Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

 MAWAZO YA BIBLIA

Usafi

Usafi

Mungu anataka tuwe na usafi wa mwili?

“Tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili na roho.” —2 Wakorintho 7:1.

MAWAZO YA BIBLIA

Muumbaji wetu anatupenda na anataka tuwe na afya nzuri na maisha marefu, na nguvu ya kufanya mambo mbalimbali. Ndio sababu Mungu anatuambia hivi: “Moyo wako upate kushika amri kwa sababu utaongezewa urefu wa siku na miaka ya uzima na amani.” (Methali 3:1, 2) Amri ambazo Mungu aliwatolea Waisraeli zilikuwa na maagizo yaliyo wazi juu ya usafi wa mwili; zilionyesha kwamba anapenda wanadamu. (Kumbukumbu la Torati 23:12-14) Wakati Waisraeli walitii sheria hizo, afya yao ilikuwa muzuri na waliepuka magonjwa yaliyopata mataifa jirani kama vile Wamisri, ambao hawakuwa na sheria za hali ya juu kama hizo.—Kumbukumbu la Torati 7:12, 15.

Leo pia, watu ‘wanaojisafisha kila unajisi [uchafu] wa mwili’, kama vile tabia mubaya ya kuvuta tumbako, ulevi, na kutumia dawa za kulewesha, wanapunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya mwili na akili, na vilevile kufa mbele ya wakati. Kwa kuwa tunaishi kila siku na watu, kutii kanuni za Mungu za usafi kunaonyesha pia kama tunajali ao tunapenda wengine.—Marko 12:30, 31.

 Mungu anataka tuwe na mwenendo safi na kuwa safi kiroho?

‘Muue viungo vya mwili wenu kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono, tamaa yenye mazara, na kutamani, ambako ni ibada ya sanamu. Kwa sababu ya mambo hayo gazabu ya Mungu inakuja.’—Wakolosai 3:5, 6.

MAWAZO YA BIBLIA

: Kama tulivyoona hapo mbele, Biblia inatushauri ‘tujisafishe kila unajisi wa mwili na roho.” Wakati Yesu alikuwa katika dunia, watu wengi, viongozi wa dini ya Wayahudi pia walijikaza sana kuwa na usafi wa mwili lakini walizarau kuwa na mwenendo safi na kuwa safi kiroho. (Marko 7:1-5) Ili kusaidia watu wawe na maoni mazuri, Yesu alisema hivi: ‘Hakuna chochote kutoka inje kinachoingia ndani ya mutu ambacho kinaweza kumutia unajisi kwa kuwa hicho kinapita na kuingia . . . ndani ya matumbo yake nacho kinatoka inje na kuingia ndani ya shimo la choo.’ Kisha aliongeza: ‘Kile ambacho kinatoka ndani ya mutu ndicho kinamutia mutu unajisi; kwa maana kutoka ndani, kutoka katika moyo wa watu, kunatoka mawazo mabaya: uasherati, wizi, mauaji, uzinzi, kutamani, matendo ya uovu, udanganyifu, mwenendo mupotovu, jicho lenye wivu, . . . ukosefu wa akili. Mambo hayo yote maovu . . . yanamutia mutu unajisi.’—Marko 7:18-23.

Kulingana na Yesu, watu wanaohangaikia sana usafi wa mwili lakini wanazarau kuwa na mwenendo muzuri na kuwa safi kiroho wanafanana na vikombe vilivyo safi inje lakini vyenye kujaa uchafu ndani.—Mathayo 23:25, 26.

Kanuni za Biblia zinapita uwezo wetu?

‘Kumupenda Mungu kunamaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake; na bado amri zake si muzigo muzito.’—1 Yohana 5:3.

MAWAZO YA BIBLIA

: Kwenye Mika 6:8, tunasoma hivi: ‘Yehova anataka nini kutoka kwako ila kutenda haki na kupenda fazili na kuwa na kiasi katika kutembea na Mungu wako?’ Mambo hayo si muzigo muzito, sivyo? Zaidi ya hilo Muumbaji wetu anataka tumutii kwa sababu tunamupenda. Tunapomutii, tunapata furaha kubwa. (Zaburi 40:8) Na wakati tunakosea, rehema ya Mungu inaweza kutufariji. “Kama vile baba anavyowaonyesha wanawe rehema, ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa. Kwa maana yeye mwenyewe analijua vema umbo letu, akikumbuka kwamba sisi ni mavumbi,” ao tuna uzaifu mbalimbali.—Zaburi 103:13, 14.

Kwa kifupi, kanuni za Mungu zinazohusu usafi wa mwili, mwenendo na usafi wa kiroho zinaonyesha kwamba Mungu ni mwema na anatupenda. Kutii kanuni hizo kunaonyesha kwamba tuna hekima na tunamupenda.