Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Walimaji wa Bustani Wanaoruka wa Misitu ya Mvua

Walimaji wa Bustani Wanaoruka wa Misitu ya Mvua

KILA mulimaji wa bustani anajua kama ili kupata mavuno mazuri inafaa kupanda mbegu muzuri na kwa wakati unaofaa. Lakini, unaweza kushangaa kujua kama mbegu nyingi katika misitu ya mvua zinapandwa usiku, wale wanaozipanda wanafanya hivyo wakiwa katika anga. Walimaji hao wanaopanda mbegu ni popo wanaokula matunda, wengine kati yao wanajulikana kwa jina la mbweha wanaoruka.  *

Kueneza mbegu

Popo wengi wanaokula matunda wanazungukazunguka usiku katika pori wakitafuta miti iliyo na matunda matamu ao maua yaliyo na maji matamu. Wanaporuka huku na huku ili kutafuta chakula, popo hao wanameza matunda na kuangusha mavi iliyo na ngozi na mbegu ambazo hazikusagika. Il kukamilisha kazi yao, popo wanatia kwenye maua unga wa rangi ya manjano ili yazae matunda, na wanafanya hivyo wakiwa wenye kunywa maji matamu ya maua ambayo wanapenda sana.

Popo wanaweza kueneza mbegu mupaka sehemu za mbali kwa sababu wanaweza kuenda safari murefu usiku. Pia kwa sababu popo hao wanaangusha mavi iliyo na mbegu fulani, wanatoa pia “mbolea” inayosaidia mbegu kukomaa. Haishangaze kuwa popo ndio wanatia kwenye maua ya mimea mingi unga wa rangi ya manjano ili mimea hiyo izae matunda ao wanasambaza mbegu zake.

 Kwa kuwa mimea inapatikana mahali mbalimbali, popo hao wanapaswa kuwa na uwezo wa kusafiri na kuona muzuri. Wakati wa giza, popo hao wanaweza kuona muzuri kuliko watu. Wanaweza hata kutofautisha rangi fulani. Pia, popo wanaweza kuruka muchana na vilevile usiku.

Namna Wanaishi

ULIJUA? Tofauti na popo zingine, popo wanaokula matunda hawatambue mahali chakula chao kinapatikana kupitia mawimbi ya sauti, lakini ni kupitia uwezo wao wa kuona na kunusa. Macho yao makubwa yanafaa kabisa kwa kazi yao ya usiku

Mbweha wanaoruka wa Samoa (Pteropus samoensis) wanaishi wawili-wawili muda wa maisha yote. Uchunguzi wa aina fulani za mbweha hao ulionyesha kama popo wa kike anatunza muzuri kitoto chake, anakibeba kwa majuma machache na anaendelea kukinyonyesha karibu mupaka wakati kinakuwa kikubwa. Kuhusu aina mbili za popo wanaokula matunda, popo wa kike anaweza hata kusaidiwa na popo wa kike mwengine wakati anazaa.

Lakini, popo wengi wanaokula matunda wameanza kukosekana, sababu moja ni kuharibiwa kwa makao yao. Katika Visiwa vya Pasifiki ya Kusini, kumalizika kwa popo fulani kunaweza kuleta matatizo kwa sababu inaonekana kuwa maua ya aina fulani za mimea za visiwa hivyo hayawezi kuzaa matunda bila musaada wa popo. Kwa kweli, kazi ya walimaji hao wanaoruka ni ya maana sana.

^ fu. 2 Popo wanaokula matunda wanapatikana katika Afrika, Asia, Australia, na Visiwa fulani vya Pasifiki.