^ fu. 8 Ili kupata habari zingine soma sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? Kitabu hicho kinapatikana pia kwenye adresi yetu ya Internete www.pr418.com.