Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Kanuni za Sheria ya Musa zilitumiwa kabisa ili kumaliza matatizo ya kila siku ya kukosa kuelewana katika Israeli ya zamani?

NDIYO, wakati fulani. Fikiria mufano huu. Andiko la Kumbukumbu la Torati 24:14, 15 linasema hivi: ‘Haupaswe kumupunja mufanyakazi wa kukodiwa [ao, kulipwa] aliye katika taabu na aliye maskini, awe wa ndugu zako ao wa wakaaji wageni wako walio katika inchi yako . . . ili asimulilie Yehova juu yako, na ikuwe zambi kwako.’

Kipande cha chombo cha udongo chenye kuwa na maandishi ya ombi la mufanyakazi katika shamba

Habari moja yenye kuwa na ombi kama hilo lenye lilifanywa mbele ya mwaka wa 600 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, ilipatikana karibu na Ashdodi. Inawezekana kuwa iliandikwa juu ya mufanyakazi mumoja mwenye kutumika katika shamba mwenye pengine alishindwa kueneza kiasi fulani cha mavuno; maandishi hayo yenye yaliandikwa kwenye chombo fulani cha udongo, yalisema hivi: “Kisha mutumishi wako [mutu mwenye alifanya ombi] kumaliza kuweka mavuno siku fulani zenye zimepita, Hoshayahu mwana wa Shobai alikuja na kuchukua nguo ya mutumishi wako. . . . Wenzangu wote wenye walikuwa wanavuna pamoja na mimi wakati wa jua kali wanaweza kushuhudia . . . kama mambo yenye nimesema ni ya kweli. Sikufanya hata kosa moja. . . . Ikiwa gavana anaona kuwa mutumishi wako hapaswe kurudishiwa nguo yake, afanye hivyo kwa sababu ya huruma! Usibakie kimya wakati mutumishi wako hana nguo yake.”

Mwanahistoria Simon Schama anasema kama ombi hilo “halionyeshe tu mahangaiko ya mulimaji huyo ya kurudishiwa [nguo yake]. Linaweza kuonyesha pia kama mutu huyo alijua jambo fulani juu ya sheria yenye kuwa katika Biblia, zaidi sana amri zenye kupatikana katika Walawi na Kumbukumbu la Torati zenye kukataza kumutendea mubaya mutu maskini.”