Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ujikaze kujua musaada, mahangaiko ya moyo, na kitia-moyo kutoka katika Biblia chenye ndugu na dada zako wako nacho lazima

Unaweza Kusaidia Katika Kutaniko Lako?

Unaweza Kusaidia Katika Kutaniko Lako?

MBELE ya kurudia mbinguni, Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: ‘Mutakuwa mashahidi wangu . . . mupaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.’ (Matendo 1:8) Namna gani wangeweza kuhubiri katika dunia yote?

Martin Goodman, profesa kwenye Université ya Oxford, anasema kwamba “kufanya kazi hiyo kulionyesha tofauti kati ya Wakristo na dini ya Wayahudi na vikundi vingine vyote vya dini, katika utawala wote wa Roma.” Yesu alisafiri kila mahali ili kuhubiri. Wakristo wa kweli walipaswa kuiga mufano wake kwa kuhubiri “habari njema ya ufalme wa Mungu” kila mahali. Walipaswa kutafuta watu wenye walipenda kujua kweli. (Luka 4:43) Ndiyo sababu waliitwa “mitume,” neno lenye kumaanisha wale wenye wametumwa ili kufanya jambo fulani. (Marko 3:14) Yesu alitolea wafuasi wake amri hii: ‘Kwa hiyo, muende mufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.’—Mathayo 28:18-20.

Mitume 12 wa Yesu hawako tena duniani, lakini watumishi wengi wa Yehova wanaiga mufano wao katika kazi ya kuhubiri. Wakati wanaombwa kuhubiri mahali penye kuwa lazima kubwa ya wahubiri, wanasema hivi: ‘Mimi hapa! Unitume mimi!’ (Isaya 6:8) Wamoja wamehamia katika inchi za mbali, kama vile maelfu ya wale wenye wamemaliza Masomo ya Gileadi. Wengine wamehamia katika maeneo mengine ya inchi yao. Wengi wamejifunza luga mupya ili wasaidie kutaniko ao kikundi fulani. Wakati fulani ilikuwa vigumu kufanya hivyo, lakini ndugu na dada hao wote walikuwa tayari kujitolea ili kuonyesha kwamba wanamupenda Yehova na wanapenda watu. Kwa hiyo, walifanya mipango kwa uangalifu na kutumia wakati wao, nguvu zao, na feza zao ili kusaidia kuhubiri mahali penye kuwa lazima kubwa. (Luka 14:28-30) Kazi yenye ndugu na dada hao wanafanya ni ya maana sana.

Sisi wote hatuwezi kuhamia mahali penye kuwa lazima kubwa ya wahubiri ao kujifunza luga mupya. Lakini sisi wote tunaweza kuwa wamisionere katika makutaniko yetu.

UKUWE MISIONERE KATIKA KUTANIKO LAKO

kwa kutoa musaada wenye kufaa

Wakati wa mitume, Wakristo walihubiri kwa bidii hata kama wengi kati yao hawakuhamia mahali pengine na hawakuwa wamisionere. Mutume Paulo alimuambia Timotheo hivi: “Fanya kazi ya mweneza-injili, timiza kwa ukamili huduma yako.” (2 Timotheo 4:5) Wakristo wa kwanza walitii maneno hayo, na sisi tunayatii leo. Wakristo wote wanapaswa kutii amri ya kuhubiri ujumbe wa Ufalme na kufanya wanafunzi. Na hata katika kutaniko letu, tunaweza kuwa wamisionere katika njia nyingi.

Kwa mufano, wakati wamisionere wanahamia katika inchi ingine, mambo yanabadilika kabisa, na wanapaswa kuwa tayari kujipatanisha na namna mupya ya kuishi. Hata kama hatuwezi kuhamia mahali penye kuwa lazima kubwa ya wahubiri, je, tunaweza kutafuta njia mupya za kuhubiria watu? Kwa mufano, katika mwaka wa 1940, ndugu na dada zetu walitiwa moyo kuhubiri kwanza katika barabara siku moja katika juma. Umekwisha kujaribu kuhubiri katika barabara? Umekwisha kutumia meza, vyombo vya kusukuma, na vifaa vingine vya kuwekea vichapo? Jambo la maana ni hili: Uko tayari kujaribu njia mupya za kuhubiri habari njema?

kwa kutia wengine moyo ‘wafanye kazi ya mweneza-injili’

Mutu mwenye kuwa na maoni ya muzuri anaamini kwamba watu wa eneo lake watakubali kweli na kwamba atapata matokeo mazuri kwa kutumia njia mbalimbali za kuhubiri. Mara nyingi wale wenye wanahamia mahali penye kuwa lazima kubwa ao wenye wanajifunza luga mupya ni wahubiri wenye uzoefu mwingi na wanaweza kusaidia sana kutaniko. Kwa mufano, wako wa kwanza katika kazi ya kuhubiri. Mara nyingi wamisionere wanaongoza mambo katika makutaniko mupaka wakati ndugu wa makutaniko hayo watastahili kuongoza. Ikiwa wewe ni ndugu mwenye kubatizwa, je, ‘unajitahidi [unajikaza] kufikia’ madaraka, ni kusema, uko tayari kuwa mutumishi wa huduma ao muzee ili kutumikia ndugu na dada katika kutaniko lako?—1 Timotheo 3:1.

UKUWE ‘MUSAADA WENYE KUTIA NGUVU’

Utolee wengine musaada wenye kufaa

Tunaweza pia kusaidia kutaniko letu katika njia zingine pia. Sisi wote, vijana na wazee, ndugu na dada, tunaweza kuwa ‘musaada wenye kutia nguvu’ kwa waamini wenzetu wenye kuwa na lazima ya musaada.—Wakolosai 4:11.

Tunapaswa kujua muzuri ndugu na dada zetu ili tuone namna ya kuwasaidia. Biblia inatutia moyo “tufikiriane,” ao kufikiria mambo yenye ndugu na dada zetu wako nayo lazima, wakati tunakusanyika pamoja nao. (Waebrania 10:24) Hilo halimaanishe kwamba tunapaswa kujikaza kujua mambo ao maelezo yote ya kipekee juu ya maisha ya wengine. Inamaanisha kwamba tunapaswa kujikaza kuelewa ndugu na dada zetu na kujua mambo yenye wako nayo lazima. Wanaweza kuwa na lazima ya musaada fulani, wanaweza kuwa na mahangaiko fulani katika moyo wao, ao wanaweza kuwa na lazima ya kitia-moyo kutoka katika Biblia. Ni kweli kwamba katika hali fulani ni wazee tu na watumishi wa huduma ndio wanaweza kuwasaidia. (Wagalatia 6:1) Lakini sisi wote tunaweza kusaidia familia fulani, ao ndugu na dada wenye kuzeeka wenye kupata magumu.

kwa kutia moyo wale wenye kupambana na magumu katika maisha yao

Ndugu Salvatore alisaidiwa kwa njia hiyo. Kwa sababu ya matatizo ya kupata feza, aliuzisha biashara yake, nyumba yake, na vitu vingine vingi vyenye familia yake ilikuwa navyo. Aliogopea sana familia yake. Familia moja katika kutaniko lake iliona kwamba ndugu Salvatore na familia yake walikuwa na lazima ya musaada. Walimupatia ndugu Salvatore kiasi fulani cha feza na walimusaidia yeye na bibi yake kupata kazi. Na siku fulani mangaribi walipitisha wakati pamoja ili kuwasikiliza na kuwatia moyo. Wakakuwa marafiki wa sana. Sasa familia hizo mbili zinakumbuka mambo mazuri ya wakati wenye walipitisha pamoja katika magumu.

Wakristo wa kweli hawasite kuelezea wengine mambo yenye wanaamini. Tunapaswa kumuiga Yesu na kujulisha watu wote ahadi za muzuri sana za Mungu. Iwe tuko na uwezo wa kuhamia mahali penye kuwa lazima kubwa ya wahubiri ao hapana, sisi wote tunaweza kufanya nguvu yetu yote ili kusaidia wengine katika kutaniko letu. (Wagalatia 6:10) Wakati tunatolea wengine, tunakuwa na furaha na ‘kuendelea kuzaa matunda katika kila kazi njema.’—Wakolosai 1:10; Matendo 20:35.