Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Vijana—Namna Gani Munaweza Kujitayarisha kwa Ajili ya Ubatizo?

Vijana—Namna Gani Munaweza Kujitayarisha kwa Ajili ya Ubatizo?

“Ee Mungu wangu, nimependezwa na kufanya mapenzi yako.”ZABURI 40:8.

NYIMBO: 51, 58

1, 2. (a) Eleza sababu gani kubatizwa ni uamuzi muzito. (b) Mbele ya kubatizwa, mutu anapaswa kuwa hakika na jambo gani, na sababu gani?

WEWE ni kijana mwenye anapenda kubatizwa? Ikiwa ni ndiyo, hilo ni pendeleo kubwa zaidi lenye unaweza kuwa nalo. Kama vile tuliona katika habari yenye ilitangulia, kubatizwa ni uamuzi muzito. Ubatizo unaonyesha wengine kwamba umejitoa kwa Yehova, ni kusema, umemuahidi kwamba utamutumikia milele na kwamba jambo la maana zaidi katika maisha yako ni kufanya mapenzi yake. Kwa sababu ubatizo ni ahadi nzito, unapaswa kubatizwa wakati tu umekomaa kwa kiasi fulani, wakati uamuzi wa kubatizwa umetoka katika moyo wako, na wakati unaelewa maana ya kujitoa kwa Mungu.

2 Hata hivyo, pengine unaona kwamba hauko tayari kwa ajili ya ubatizo. Ao pengine unaona kwamba uko tayari lakini wazazi wako wanaona kwamba unapaswa kungojea mupaka ukomae kwa kiasi fulani na upate uzoefu zaidi katika maisha. Unapaswa kufanya nini? Usivunjike moyo. Lakini, utumie wakati huo kufanya maendeleo yenye yatakusaidia ili kisha muda fulani uweze kutimiza mambo yenye kuombwa ili kubatizwa. Kwa hiyo, unaweza kujiwekea miradi katika njia tatu hizi: (1) mambo yenye unaamini, (2) matendo yako, na (3) shukrani yako.

MAMBO YENYE UNAAMINI

3, 4. Mufano wa Timotheo unaweza kufundisha vijana nini?

3 Fikiria namna unaweza kujibu maulizo haya: Ni nini inanihakikishia kwamba Mungu iko? Ni nini inanihakikishia kwamba Biblia inatoka kwa Mungu? Sababu gani ninatii amri za Mungu kuliko kuiga mwenendo wa watu wa ulimwengu? Maulizo hayo yanaweza kukusaidia kutii shauri hili la mutume Paulo: ‘Mujihakikishie wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.’ (Waroma 12:2) Sababu gani unapaswa kufanya hivyo?

Timotheo alikubali kweli kwa sababu alifikiri sana juu ya mambo yenye alikuwa amejifunza na kusadikishwa

4 Mufano wa Timotheo unaweza kukusaidia. Alijua muzuri Maandiko kwa sababu mama yake na tate (nkambo) yake mwanamuke walimufundisha. Hata hivyo, mutume Paulo alimuambia Timotheo hivi: ‘Uendelee katika mambo uliyojifunza na uliyoshawishiwa kuamini.’ (2 Timotheo 3:14, 15) Katika andiko hili, neno ‘kushawishiwa’ linamaanisha “kusadikishwa na kuwa hakika juu ya ukweli wa jambo fulani.” Kwa hiyo, Timotheo alipaswa kusadiki kwamba mambo yenye alijifunza katika Maandiko yalikuwa kweli. Alikubali mambo hayo, si kwa sababu tu mama yake na tate yake walimufundisha, lakini pia kwa sababu alifikiri sana juu ya mambo yenye alikuwa amejifunza na kusadikishwa.—Soma Waroma 12:1.

5, 6. Sababu gani ni jambo la maana ujifunze kutumia “nguvu za ufahamu” wakati ungali kijana?

5 Halafu wewe? Pengine umejifunza kweli tangu miaka mingi. Ikiwa ni hivyo, ujiwekee muradi wa kufikiri juu ya sababu zenye zinakuchochea uamini kweli hiyo. Kufanya hivyo kutakusaidia kutia nguvu imani yako na kuepuka kuchukua maamuzi mabaya kwa sababu ya mikazo ya vijana wenzako, mawazo ya watu wa ulimwengu, ao mawazo yako mwenyewe.

6 Ikiwa unajifunza kutumia ‘nguvu zako za ufahamu’ wakati ungali kijana, utakuwa na uwezo wa kujibu maulizo ya vijana wenzako kama vile: ‘Ni nini inakuhakikishia kwamba Mungu iko? Ikiwa Mungu anatupenda, sababu gani anaacha mambo mabaya yatokee? Sababu gani ninaamini kwamba Mungu ni wa milele?’ Ikiwa unazoea kujifunza Biblia kwa ukawaida, maulizo kama hayo hayatakufanya ukuwe na mashaka, lakini yatakusaidia kutia nguvu imani yako.

7-9. Eleza namna gani misaada ya kujifunza yenye kichwa “Biblia Inafundisha Kabisa Nini?” yenye kupatikana kwenye adresi yetu Internete, inaweza kukusaidia kutia nguvu imani yako.

7 Kujifunza kipekee kwa uangalifu kunaweza kukusaidia kujibia maulizo, umalize mashaka yote, na kutia nguvu imani yako. (Matendo 17:11) Tuko na vichapo vingi vyenye vinaweza kukusaidia kufanya hivyo. Vijana wengi wamepata faida nyingi kwa kujifunza broshua Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai na kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Pia, vijana wengi wamepata faida na kufurahia habari zenye kichwa “Biblia Inafundisha Kabisa Nini?” zenye kupatikana kwenye adresi yetu ya Internete jw.org. Unaweza kupata habari hizo chini ya kichwa MAFUNDISHO YA BIBLIA > MATINEJA. Kila musaada wa kujifunza katika habari hizo umetayarishwa ili kukusaidia kutia nguvu imani yako juu ya habari fulani ya Biblia.

8 Kwa sababu uko mwanafunzi wa Biblia, pengine tayari unajua majibu ya maulizo fulani kati ya maulizo yenye kupatikana katika misaada ya kujifunza. Lakini, uko hakika na majibu yako? Misaada ya kujifunza itakusaidia ufikiri kwa uangalifu juu ya maandiko mbalimbali na itakuchochea uandike sababu zenye zinakufanya uamini mambo hayo. Hilo litakusaidia kujua namna ya kuwaelezea wengine mambo yenye unaamini. Ikiwa uko na uwezo wa kupata habari zenye kichwa “Biblia Inafundisha Kabisa Nini?” kwenye adresi yetu ya Internete, unaweza kutumia habari hizo katika funzo lako la pekee ili zikusaidie kutia nguvu imani yako.

9 Unaweza kujihakikishia mwenyewe kwamba hiyo ndiyo kweli. Jambo hilo litakusaidia ujitayarishe kwa ajili ya ubatizo. Dada moja kijana alisema hivi: “Mbele nichukue uamuzi wa kubatizwa, nilijifunza Biblia na nikaona kuwa hii ndiyo dini ya kweli. Na kila siku imani yangu inaendelea kuwa nguvu.”

MATENDO YAKO

10. Sababu gani ni jambo lenye kufaa Mukristo mwenye kubatizwa akuwe na matendo yenye kupatana na imani yake?

10 Biblia inasema hivi: “Imani, ikiwa haina matendo, imekufa yenyewe.” (Yakobo 2:17) Ikiwa uko na imani yenye nguvu, hilo litaonekana kupitia matendo yako. Utakuwa na mambo yenye Biblia inaita “matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ujitoaji-kimungu [kushikamana na Mungu].”—Soma 2 Petro 3:11.

11. Eleza maana ya maneno “matendo matakatifu ya mwenendo.”

11 “Matendo matakatifu ya mwenendo” ni nini? Ikiwa matendo yako ni matakatifu, utakuwa na mwenendo safi. Kwa mufano, ufikirie miezi sita yenye imepita. Wakati ulijaribiwa kufanya jambo fulani la mubaya, je, mbele ya kufanya uamuzi, ulifikiri kwa uangalifu juu ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa? (Waebrania 5:14) Unakumbuka wakati fulani wa pekee wenye haukujiachilia uangukie katika jaribu ao katika mikazo ya vijana wenzako? Kwenye masomo, uko mufano muzuri kwa wanafunzi wenzako? Unabakia muaminifu kwa Yehova, ao unajaribu kujifanya kama wanafunzi wenzako ili wasikuchekelee? (1 Petro 4:3, 4) Kwa kweli, sisi wote hatuko wakamilifu. Hata wale wenye wamemutumikia Yehova kwa miaka mingi wanaweza kusikia haya wakati fulani na kuona kuwa ni vigumu kuhubiria wengine. Lakini, mutu mwenye amejitoa kwa Mungu atajivunia kuwa Shahidi wa Yehova, na anaonyesha hilo kupitia mwenendo wake muzuri.

12. Taja ‘vitendo fulani vya ujitoaji-kimungu,’ na unapaswa kuviona namna gani?

12 “Vitendo vya ujitoaji-kimungu” ni nini? Ni mambo yenye unafanyaka katika kutaniko, kama vile, kuenda kwenye mikutano na kuhubiri. Lakini kuko pia mambo mengine yenye watu wengine hawaone, kama vile, kusali kwa Yehova na kufanya funzo la pekee. Mutu mwenye amejitoa kwa Yehova hataona kuwa mambo hayo ni muzigo muzito. Atajisikia kama vile Mufalme Daudi. Alisema hivi: ‘Nimependezwa na kufanya mapenzi yako, na sheria yako iko ndani yangu.’—Zaburi 40:8.

Unataja mambo waziwazi katika sala zako, na zinafunua nini juu ya upendo wako kwa Yehova?

13, 14. Ni chombo gani kinaweza kukusaidia ufanye “vitendo vya ujitoaji-kimungu,” na vijana fulani wamepata faida gani kwa kutumia chombo hicho?

13 Ili kukusaidia ujiwekee miradi, tuko na karatasi ya mazoezi kwenye ukurasa wa 308 na 309 wa kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2. Kwenye karatasi hiyo, unaweza kuandika majibu yako juu ya maulizo kama haya: “Unataja mambo waziwazi katika sala zako, na zinafunua nini juu ya upendo wako kwa Yehova?” “Unajifunza habari gani wakati wa funzo lako la pekee?” “Unaenda katika mahubiri hata kama wazazi wako hawaende?” Karatasi hiyo iko pia na nafasi kwenye unaweza kuandika kila muradi wenye unajiwekea juu ya sala, funzo lako la pekee, na kazi ya kuhubiri.

14 Vijana wengi wenye wanapenda kubatizwa wameona kuwa karatasi hiyo ni chombo kizuri. Dada kijana mwenye anaitwa Tilda alisema hivi: “Nilitumikisha karatasi hiyo ili kujiwekea miradi. Nilifikia miradi hiyo polepole, na kisha mwaka moja hivi nilikuwa tayari kwa ajili ya ubatizo.” Ndugu kijana mwenye anaitwa Patrick alipata pia matokeo kama hayo. Alisema hivi: “Nilijua muzuri miradi yangu, lakini kuandika miradi hiyo kulinisaidia nitumike sana ili niifikie.”

Utaendelea kumutumikia Yehova hata kama wazazi wako wanaacha kumutumikia? (Picha hii inapatana na fungu la 15)

15. Eleza sababu gani uamuzi wa kujitoa kwa Mungu unapaswa kutoka katika moyo wa mutu.

15 Ulizo moja kati ya maulizo yenye kuwa kwenye karatasi hiyo ni hili: “Utaendelea kumutumikia Yehova hata kama wazazi na marafiki wako wanaacha kumutumikia?” Wakati unajitoa kwa Yehova na kubatizwa, unakuwa na urafiki wa pekee pamoja naye. Kwa hiyo, wazazi wako ao mutu mwengine yeyote hawapaswe kukukaza kumutumikia Yehova. Matendo yako matakatifu ya mwenendo na matendo yako ya kushikamana na Mungu yataonyesha kama uko hakika kwamba uko katika dini ya kweli na unapenda kutii kanuni za Mungu, na kwamba unajitayarisha kwa ajili ya ubatizo.

SHUKRANI YAKO

16, 17. (a) Ni nini inapaswa kumuchochea mutu akuwe Mukristo? (b) Kuwa na shukrani kwa ajili ya zabihu ya ukombozi kunaweza kufananishwa na hali gani?

16 Siku moja, mutu fulani mwenye kujua sana Sheria ya Musa alimuuliza Yesu hivi: ‘Amri iliyo kubwa ni gani?’ Yesu alimujibia hivi: ‘Lazima umupende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.’ (Mathayo 22:35-37) Yesu alieleza kwamba jambo lenye linapaswa kumuchochea mutu fulani abatizwe na kuwa Mukristo ni kumupenda Yehova. Njia moja kati ya njia za muzuri zaidi za kukusaidia kutia nguvu upendo wako kwa Yehova ni kufikiri sana juu ya zabihu ya ukombozi, ni kusema, zawadi kubwa yenye Mungu alitolea wanadamu. (Soma 2 Wakorintho 5:14, 15; 1 Yohana 4:9, 19.) Ukifanya hivyo, utakuwa tayari kuonyesha shukrani yako juu ya zawadi hiyo ya muzuri zaidi.

17 Shukrani yako juu ya zabihu ya ukombozi inaweza kuelezwa katika njia hii: Wazia kwamba uko karibu kuzama katika maji, kisha mutu fulani anakuokoa. Utarudia nyumbani, unakausha nguo zako, na kusahau jambo lenye mutu huyo alikufanyia? Hapana! Utaendelea kumuonyesha shukrani mutu huyo mwenye aliokoa uzima wako! Vilevile, tunapaswa kuwa wenye shukrani sana kwa Yehova na Yesu kwa ajili ya zabihu ya ukombozi. Wao ndio waliokoa uzima wetu! Wametukomboa kutoka katika zambi na kifo. Kwa sababu wanatupenda, sasa tuko na tumaini la kuishi milele katika dunia Paradiso!

18, 19. (a) Sababu gani haupaswe kuogopa kujitoa kwa Yehova? (b) Namna gani kumutumikia Yehova kunafanya maisha yako yakuwe mazuri zaidi?

18 Uko mwenye shukrani kwa ajili ya mambo yenye Yehova amekufanyia? Ikiwa ni ndiyo, jambo la maana lenye unaweza kufanya ni kujitoa kwa Yehova na kubatizwa. Kujitoa kwa Mungu ni kumuahidi kwamba utafanya mapenzi yake milele. Unapaswa kuogopa kufanya ahadi hiyo? Hapana! Yehova anapenda ukuwe na maisha ya muzuri zaidi, na atawabariki wale wenye kufanya mapenzi yake. (Waebrania 11:6) Hautumie maisha yako mubaya wakati unabatizwa, lakini hilo linafanya maisha yako yakuwe ya muzuri zaidi! Ndugu moja mwenye kuwa na miaka 24, alibatizwa wakati angali mutoto. Anasema hivi: “Ningeelewa muzuri zaidi mafundisho ya Biblia ikiwa ningengojea nikomae kwa kiasi fulani, lakini uamuzi wa kujitoa kwa Yehova ulinisaidia niepuke kufuatilia miradi ya ulimwengu.”

Shetani anajipenda mwenyewe na hakuhangaikie

19 Yehova anapenda ukuwe na maisha ya muzuri zaidi. Lakini, Shetani anajipenda mwenyewe na hakuhangaikie. Ukimufuata, hawezi kukupatia kitu fulani kizuri. Namna gani anaweza kukupatia kitu chenye hana? Hana habari njema, na hana tumaini lolote. Anaweza tu kukuongoza kwenye uharibifu, kwa sababu ataharibiwa hivi karibuni!—Ufunuo 20:10.

20. Ni nini inaweza kumusaidia kijana afanye maendeleo mupaka afikie kujitoa kwa Yehova na kubatizwa? (Soma pia kisanduku “Mambo Yenye Yatakusaidia Kufanya Maendeleo.”)

20 Uamuzi muzuri zaidi wenye unaweza kuchukua ni kutoa maisha yako kwa Yehova. Uko tayari kufanya hivyo? Ikiwa ni ndiyo, usiogope kufanya ahadi hiyo. Lakini ikiwa unaona kwamba hauko tayari, utumikishe mashauri yenye kupatikana katika habari hii ili uendelee kufanya maendeleo. Mutume Paulo alishauria Wakristo katika muji wa Filipi waendelee kufanya maendeleo. (Wafilipi 3:16) Ikiwa unatii mashauri hayo, kisha muda fulani utakuwa tayari kutoa maisha yako kwa Yehova na kubatizwa.