Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Yehova Anaongoza Watu Wake Katika Njia ya Uzima

Yehova Anaongoza Watu Wake Katika Njia ya Uzima

‘Hii ndiyo njia. Mutembee ndani yake.’ISAYA 30:21.

NYIMBO: 65, 48

1, 2. (a) Ni onyo gani lenye limeokoa uzima wa watu wengi? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Watu wa Mungu wako na muongozo gani wenye unaweza kuokoa uzima wao?

“SIMAMA, TAZAMA, SIKILIZA.” Maneno hayo yalionekana kwenye pankarte kubwa zenye zilipatikana nafasi barabara zinakutana na njia za treni katika Amerika ya Kaskazini. Maneno hayo yalitumiwa zaidi ya miaka 100. Sababu gani? Kwa sababu treni zenye kukimbia sana zingegonga motokari zenye kuvuka njia hizo. Watu wengi waliokoa uzima wao kwa sababu ya kutii maneno hayo ya kuonya.

2 Yehova hatuandikie kwenye pankarte maneno ya kutuonya; lakini anatufanyia jambo fulani la maana zaidi. Anaongoza watu wake ili waepuke hatari na wapate uzima wa milele. Yehova ni kama muchungaji mwenye upendo mwenye anaongoza na kuonya kondoo zake ili wasipite katika njia zenye kuwa na hatari.—Soma Isaya 30:20, 21.

YEHOVA AMEONGOZA WATU WAKE TANGU ZAMANI

3. Namna gani wanadamu wote waliingia katika njia yenye kuongoza kwenye kifo?

3 Tangu wakati aliumba mwanadamu, Yehova amewapatia maagizo ao miongozo yenye kuwa wazi. Kwa mufano, katika shamba la Edeni, Yehova alitoa maagizo yenye kuwa wazi yenye ingeongoza wanadamu kwenye uzima wa milele na kuwaletea furaha. (Mwanzo 2:15-17) Lakini Adamu na Eva hawakufuata muongozo wa Baba yao mwenye upendo. Eva alisikiliza mashauri yenye Shetani alimutolea kupitia nyoka, na kisha Adamu alimusikiliza Eva, bibi yake. Ni nini iliwapata? Wote wawili walipata mateso, na walikufa bila kuwa na tumaini lolote. Pia, kwa sababu walishindwa kutii, waliongoza wanadamu wote katika njia yenye kuongoza kwenye kifo.

4. (a) Sababu gani wanadamu walikuwa na lazima ya maagizo mengine kisha Garika? (b) Namna gani hali mupya ya wanadamu ilionyesha mawazo ya Mungu?

4 Mungu alimupatia Noa maagizo yenye iliokoa uzima. Kisha Garika, Yehova aliwapatia wanadamu amri yenye kuwakataza kula ao kunywa damu. Sababu gani? Kwa sababu Yehova alikuwa tayari kuwaruhusu waanze kula nyama. Hali hiyo mupya ilifanya wakuwe na lazima ya maagizo haya mapya: ‘Isipokuwa tu nyama pamoja na nafsi [uzima] yake—damu yake—musikule.’ (Mwanzo 9:1-4) Amri hiyo inatusaidia kujua mawazo ya Mungu juu ya uzima, kwa sababu ulitoka kwake. Yeye ni Muumbaji na anatupatia uzima; kwa hiyo, iko na haki ya kutupatia maagizo juu ya uzima. Kwa mufano, alitolea wanadamu amri yenye kuwakataza kuuana. Mungu anaona uzima na damu kuwa vitakatifu; kwa hiyo, atawapatia malipizi watu wenye kutumia mubaya mambo hayo.—Mwanzo 9:5, 6.

5. Tutazungumuzia nini, na sababu gani?

5 Kisha wakati wa Noa, Mungu hakuacha kuongoza watu wake. Katika habari hii, tutazungumuzia mifano fulani yenye kuonyesha namna aliwaongoza. Kuzungumuzia tena mifano hiyo kutatusaidia tuamue kufuata kabisa maagizo yenye Yehova atatupatia katika dunia mupya.

TAIFA MUPYA LINAPEWA MUONGOZO MUPYA

6. Sababu gani watu wa Mungu walipaswa kutii sheria zenye aliwapatia kupitia Musa, na Waisraeli walipaswa kuziona namna gani?

6 Wakati wa Musa, Yehova alipatia watu wake muongozo wenye kuonyesha namna walipaswa kujiendesha na namna ya kumuabudu. Sababu gani? Kwa sababu hali ya watu wake ilikuwa imebadilika tena. Waisraeli walikuwa watumwa katika inchi ya Misri kwa muda wa miaka zaidi ya 200. Waliishi kati ya watu wenye waliabudu wafu, wenye kutumia sanamu, na wenye kufanya mambo mengine mengi yenye kumukosea Mungu heshima. Wakati watu wa Mungu walikombolewa kutoka Misri, walikuwa na lazima ya maagizo mapya. Walipaswa kuwa taifa lenye kufuata Sheria ya Yehova tu. Vitabu fulani vinasema kwamba neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “sheria” linapatana na neno lenye kumaanisha “muongozo, kiongozi, ao mwalimu.” Sheria iliwalinda Waisraeli ili wasikuwe na mwenendo muchafu na waepuke dini ya uongo ya mataifa yenye yaliwazunguka. Wakati Waisraeli walitii Sheria hiyo, Mungu aliwabariki. Wakati walishindwa kutii, walipatwa na mambo mabaya sana.—Soma Kumbukumbu la Torati 28:1, 2, 15.

7. (a) Eleza sababu gani Yehova aliwapatia watu wake muongozo. (b) Namna gani Sheria ilikuwa mutunzaji wa Waisraeli?

7 Kulikuwa sababu ingine yenye ilifanya Waisraeli wapewe muongozo mupya. Sheria iliwatayarisha kwa ajili ya tukio la maana sana katika mupango wa Yehova, ni kusema, kufika kwa Masiya, Yesu Kristo. Sheria iliwakumbusha Waisraeli kwamba walikuwa watenda-zambi. Iliwasaidia pia waelewe kwamba walikuwa na lazima ya zabihu ya ukombozi, ni kusema, zabihu yenye kukamilika yenye ingeondoa kabisa zambi zao. (Wagalatia 3:19; Waebrania 10:1-10) Tena, Sheria ililinda kizazi cha Masiya na kusaidia Waisraeli wamutambue wakati angetokea. Kwa kweli, Sheria ilikuwa kiongozi wa muda, ao ‘mutunzaji,’ mwenye kuongoza kwa Kristo.—Wagalatia 3:23, 24.

8. Sababu gani tunapaswa kuongozwa na kanuni za Sheria ya Musa?

8 Muongozo wenye Yehova aliwapatia Waisraeli katika Sheria unaweza pia kutuletea faida sisi Wakristo. Namna gani? Tunaweza kusimama na kutazama kanuni za Sheria hiyo. Hata kama hatushike sheria hizo, tunaweza kuacha nyingi kati ya hizo ziongoze maisha yetu ya kila siku na ibada yenye tunamutolea Yehova. Ameandikisha sheria hizo katika Biblia ili zitufundishe, ili kanuni za sheria hizo zituongoze, na tumushukuru Yesu kwa sababu alitufundisha jambo fulani kubwa zaidi kuliko Sheria hiyo. Sikiliza maneno yenye Yesu alisema: “Mulisikia kwamba ilisemwa: ‘Usifanye uzinzi [uzinifu].’ Lakini mimi ninawaambia ninyi kwamba kila mutu ambaye anaendelea kumutazama mwanamuke na kumutamani tayari amefanya uzinzi pamoja naye moyoni mwake.” Kwa hiyo, tunapaswa kuepuka kufanya uzinifu, lakini tunapaswa pia kuepuka kuwa na mawazo mabaya na tamaa mbaya.—Mathayo 5:27, 28.

9. Ni hali gani mupya ilifanya Mungu atoe muongozo mupya?

9 Kisha kufika kwa Masiya, ni kusema, Yesu Kristo, Yehova alitoa muongozo mupya na maelezo zaidi juu ya mupango wake. Sababu gani muongozo huo ulikuwa wa maana? Kwa sababu katika mwaka wa 33, alikataa taifa la Israeli na kuchagua kutaniko la Kikristo. Kwa hiyo, hali ya watu wa Mungu ilibadilika tena.

ISRAELI WA KIROHO WANAPEWA MUONGOZO

10. Sababu gani kutaniko la Kikristo lilipewa sheria za mupya, na namna gani sheria hizo zilikuwa tofauti na sheria zenye Waisraeli walipewa?

10 Yehova aliwapatia Waisraeli Sheria ya Musa ili kuwafundisha namna ya kuishi na kumuabudu. Kuanzia wakati wa mitume, Mungu hakuchagua tena watu wake kutoka katika taifa moja tu, lakini aliwachagua kutoka katika mataifa mengi yenye kuwa na desturi mbalimbali, na waliitwa Israeli wa kiroho. Walifanyiza kutaniko la Kikristo na waliongozwa na agano mupya. Yehova aliwapatia muongozo mupya ao wenye kuwa wazi wenye kuonyesha namna walipaswa kuishi na kumuabudu. Kwa kweli, ‘Mungu hana ubaguzi, bali [lakini] katika kila taifa mutu ambaye anamuogopa na kutenda uadilifu [haki] anakubalika kwake.’ (Matendo 10:34, 35) Waliongozwa na “sheria ya Kristo,” yenye ilitegemea sana kanuni zenye kuandikwa katika mioyo yao kuliko kuandikwa juu ya majiwe. Sheria hiyo ingewaongoza Wakristo wote na kuwaletea faida hata kama wanaishi wapi.—Wagalatia 6:2.

11. “Sheria ya Kristo” inazungumuzia sehemu mbili gani za maisha ya Mukristo?

11 Israeli wa kiroho walipata faida kubwa kwa kutii maagizo yenye Yehova aliwapatia kupitia Yesu. Mbele tu ya kuanzisha agano mupya, Yesu aliwapatia amri mbili za lazima. Amri moja ilizungumuzia kazi ya kuhubiri. Amri ingine ilizungumuzia namna Wakristo wanapaswa kutendeana. Wakristo wote walipewa maagizo hayo; kwa hiyo, sisi wote leo tunapaswa kutii maagizo hayo iwe tuko na tumaini la kuishi milele mbinguni ao duniani.

12. Wanafunzi walipewa muongozo gani mupya juu ya kazi ya kuhubiri?

12 Zamani, watu wa mataifa walikuja katika Israeli ili kumutumikia Yehova. (1 Wafalme 8:41-43) Kisha, Yesu alitoa amri yenye kupatikana kwenye Mathayo 28:19, 20. (Soma.) Yesu aliambia wanafunzi wake ‘waende’ kwa watu wote. Kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33, Yehova alionyesha kwamba anapenda habari njema ihubiriwe katika dunia yote. Siku hiyo, watu 120 hivi wa kutaniko mupya walijazwa na roho takatifu na walianza kusema katika luga mbalimbali na Wayahudi na watu wenye waliamini dini ya Kiyahudi. (Matendo 2:4-11) Kisha, wanafunzi hao waliendelea kuhubiri mupaka Samaria. Na katika mwaka wa 36, eneo lao lilipanuka sana kufikia hata Watu wa Mataifa wenye hawakutahiriwa. Hilo lilimaanisha kwamba Wakristo walipaswa kuhubiria kila mutu katika dunia!

13, 14. (a) ‘Amri mupya’ yenye Yesu alitoa ilikuwa na jambo gani lingine? (b) Mufano wenye Yesu alituachia unatufundisha nini?

13 Yesu alitoa pia ‘amri mupya’ yenye kuonyesha namna tunapaswa kuwatendea ndugu na dada zetu. (Soma Yohana 13:34, 35.) Kila siku tunapaswa kuwaonyesha kwamba tunawapenda, na kuwa tayari kutoa uzima wetu kwa ajili yao. Sheria ya Musa haikuomba watu watoe uzima wao kwa ajili ya wengine.—Mathayo 22:39; 1 Yohana 3:16.

14 Yesu alionyesha mufano muzuri zaidi wa upendo huo wa kujitoa. Alikuwa tayari kutoa uzima wake kwa ajili ya wanafunzi wake kwa sababu alikuwa anawapenda sana. Anapenda wafuasi wake wote waonyeshe upendo kama huo. Kwa hiyo, tunapaswa kuwa tayari kuvumilia mateso na hata kufa kwa ajili ya ndugu na dada zetu.—1 Wathesalonike 2:8.

MUONGOZO KWA AJILI YA LEO NA WAKATI UNAOKUJA

15, 16. Tuko sasa katika hali gani mupya, na namna gani Mungu anatuongoza?

15 Yesu amemuweka ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara’ ili apatie wafuasi wake chakula cha kiroho kwa wakati wenye kufaa. (Mathayo 24:45-47) Chakula hicho kinatoa pia muongozo wenye Mungu anapatia watu wake wakati hali zinabadilika. Ni nini inaonyesha kwamba tunaishi katika hali mupya?

16 Tunaishi “katika siku za mwisho,” na hivi karibuni kutakuwa mateso makubwa yenye haijatokeaka. (2 Timotheo 3:1; Marko 13:19) Pia, wanadamu wanateseka sana kwa sababu Shetani na mashetani wake wamefukuzwa kutoka mbinguni na kutupwa katika dunia. (Ufunuo 12:9, 12) Zaidi ya hilo, tunatii amri ya Yesu ya kuhubiria watu wengi zaidi katika dunia yote na katika luga nyingi zaidi kuliko zamani!

17, 18. Tunapaswa kuona namna gani miongozo yenye tunapewa?

17 Tengenezo la Mungu linatupatia vyombo vingi vya kutusaidia katika kazi ya kuhubiri. Unatumia vyombo hivyo? Kwenye mikutano yetu, tunapewa muongozo wenye kuonyesha namna ya kutumia muzuri vyombo hivyo. Unaona kuwa miongozo hiyo inatoka kabisa kwa Mungu?

18 Ili Mungu atubariki, tunapaswa kufuata miongozo yote yenye anatupatia kupitia kutaniko la Kikristo. Ikiwa tunatii tangu leo, tutakuwa tayari kutii miongozo yenye tutapewa wakati wa ‘ziki kubwa [mateso makubwa],’ wakati ulimwengu wote muovu wa Shetani utaharibiwa. (Mathayo 24:21) Kisha, tutakuwa na lazima ya maagizo mapya kwa ajili ya maisha katika dunia mupya yenye haki yenye haitachochewa tena na Shetani.

Katika dunia mupya, tutapewa vitabu vya kukunjwa vyenye kuwa na maagizo kwa ajili ya maisha katika Paradiso (Picha hii inapatana na fungu la 19, 20)

19, 20. Ni vitabu gani vya kukunjwa vyenye vitafunguliwa, na matokeo yatakuwa nini?

19 Taifa la Israeli lilikuwa na lazima ya maagizo mapya wakati wa Musa; ndiyo sababu Mungu aliwapatia Sheria. Kisha, kutaniko la Kikristo lilipaswa kutii “sheria ya Kristo.” Vilevile, Biblia inatuambia kwamba, katika dunia mupya, Yehova atatupatia maagizo mapya kupitia vitabu vya kukunjwa. (Soma Ufunuo 20:12.) Pengine, vitabu hivyo vitatuambia mambo yenye Yehova anapenda tufanye wakati huo. Kujifunza vitabu hivyo kutasaidia watu wote wajue mambo yenye Mungu anapenda wafanye; kati ya watu hao kuna pia wale wenye watafufuliwa. Vitabu vya kukunjwa vitatusaidia kujifunza mambo mengi zaidi yenye kuonyesha namna Yehova anaona mambo. Pia, katika Paradiso tutaelewa Biblia muzuri zaidi; kwa hiyo, tutapendana, tutaheshimia, na kutendeana kwa haki. (Isaya 26:9) Fikiria mambo mengi sana yenye tutajifunza na kufundisha wengine katika utawala wa Mufalme, Yesu Kristo!

20 Ikiwa tunafuata maagizo yenye ‘kuandikwa katika vitabu’ hivyo na kubakia waaminifu kwa Yehova wakati wa jaribu la mwisho, ataandika majina yetu katika “kitabu cha uzima,” na yatabakia milele katika kitabu hicho. Tunaweza kupata uzima wa milele! Kwa hiyo, tunapaswa KUSIMAMA ili kusoma mambo yenye Biblia inasema, KUTAZAMA ili kuelewa maana ya maneno hayo, na KUSIKILIZA kwa kutii muongozo wenye Mungu anatupatia leo. Ikiwa tunafanya hivyo, tutaokoka mateso makubwa na kufurahia kujifunza milele juu ya Yehova, Mungu wetu mwenye hekima na upendo.—Mhubiri 3:11; Waroma 11:33.