Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Vijana—Muko Tayari kwa Ajili ya Ubatizo?

Vijana—Muko Tayari kwa Ajili ya Ubatizo?

‘Ni nani kati yenu anayetaka kujenga munara ambaye hakae kwanza na kuhesabu garama, ili aone kama ana kiasi cha kutosha kuukamilisha?’LUKA 14:28.

NYIMBO: 120, 64

Habari hii na ile yenye kufuata zilitayarishwa kwa ajili ya vijana wenye wanapenda kubatizwa

1, 2. (a) Ni nini inaletea watu wa Mungu furaha leo? (b) Namna gani wazazi Wakristo na wazee wanaweza kusaidia vijana waelewe maana ya kubatizwa?

“MUZEE moja wa kutaniko alimuambia hivi kijana Christopher, mwenye kuwa na miaka 12: “Nimekujua tangu wakati ulizaliwa, na ninafurahi kusikia kwamba unapenda kubatizwa. Ninapenda kukuuliza hivi: ‘Sababu gani unapenda kubatizwa?’” Muzee huyo alikuwa na sababu nzuri za kuuliza ulizo hilo. Tunafurahi sana kuona vijana wengi wanabatizwa kila mwaka. (Mhubiri 12:1) Lakini wazazi Wakristo na wazee wa kutaniko wanahakikisha kwamba vijana wamechukua uamuzi huo wao wenyewe na kwamba wameelewa maana ya kubatizwa.

2 Biblia inatufundisha kwamba wakati mutu anajitoa kwa Mungu na kubatizwa, anakuwa Mukristo na anaanza kuishi maisha ya mupya. Maisha hayo yanaleta baraka nyingi kutoka kwa Yehova, na mateso kutoka kwa Shetani. (Methali 10:22; 1 Petro 5:8) Ndiyo sababu wazazi Wakristo wanapaswa kutumia wakati wa kutosha ili kufundisha watoto wao inamaanisha nini kabisa kuwa mufuasi wa Kristo. Ikiwa vijana fulani hawana wazazi wenye kuwa Mashahidi, wazee katika kutaniko watawasaidia kwa upendo waelewe maana ya kujitoa kwa Mungu na kubatizwa. (Soma Luka 14:27-30.) Inaomba kujitayarisha ili kumaliza kazi ya kujenga nyumba; vilevile vijana wanapaswa kujitayarisha mbele ya kubatizwa ili wamutumikie Yehova kwa uaminifu ‘mupaka mwisho.’ (Mathayo 24:13) Ni nini itasaidia vijana waamue kumutumikia Yehova milele? Acha tuone.

3. (a) Namna gani maneno ya Yesu na ya Petro yanatusaidia kuelewa kwamba ubatizo ni wa maana? (Mathayo 28:19, 20; 1 Petro 3:21) (b) Tutajibia maulizo gani, na sababu gani?

3 Wewe ni kijana mwenye anapenda kubatizwa? Ikiwa ni ndiyo, huo ni muradi muzuri zaidi! Ni pendeleo kubwa kubatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova. Pia, ni jambo lenye Mukristo anapaswa kufanya, na ni hatua ya maana sana kwa wale wenye wataokolewa wakati wa mateso makubwa. (Mathayo 28:19, 20; 1 Petro 3:21) Wakati unabatizwa, unaonyesha kwamba unamuahidi Yehova kwamba utamutumikia milele. Unapenda kabisa kutimiza ahadi hiyo; kwa hiyo, maulizo haya yatakusaidia uone ikiwa uko tayari kwa ajili ya ubatizo: (1) Nimekomaa kwa kiasi fulani ili kuchukua uamuzi huo? (2) Uamuzi huo unatoka kabisa katika moyo wangu? (3) Ninaelewa kabisa maana ya kujitoa kwa Yehova? Tujibie basi maulizo hayo.

WAKATI UMEKOMAA KWA KIASI FULANI

4, 5. (a) Sababu gani haiko watu wenye wamekomaa tu ndio wanapaswa kubatizwa? (b) Kukomaa kunamaanisha nini kwa Mukristo?

4 Biblia haiseme kwamba ni watu wenye wamekomaa tu ao wale wenye wamefikia miaka fulani ndio wanaweza kubatizwa. Andiko la Methali 20:11 linasema kwamba kwa matendo yake, mutoto anajitambulisha kama matendo yake ni safi na mazuri. Kwa hiyo, hata mutoto anaweza kuelewa inamaanisha nini kufanya mambo yenye kuwa sawa na kujitoa kwa Muumbaji wake. Kwa hiyo, kubatizwa ni hatua ya maana na yenye kufaa kwa kijana mwenye ameonyesha kwamba amekomaa na kwamba amejitoa kwa Yehova.—Methali 20:7.

5 Kukomaa kunamaanisha nini? Hakumaanishe kila mara miaka ya mutu ao kukomaa kwa mwili. Biblia inasema kwamba watu wenye kukomaa wamezoeza “nguvu zao za ufahamu” ili kujua tofauti kati ya mambo yenye kuwa sawa na yenye kuwa makosa. (Waebrania 5:14) Mutu mwenye kukomaa anajua mambo yenye kuwa sawa na anaamua katika moyo wake kufanya mambo hayo. Kwa hiyo, ni vigumu wengine wamuchochee kufanya makosa. Na, hana lazima kila mara mutu mwengine amuambie mambo yenye kuwa sawa yenye anapaswa kufanya. Ndiyo sababu kijana mwenye anapenda kubatizwa anapaswa kuwa na uwezo wa kufanya mambo yenye kuwa sawa hata kama wazazi wake ao watu wengine wenye kukomaa hawako pembeni yake.—Linganisha na Wafilipi 2:12.

6, 7. (a) Eleza magumu yenye Danieli alipata wakati alikuwa katika Babiloni. (b) Namna gani Danieli alionyesha kwamba alikuwa mwenye kukomaa?

6 Je, kijana anaweza kabisa kufikia ukomavu huo? Tuzungumuzie mufano wa Danieli. Pengine alikuwa na miaka kati ya 13 na 19, wakati alipelekwa huko Babiloni mbali na wazazi wake. Bila kutazamia, Danieli alianza kuishi pamoja na watu wenye hawakuwa wanatii amri za Mungu. Tuzungumuzie basi kwa uangalifu mufano wa Danieli. Alitendewa kwa njia ya pekee huko Babiloni. Alikuwa kati ya vijana fulani wenye walichaguliwa kwa uangalifu ili wamutumikie mufalme. (Danieli 1:3-5, 13) Inaonekana kuwa Danieli alikuwa na cheo chenye hangeweza kupata katika Israeli.

7 Kijana Danieli alitenda namna gani? Aliruhusu watu wa Babiloni wamugeuze ao waregeze imani yake? Hapana kabisa! Biblia inasema kwamba wakati alikuwa katika Babiloni, aliamua “moyoni mwake kwamba hatajitia unajisi [uchafu],” ni kusema, hatajiingiza katika mambo ya ibada ya uongo. (Danieli 1:8) Hilo lilionyesha kabisa kwamba yeye ni mwenye kukomaa!

Kijana mwenye kukomaa hajionyeshe kuwa rafiki ya Mungu kwenye Jumba la Ufalme, lakini rafiki ya ulimwengu kwenye masomo

(Picha hizi zinapatana na fungu la 8)

8. Mufano wa Danieli unaweza kukufundisha nini?

8 Mufano wa Danieli unaweza kukufundisha nini? Hata wakati wa magumu, kijana mwenye kukomaa hataregeza imani yake. Hatakuwa kama kigeugeu (Caméleon) mwenye anabadilisha rangi yake ili afanane na vitu vyenye kuwa pembeni yake. Hajionyeshe kuwa rafiki ya Mungu kwenye Jumba la Ufalme, lakini rafiki ya ulimwengu kwenye masomo. Lakini, atabakia muaminifu hata wakati anajaribiwa.—Soma Waefeso 4:14, 15.

Hata wakati wa magumu, kijana mwenye kukomaa hataregeza imani yake

9, 10. (a) Kijana anaweza kupata faida gani wakati anafikiria namna alitenda wakati imani yake ilijaribiwa katika siku zenye zimepita? (b) Kubatizwa kunamaanisha nini?

9 Ni kweli kwamba sisi wote hatuko wakamilifu. Vijana na watu wenye kukomaa wanafanya makosa wakati fulani. (Mhubiri 7:20) Lakini ikiwa unapenda kubatizwa, ni jambo la hekima ujichunguze ili kujua ikiwa umeamua kabisa kutii amri za Yehova. Ujiulize hivi: ‘Nimemutii Yehova kwa muda fulani?’ Ufikirie namna ulitenda wakati imani yako ilijaribiwa katika siku zenye zimepita. Uliweza kuamua mambo yenye kuwa sawa yenye ulipaswa kufanya? Kama vile Danieli, kuna mutu fulani mwenye amekuchochea utumie uwezo wako mbalimbali katika ulimwengu huu wa Shetani? Ikiwa unapata jaribu kama hilo, unaweza kutambua kabisa mambo yenye Yehova anapenda ufanye?—Waefeso 5:17.

10 Sababu gani ni jambo la lazima utafute majibu ya maulizo hayo? Kwa sababu yatakusaidia uelewe kwamba ubatizo ni uamuzi muzito kabisa. Kubatizwa kunaonyesha wengine kwamba umetoa ahadi ya maana sana kwa Yehova. Umemuahidi kumupenda na kumutumikia milele kwa moyo wako wote. (Marko 12:30) Kila mutu mwenye amebatizwa anapaswa kujikaza kutimiza ahadi yake kwa Yehova.—Soma Mhubiri 5:4, 5.

UMEAMUA WEWE MWENYEWE?

11, 12. (a) Mutu mwenye anafikiria kubatizwa anapaswa kuhakikisha jambo gani? (b) Ni nini itakusaidia ukuwe na maoni ya muzuri juu ya mupango wa Yehova wa ubatizo?

11 Biblia inasema kwamba watumishi wote wa Yehova, vijana na wazee, watamutumikia “kwa hiari [kwa kujipendea].” (Zaburi 110:3) Kwa hiyo, mutu mwenye anapenda kubatizwa anapaswa kuwa hakika kwamba amechukua uamuzi huo yeye mwenyewe. Kwa hiyo, unapaswa kuchunguza uamuzi wako kwa uangalifu, zaidi sana ikiwa ulikomalia katika kweli.

12 Pengine wakati unaendelea kukomaa, unaona namna watu wengi wanabatizwa. Watu hao wanaweza kuwa marafiki ao watu wa familia yako. Lakini, unapaswa kuwa muangalifu ili usianze kufikiri kwamba unapaswa kubatizwa kwa sababu tu umefikia miaka fulani ao kwa sababu watu wengi wanabatizwa. Namna gani unaweza kuhakikisha kwamba uko na maoni ya Yehova juu ya ubatizo? Uchukue wakati wa kufikiria sababu gani ubatizo ni wa maana sana. Utapata sababu nyingi za muzuri katika habari hii na ile yenye kufuata.

13. Namna gani unaweza kuonyesha ikiwa uamuzi wako wa kubatizwa umetoka katika moyo wako?

13 Njia moja ya kuonyesha ikiwa uamuzi wa kubatizwa umetoka katika moyo wako ni kuchunguza sala zako. Unasali kwa Yehova kwa ukawaida? Unamuambia Yehova mambo waziwazi katika sala zako? Majibu ya maulizo hayo yataonyesha ikiwa uko na urafiki wa sana pamoja na Yehova ao hapana. (Zaburi 25:4) Mara nyingi, Yehova anajibia sala zetu kupitia Biblia. Njia ingine ya kuonyesha ikiwa unapenda kabisa kumukaribia Yehova na kumutumikia kwa moyo wako wote, ni kuchunguza programe yako ya kujifunza. (Yoshua 1:8) Ujiulize hivi: ‘Ninafanya funzo la pekee kwa ukawaida? Ninategemeza ibada yetu ya familia kwa moyo wangu wote?’ Majibu ya maulizo hayo yatakusaidia ujue ikiwa uamuzi wa kubatizwa umetoka katika moyo wako.

MAANA YA KUJITOA KWA MUNGU

14. Eleza tofauti kati ya kujitoa kwa Mungu na kubatizwa.

14 Vijana fulani wanaweza kushindwa kuelewa muzuri tofauti kati ya kujitoa kwa Mungu na kubatizwa. Wamoja wanaweza kusema kwamba wamekwisha kutoa maisha yao kwa Yehova lakini hawako tayari kwa ajili ya ubatizo. Lakini, hilo linawezekana kabisa? Kujitoa kwa Yehova ni kumuambia katika sala kwamba unatoa ahadi ya kumutumikia milele. Wakati unabatizwa, unaonyesha wengine kwamba umekwisha kujitoa kwa Yehova. Kwa hiyo, unapaswa kwanza kuelewa maana ya kujitoa kwa Mungu mbele ubatizwe.

15. Kujitoa kwa Mungu kunamaanisha nini?

15 Wakati unatoa maisha yako kwa Yehova, unamuambia kwamba umekuwa wake. Unamuahidi kwamba jambo lenye litakuwa la maana zaidi katika maisha yako, ni kumutumikia. (Soma Mathayo 16:24.) Ahadi hiyo yenye unatoa kwa Mungu ni ahadi nzito! (Mathayo 5:33) Kwa hiyo, namna gani unaonyesha kwamba hauishi tena kwa ajili yako mwenyewe lakini unaishi kwa ajili ya Yehova?—Waroma 14:8.

16, 17. (a) Kujitoa wenyewe kunamaanisha nini? Eleza. (b) Kwa kweli, mutu mwenye anajitoa kwa Mungu anamuambia nini kabisa?

16 Tuzungumuzie basi mufano moja. Wazia kwamba rafiki yako anakupatia motokari. Anakupatia vikaratasi vya motokari (documents) kisha anakuambia hivi: “Hii ni motokari yako.” Lakini anasema hivi: “Nitabakia na funguo za motokari. Wewe hautakuwa unatembeza; mimi mwenyewe nitakuwa ninatembeza.” Utaona zawadi hiyo namna gani? Utamuona namna gani rafiki huyo mwenye alikupatia motokari?

17 Wakati mutu anajitoa kwa Yehova, anamuambia hivi: “Ninakupatia maisha yangu. Mimi ni wako.” Yehova iko na haki ya kuomba mutu huyo atimize ahadi yake. Lakini, Yehova atamuona namna gani ikiwa anaanza kushindwa kumutii kwa kuchumbiana kwa njia ya siri na mutu fulani mwenye haiko Shahidi? Ao ikiwa anakubali kazi yenye itamufanya ashindwe kuhubiri ao kukusanyika kwa ukawaida? Kwa kufanya hivyo, mutu huyo atakuwa hatimize ahadi yake kwa Yehova. Itakuwa kama vile anabakia na funguo za motokari. Wakati tunatoa maisha yetu kwa Yehova, tunamuambia hivi: “Nimekupatia maisha yangu, haiko yangu tena.” Kwa hiyo, kuliko kufanya mapenzi yetu wenyewe, tutafanya mapenzi ya Yehova sikuzote. Tumuige basi mufano wa Yesu. Alisema hivi: “Nimeshuka kutoka mbinguni kufanya, si mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.”—Yohana 6:38.

Kubatizwa ni uamuzi muzito na ni pendeleo kubwa

18, 19. (a) Maneno ya dada Rose na ndugu Christopher yanaonyesha namna gani kwamba kubatizwa ni pendeleo lenye kuleta baraka nyingi? (b) Unaona namna gani pendeleo la kubatizwa?

18 Ni wazi kwamba ubatizo ni uamuzi muzito kabisa. Ni pendeleo kubwa kujitoa kwa Yehova na kubatizwa. Vijana wenye wanamupenda Yehova na wenye wameelewa maana ya kujitoa kwake, hawasite-site kutoa maisha yao kwake na kubatizwa. Hawaone kwamba walichukua uamuzi mubaya. Rose, dada kijana mwenye kubatizwa anasema hivi: “Ninamupenda Yehova, na hakuna jambo lingine lenye linaweza kuniletea furaha zaidi kuliko kumutumikia. Katika maisha yangu yote, hakuna uamuzi wenye nimechukua kwa uhakika wote kabisa kuliko uamuzi wa kubatizwa.”

19 Tuseme nini juu ya Christopher, mwenye tulitaja kwenye mwanzo wa habari hii? Anaona namna gani uamuzi wake wa kubatizwa wenye alichukua wakati alikuwa na miaka 12? Anasema kwamba anafurahi sana kwa sababu alichukua uamuzi huo. Alianza kufanya kazi ya upainia wa kawaida wakati alikuwa na miaka 17 na alikuwa mutumishi wa huduma wakati alikuwa na miaka 18. Leo anatumikia kwenye Beteli. Anasema hivi: “Nilifanya muzuri kuchukua uamuzi wa kubatizwa. Katika maisha yangu, nimemutumikia Yehova na tengenezo lake kwa furaha.” Ikiwa unapenda kubatizwa, namna gani unaweza kujitayarisha? Tutajibia ulizo hilo katika habari yenye kufuata.