Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 KICHWA | Unawaza Kufanikiwa Maana Yake Nini?

Kufanikiwa ya Kweli

Kufanikiwa ya Kweli

Biblia inatutia moyo tuwe na mawazo mazuri juu ya kufanikiwa. Haiseme kama ni watu fulani tu ndio wanaweza kufanikiwa. Tena, haikubaliane na hadisi za kuwazia zinazoonyesha kama ikiwa tu ‘unataka kutimiza ndoto zako’ utafikia mambo yote unayotamani. Wazo hilo, ambalo watoto wanafundishwa tangu miaka ya chini, linaweza kumufanya mutu avunjike moyo.

Jambo la hakika ni kwamba kila mutu anaweza kufanikiwa kabisa, lakini inaomba kujikaza. Fikiria kanuni zinazofuata.

  • MAWAZO YA BIBLIA:

    ‘Anayependa feza hatatosheka na feza, wala anayependa mali hatatosheka na mapato.’—Mhubiri 5:10.

    MAANA YAKE. Kupenda sana vitu vya kimwili hakulete furaha. Lakini, kunaletea huzuni. Katika kitabu chake kimoja, Profesa Jean M. Twenge aliandika hivi: “Watu ambao hamu yao kubwa ni kupata feza wana muelekeo zaidi wa kuwa na wasiwasi na kuvunjika moyo kuliko watu walio na urafiki muzuri na wengine.” (Generation Me) Aliongeza hivi: “Uchunguzi ulionyesha waziwazi kama feza haziwezi kuuza furaha kwa sababu kisha mutu kupata uwezo wa kujitimizia mahitaji yake ya lazima, feza hazimusaidie mutu atosheke kabisa katika maisha.”

    MAMBO YA KUFANYA. Jiwekee muradi wa kufuatia jambo fulani lenye faida kubwa kuliko utajiri na vitu vya kimwili. Yesu alisema: ‘Mujilinde na kila namna ya tamaa, kwa sababu hata wakati mutu ana vitu vingi uzima wake hautokane na vitu alivyo navyo.’—Luka 12:15.

  •  MAWAZO YA BIBLIA:

    ‘Kiburi kinatangulia kuanguka, na roho ya majivuno inatangulia kujikwaa.’— Methali 16:18.

    MAANA YAKE. Kutamani kuwa tajiri haraka na kujiona kuwa wa lazima sana hakuwezi kukusaidia ufanikiwe kabisa. Kitabu kimoja kinaonyesha kama viongozi wa kompanyi ambao wamepata mafanikio kwa miaka mingi ni wenye kiasi kwa njia yenye kushangaza, hawatafute kujionyesha. (Good to Great) Lakini, sehemu 2 juu ya 3 ya kompanyi hizo ziliongozwa na watu waliokuwa wanatafuta sana faida zao, kwa hiyo kompanyi hizo zilifunga milango ao hazikuendelea muzuri.” Hilo linatufundisha nini? Ni wazi kwamba kujifikiria sana kunafanya mutu asifanikiwe.

    MAMBO YA KUFANYA. Kuliko kutafuta sifa, onyesha kiasi. Biblia inasema: “Kwa maana yeyote akifikiri kuwa yeye ni kitu wakati yeye si kitu, anaidanganya akili yake mwenyewe.” Kufikiri hivyo hakuonyeshe kama mutu amefanikiwa.— Wagalatia 6:3.

  •  MAWAZO YA BIBLIA:

    ‘Kwa mwanadamu hakuna jambo bora kuliko kwamba aone mema kwa sababu ya kazi yake ngumu.’Mhubiri 2:24.

    MAANA YAKE. Ikiwa unajizoeza kufanya kazi kwa bidii, utafurahia kazi yako sana. Profesa Madeline Levine aliandika: “Ili kuweza kufanya jambo fulani ni vizuri kujua muzuri jambo hilo na ili kujua muzuri jambo hilo inaomba zaidi sana kufanya nguvu na kuwa muvumilivu.” (Teach Your Children Well) Inaomba pia kuwa na uwezo wa kupambana na matatizo yanayoweza kutokea.

    MAMBO YA KUFANYA. Jikaze kuwa mufanyakazi muzuri, na usivunjike moyo wakati wa matatizo. Ikiwa uko na watoto, waache (kulingana na miaka na uwezo wao) watafute namna ya kumaliza matatizo yao. Usiwe haraka kumaliza matatizo yao pa nafasi yao. Wakati vijana wanaweza kupambana na matatizo, wanafurahi na hilo linawatolea mazoezi mazuri yatakayowasaidia wakati watakuwa wakubwa.

  • MAWAZO YA BIBLIA:

    ‘Imbwa aliye hai ni afazali kuliko simba aliyekufa.’— Mhubiri 9:4.

    MAANA YAKE. Ikiwa una kazi ya kimwili, unapaswa kuiona kuwa sehemu ya maisha yako, haipaswe kukamata maisha yako yote. Unaweza kujisikia mwenye kufanikiwa kabisa ikiwa kazi yako inakamata maisha yako yote lakini inaharibisha afya yako ao inafanya familia yako isikuheshimie? Watu ambao wamefanikiwa kabisa wanajikaza kuwa na usawaziko kuhusiana na kazi, afya, na familia.

    MAMBO YA KUFANYA. Hangaikia hali yako. Pumuzika vya kutosha. Kuwa mutumwa wa kazi hivi kwamba haujali tena afya, familia, na marafiki, haiko kufanikiwa ya kweli na haiwezi kukuletea faida kubwa.

  • MAWAZO YA BIBLIA:

    “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.”— Mathayo 5:3.

    MAANA YAKE. Ni lazima kujifunza na kutumia kanuni za Biblia ili kufanikiwa kabisa. Kwa mufano, mamilioni ya Mashahidi wa Yehova wametambua kama kutia mambo ya Mungu pa nafasi ya kwanza katika maisha yao kunawasaidia wasihangaike sana juu ya vitu vya kimwili.—Mathayo 6:31-33.

    MAMBO YA KUFANYA. Ona namna Biblia inaweza kukusaidia ufanikiwe kabisa. Ili kupata habari zaidi, zungumuza na Mashahidi wa Yehova wa kwenu ao fungua adresi yetu ya Internete www.pr418.com.